Mbowe amkaribisha rasmi Lowassa CHADEMA

Mbowe amkaribisha rasmi Lowassa CHADEMA

Na kama ndiyo hivyo sina sababu ya kujiandikisha kupiga kura!Ili iweje?Nampigia kura fisadi,mwizi wa mali za umma,mla rushwa asiye na haya mpaka kutaka kununua urais?

Hivi hawaoni huyu aliyemsaidia kuununua urais ametufikisha wapi?

Kweli wakimuingiza CDM waisubirie kadi yangu huko huko ufipa.

Nikisema unanitukana,CDM imeshawakaribisha wawekezaji wapya teh teh na wale kwa sasa ndo wana maamuzi ya wapi chama kinaenda hata jina la mgombea wenu limekwama kisa jamaa wenye chama wametia maguu! Njaa mbaya sana! Wawekezaji kwanza Wanachama keshokutwa!chezea hela weye!
 
mkuu tulia kwanza yapo mawili yatakukuta mwaka huu
1, kumtangaza waziwazi ili tuchanje mbuga kweda ikulu au
2, kutumia pesa zake na wewe ukiwemu kwenye kampaini zao na malipo yake nafasi ya uwaizri mkuu au bihashara,

hakuna namna ya kuyakwepa haya maana makubaliano tayari japo kwa siri sana lakini ukweli haufichiki,maamuzi makuu ni ya wenye chama mtu na mkwe wake basi,
na kimia hiki kinasoma upepo,lakini hakisaidi wala hakitabadilisha yaliyopangwa,

Hiki Chama siyo cha Mbowe,Mtei wala Dr.Slaa.Chama hiki kinaweza kumshtaki yeyote katinyao atakayeenda kinyume na katiba ya chama

Ninategemea hata wanachama wa kawaida wanaweza kuweka court order kupinga kukaribishwa kwa Lowassa.Ni kiasi cha kuulizia wanasheria.

Kama walianzisha chama ili kiwe cha familia wasingekuwa na haja ya kutafuta wanachama.

Na mwisho waanzilishi wa CDM siyo Mtei peke yake hivyo hana mandate ya kusema chama ni chake.

Walioanzisha wapo usipoteze watu.Na si Mtei wala Mbowe mwenye uwezo wa.kulazimisha kupokelewa kwa Lowassa.Kionhozi wangu ulimi labda uliteleza akajiuma....
 
alishindwa kuonxoa rushwa,wizi na ufisadi kwenye wizara yake.alihusika kuuza nyumba za serikali na.kugawa kwa hawara yake.hata uniambiaje nitakujibu nilivhojibu.

Huyu ni mbwa mwitu amevaa ngozi ya kondoo.na ukitaka kuwa thomaso kuwa tu lakini
tunaye mfahamu hafai hata kutuchungia kuku.

Kilicho tokea ndani ya chungu huwezi jua kulikuwa na nini kwenye jiko.ukiona maharage yameiva ujue mkaa umeteketea.

mkuu hachana na poroja za wanafiki wa siasa ,katika wizara ambayo haina wizi ni pamoja na wizara ya ujenzi,tafuta mkandarasi yeyote muulize atakwambia ukweli
pili,
hakuna ambapo waziri anatoa kibali cha kuuza mali za umma,aliyetoa kibali hicho ni mkapa baada ya serikali kushidwa kutoa pesa za kufanya matengenezo ya nyumba hizo,

hii ni sawa na aliposema magari nyenye uzito mkubwa yasipite kwenye barabara pinda akaja juu na kumwambia akae kimia yeye kama waziri angefanyaje? Au ngekuwa wewe ungefanyaje?

 
I love U ghafla!!
Unaweza kunijibu hili?Kwanini alikuwa analipa watu pssa kwa ajili ya kumchagua?Rafiki huyo tuliyenaye alipita njia hizo hizo alizokua anapita rafikiye!Ila tatizo ni kuwa rafikiye amempenda mwingine achukue mikoba yake!

Lakini njia alizopita ndizo alizopita ndizo hizo hizo za.kulipa na kutoa rushwa ili apate uongozi.Tofauti hawana.ila mimi na wewe tujiulize atarejeshaje pesa alizokopa kwa ajili ya kusaka urais?

Uzuri ananua njia aliyotumia kutaka kuteuliwa ziyo sahihi.Asi getoa pesa nina uhakika asingekuwa na sababu ya kuukosa.

