Kamanda wa Kweli
JF-Expert Member
- Jul 13, 2014
- 1,448
- 847
Tatizo Sio Kuitoa CCM Madarakani.Tatizo Ni Kua Hakuna Mbadala Wake.Kama Watu Wao Wa Karibu Na Waasisi Wa UKAWA Wameshindwa Kuwaamini.Basi Hata Sisi Hatuwaamini.
Bora nife kuliko nichague chama cha majizi (CCM) wale wale waliopiga escrow, meremeta, EPA, rada, Richmond hii inamuhusu Sana Baba yenu. CCM haufai hata kwa dawa, mnaiba wanyama, meno ya tembo na pembe za ndovu na kuziuza nje !! Huku si wanyonge tunaendelea kutaabika!! Unasign mikataba mibovu ya mafuta na gesi kwa manufaa ya tumbo zako!! Huku elimu duni katika tiba ndiyo usinene!! Rip Ccm chama cha vibaka wa Mali ya ummaMhe.Mbowe Jiandae Kuwajibika Katika Hili Kwa Watanzania.
Mpasuko Unaoendelea Sasa Katika UKAWA Ni Matunda Ya Maamuzi Yako Mabovu Yaliyokosa Ridhaa Ya Pamoja Ya Viongozi Wenzako.Maamuzi Yako Yaliyokua Na Lengo La Kuwaburuza Viongozi Wenzio Kifikra Na Kimaamuzi.Na Maamuzi Yako Yaliyofishwa Na Tamaa Yako Ya Uroho Wa Madaraka Na Kukubali Kununuliwa.
Kitendo Cha Kumkaribisha Fisadi Papa No.1 Mhe.Lowassa Ndani Ya UKAWA Na Kupewa Nafasi Ya Kuteuliwa Kama Mgombea Uraisi Bila Ya Maridhiano Thabiti Kutoka Kwa Viongozi Wenzio.Kumekufanya Wewe Uwe Fisadi Papa No.11(Haukuwepo Kwenye Listi Ya Awali Ila Sasa Upo).Na Watanzania Wanatakiwa Kukuogopa Kama Ukoma.Kwa Kuweka Maslahi Yako Mbele Kuliko Maslahi Ya Taifa.
Kama Bado Unaamini Kua Kuondoka Kwa Dr.Slaa Na Prof.Lipumba Ndani Ya UKAWA Hakuna Madhara Yeyote kwa UKAWA.Basi Ukae Ukijua Kua Uko Ni Kujidanganya Na Kujilisha Upepo.
Malipo Ya Usaliti Huu Kwa Viongozi Wenzio
Yatakua Ni Kuanguka Kwako Mwezi October Na Kuporomoka Kwako Kisiasa.Na Ujiandae Kwa Aibu Kubwa
huwezi kuziongelea siasa za tanzania bila kulitaja
jina la freeman mbowe.
Mbowe ni kati ya wanasiasa ambao wanaishi katika
misingi ya siasa za kibiashara.
He is businessman turned politician and he's not shy
away from controversy. He thrives on political
controversy and challenge.
Mbowe haiangalii siasa katika jicho la kubadilisha
maisha ya wananchi kwenye msingi wa hasara.
Ni kati ya watu ambao wako tayari kubadirika wakati
wowote kutokana na mazingira ya kisiasa katika
mlengo wa faida ya kisiasa bila kujali ni nani ataumia
na maamuzi yake.
Moja ya uwezo wake mkubwa ni kuwakaanga kisiasa
wale wote ambao wanaweka uzio wa kupata biashara
ya kisiasa kwa mlengo wa faida.
Kuna wakati hakusita kuhudhuria dhifa iliyotayalishwa
na rais kikwete kwa ujio wa rais obama na
wafanyabiashara wakubwa wa marekani pamoja na
kwamba, serikali ya rais kikwete ilikuwa ni shetani
katika macho ya baadhi ya viongozi wa chadema.
Mbowe alihudhuria kwa sababu kulikuwa na faida ya
kibiashara. Wanazi walipiga kelele lakini mbowe yupo
mpaka leo.
Zitto alileta kizingiti cha kisiasa katika siasa za faida
ndani ya chadema, aliishia kuvuliwa cheo na
kufukuzwa ndani ya chadema.
Mbowe baada ya kunusa faida ya kisiasa
itakayopatikana kama atamteua lowassa kuwa
mgombea urais kwa tiketi ya chadema, hakusita
kumwambia dk. Slaa akae kando pamoja na kwamba
kamati kuu ya chadema ilikuwa imemteua awe
mgombea urais kwa tiketi ya chadema. Dk. Slaa
akazira na ''kuingia mitini'', lakini mbowe hakutikisika
katika uamuzi wake, wakati huo huo dk. Slaa
akaonekana kwa baadhi ya wana chadema kama
mpinga mabadiliko.