Leo tunalia mikopo imezidi imefika mahali hayujui kama italipika.Cha maana bakuna bali safari za kila siku,mikopo hii haijalipa mikopo iliyochukuliwa wakati wa kusaka uongozi?

Sina ubaya a Lowassa wala kwa yeye kuwa mwanachama wa chama chochote cha siasa,lakini sitakuwa na amani kwa chama chochote cha siasa kikimsimamisha kugombea urais.

Sina uhakika hata ubunge kama itawapa chama hicho.Kwangu TAIFA langu ni bora kuliko chama.Chama chweza kufa lakini si TAIFA langu.

Huu ndiyo msimamo wangu.
 
hiki chama siyo cha mbowe,mtei wala dr.slaa.chama hiki kinaweza kumshtaki yeyote katinyao atakayeenda kinyume na katiba ya chama

ninategemea hata wanachama wa kawaida wanaweza kuweka court order kupinga kukaribishwa kwa lowassa.ni kiasi cha kuulizia wanasheria.

Kama walianzisha chama ili kiwe cha familia wasingekuwa na haja ya kutafuta wanachama.

Na mwisho waanzilishi wa cdm siyo mtei peke yake hivyo hana mandate ya kusema chama ni chake.

Walioanzisha wapo usipoteze watu.na si mtei wala mbowe mwenye uwezo wa.kulazimisha kupokelewa kwa lowassa.kionhozi wangu ulimi labda uliteleza akajiuma....

kamuulize slaa kilichomkuta ndo utajua nani mwenye chama
 
Hiki Chama siyo cha Mbowe,Mtei wala Dr.Slaa.Chama hiki kinaweza kumshtaki yeyote katinyao atakayeenda kinyume na katiba ya chama

Ninategemea hata wanachama wa kawaida wanaweza kuweka court order kupinga kukaribishwa kwa Lowassa.Ni kiasi cha kuulizia wanasheria.

Kama walianzisha chama ili kiwe cha familia wasingekuwa na haja ya kutafuta wanachama.

Na mwisho waanzilishi wa CDM siyo Mtei peke yake hivyo hana mandate ya kusema chama ni chake.

Walioanzisha wapo usipoteze watu.Na si Mtei wala Mbowe mwenye uwezo wa.kulazimisha kupokelewa kwa Lowassa.Kionhozi wangu ulimi labda uliteleza akajiuma....

Duu hivi bado tu huelewi Katiba ya chama kitu gani?M/kiti kaivuruga kwa makusudi ili aendelee kuwepo na kuathiri maamuzi yule ni mfanya biashara ndo ujue keshakaribisha wawekezaji wenye hela teh teh teh WENYE CHAMA NDO WANAAMUA WENGINE MSIOTAKA AU KUKUBALIANA NA MAAMUZI YA WAMILIKI MUONDOKE!!!
 
Hiki Chama siyo cha Mbowe,Mtei wala Dr.Slaa.Chama hiki kinaweza kumshtaki yeyote katinyao atakayeenda kinyume na katiba ya chama

Ninategemea hata wanachama wa kawaida wanaweza kuweka court order kupinga kukaribishwa kwa Lowassa.Ni kiasi cha kuulizia wanasheria.

Kama walianzisha chama ili kiwe cha familia wasingekuwa na haja ya kutafuta wanachama.

Na mwisho waanzilishi wa CDM siyo Mtei peke yake hivyo hana mandate ya kusema chama ni chake.

Walioanzisha wapo usipoteze watu.Na si Mtei wala Mbowe mwenye uwezo wa.kulazimisha kupokelewa kwa Lowassa.Kionhozi wangu ulimi labda uliteleza akajiuma....
Hapo umesema,kama kweli watamkaribisha Lowassa CHADEMA, suluhisho si kurudisha kadi bali ni kupambana kwa kufuata taratibu na kanuni za chama na kumpigia kura ya kutokuwa na imani na Mwenyekiti,basi.So far namwamini zaidi Dr Slaa kuliko Mbowe.
 
Nikisema unanitukana,CDM imeshawakaribisha wawekezaji wapya teh teh na wale kwa sasa ndo wana maamuzi ya wapi chama kinaenda hata jina la mgombea wenu limekwama kisa jamaa wenye chama wametia maguu! Njaa mbaya sana! Wawekezaji kwanza Wanachama keshokutwa!chezea hela weye!