Haitashangaza kumuona akirudi
tena ofisini baada ya kugundua kina kirefu cha
kisiasa.
Kwa kutambua ulafi wa prof. Lipumba kwenye
ugombea urais, mbowe alimwacha prof. Lipumba
ajikaange mwenyewe mbele ya waaandishi wa habari
kwa kumsafisha lowassa bila kutambua kama
anayemsafisha ndiye baadaye atachukua nafasi ya
urais anayodhani ni yake ndani ya ukawa.
Kufumba na kufumbua, prof. Lipumba akajikuta yuko nje ya
matamanio yake na mbaya zaidi, hakufahamu kama
katibu wake mkuu, maalim seif pia amemgeuka
baada ya kuongea na mbowe. Akajiuzuru uwenyekiti
na kuondoka nchini wakati huo huo akaonekana kwa
wana cuf kama ni msaliti wa mageuzi.
Mbowe ni mwalimu mzuri sana katika siasa za
tanzania zilizojaa wanafiki. Ni mtu anayeongea na
mtu yoyote kama anadhani kuna maslahi katika
maongezi.
Ni kati ya mmoja wa wanasiasa ambao
hawana marafiki wa kudumu au maadui wa kudumu.
Zitto, dk. Slaa na prof. Lipumba hawawezi
kuyasahau maamuzi ya mbowe katika maisha yao.
Ukawa mnajidanganya kwa kujilisha upepo. MTU aliyekataliwa upande mwengine mnajiaminishaje kuwa anafaa upande wenu? Kwa misingi IPI? Name kwa itikadi zipi? Na akishindwa uchaguzi mtakuwa nae tayari kusimamia yale mnayoamini kama chama?
Mmekurupuka sana Ila November 2015 mwisho wenu.
Kama Mpaka Leo Bado Hujui Kama Mbowe Kanunuliwa.Basi Lazima Wewe Utakua Ni Mpumbavu Wa Mwisho.
Na Hata Huyo Lowassa Kama Yeye Sio Fisadi Na Hakuusika Na Kashfa Ya Richmond Kwanini Alikubali Kujiuzulu?.Na Vp Km Angeteuliwa Kua Mgombea Wa Uraisi Wa CCM Angeyazungumza Yale Aliyoyazungumza.
Lowassa Ni An "Opportunistic Politician" Na Yuko Kimaslahi Yake Binafsi.Na Vilaza Kama Ww Ndo Mnaomshabikia.Lakini Binadamu Mwenye Akili Timamu Hawezi Kumsupport Lowassa.
Sijataka kufikiriwa. ..ninalo sema ni ukweli mtupu. .lazima tupate viongozi watakao kuwa na huruma na taifa na wananchi wake, awe mbowe ama kingwendu lakini isiwe Ccm mana imelewa madaraka sasa
Mwambie anaacha yake anaangaika na jirani.kwanini unajidhalilisha kwa kasi kubwa hivi ? umerogwa na nani ? au kwenu mnagombea nyumba ya urithi wanataka ugongwe na gari ili wafaidi wenyewe ?
skendo ya buzwagi iliipaisha sana chadema, kipindi cha zitto hicho. baada ya zitto kusimamishwa bunge kwa muda walizunguka nchi nzima kutoa elimu kwa wananchi kuhusu skendo ya buzwagi.
uhusika wa kalamagi na waziri mkuu lowasa ulielezwa vizuri bungeni na mikutanoni. kalamagi alibeba mihuri ya serikali kwenye briefcase akaenda saini mkataba kwa niaba ya serikali hotelini London, waziri mkuu lowasa nae alijipelekea london akaweka kambi hoteli jirani na hotel aliyofikia kalamagi na wawekezaji hao. wao wajua vyema walichoongea/peana huko ila kalamagi alirudi na mkataba umeshafungwa. mbowe alilisema hili majukwaani nchi nzima.
waziri mkuu wamruhusu waziri wako atie mihuli kwa begi aende hotelini nje ya nchi kufunga mkataba kwa niaba ya serikali. haikutosha akajipeleka mwenyewe London - na kumbukumbu za ofisi ya waziri hazikuonesha kwamba waziri mkuu alienda london kiserikali, pia hakuwa likizo.
leo hii mbowe kabadilika anatuhubiria kwamba lowasa anayesaidiwa pesa na kalamagi ndiye tumaini jipya la watz, atatuvusha na kutufutia umaskini. aenda mbali zaidi na kusema hana kashfa yeyote.
mbowe adhani siye watz ni wasahaulifu sana, afikiri twamjua lowasa kwa richmond tu. twajua mengi mbowe.
kalamagi sasa ndo mfadhili mkubwa wa lowasa - ambaye ukawa watwambia akiingia ikulu atafuta ufisadi.
tutafakari zaidi watz wenzangu. kwa ufupi naweza sema anachokifanya mbowe ni unafiki,unafiki na unafiki.