Kwa sababu mmezoeamkuhongana mnadhani wote wanakubali kuhongwa?Hivi nikuulize Mwenyekiti wako anaouwezo wa kumnyooshea Lowassa kidole?

Hivi huo utajiri wa Lowassa si ndiyo ulimuingiza Mwenyekiti wako Madarakani?

Alipokuwa anasaidiwa kuununua urais hakuwaza utajiri wa Lowassa aliupatabwapi?

Nachelea kukwambia alichokifanya Mwenyekiti wamo miaka kumi iliyopita ndiyo kinatutesa leo.Tunajua wazi kama si Mapenzi yake kwa mdogo wake Maembe,leo Lowassa angekuwa anapeperusha bendera CCM.

Usichokijua usikiseme.Na wala huna haki wala mandate ya kuwasema CDM...Ikiwa mfumo.mbovu uliowekwa na CCM ndiyo uliotufikisha hapa.

Leo tumeletewa mbuzi kwenye gunia!Eti na Makomeo naye ni malaika,haya nyumba za serikali alizouza na nyingine kugawa kwa ndugu na marafiki zake?

Huyu aliyeshindwa kuuondoa rushwa,wizi,ubadhirifu wa mali za umma,ufisadi kwenye Wizara yake leo tunaaminishwa eti ataweza kuivusha bongo.

Huyu aliyeapa kuilinda CCM pamoja na uongozi uliopita mnatuhadaa eti ndiyo bora.

Samahani tunahitaji Upinzani madhubuti,imara unaoweza kujipambanua na ukisema unachukia rushwa na ufisadi basi nje na ndani waonekane hivyo.Kutoka kwa kiongozi mpaka mwanqchama wa kawaida.

Tunapiga kelele humu JF ili hata wale wabunge waliopotoka kwa kutaka kumchukua huyo fisadi warudi nyuma wanitathmin,vinginevyo wakaage bungeni kabisa.

Tunaweka UTAIFA kwanza na si chama.Kama unadhani tunaweka chama kwanza kama mfanyavho huko ndani ya CCM siyo sisi huku.
 
kamuulize slaa kilichomkuta ndo utajua nani mwenye chama

Hakuna chochote kilicho mkuta.Unadhani huku ni CCM baba,mama na watoto wote w nec?Unadhani hatujui kilichokuwa kinaendelea kwamba mwenyekiti wako alikuwa anataka kaka yake awe rais?Kli akitoka na mtoto naye awe rais?Au sijui ndiyo maana lastlady anautaka ubunge ili aje kuwa waziri wa mambo ya nje!!!!.Tunajua kilichotokea ndani kanone,usitake tukamwaga mtama kwenye kuku wengi.

Mengine usiwe unaropoka tunajua mengi zaidi ya ujuavyo.Usitupe mawe ukiwa ndani ha nyumba ya vioo.

Pole tunabisha kwa hoja na si vihoja kutengeneza Taifa bila upinzani wenye nguvu Taifa letu liko kwenye hati hati ya kumalizika kabisa.
 
Binafs sina tatizo Lowasa ila awe mwanachama km mimi. Mwacheni mzee wa watu apumzike kwani hajauwa.
 
Lowassa kuja na na best yke chenge chadema,,,,rostam nae yuko njiani mwaka huu ukawa tumejipanga...
 
Hapo umesema,kama kweli watamkaribisha Lowassa CHADEMA, suluhisho si kurudisha kadi bali ni kupambana kwa kufuata taratibu na kanuni za chama na kumpigia kura ya kutokuwa na imani na Mwenyekiti,basi.So far namwamini zaidi Dr Slaa kuliko Mbowe.

Umenifurahisha mahali nilipokuwa nimekasirika.Anyway hiyo kura unaipigia wapi?Mie ni mwanachama wa kawaida kabisa.Na ninasemea moyo wangu sababu naipenda sana nchi yangu.

Nimesikitishwa na baadhi ya mawazo ya wabunge wa CDM ya kumkaribisha Lowassa,hivi CDM imekuwa depsrate kiasi cha kutafuta mafisadi kuwa wagombea wa urais?

Hivi CDM hakuna presidential material mpaka tupate pumba toka CCM?Maan bora pumba ya mahindi ya mpunganile inayotumika kuchomea matofali huko kwetu.

Hivi Mbowe anajua ukaribisho wake maana yake nini kwa chama na watanzania?

Hivi Mbowe ametuona watanzania wapumbavu mno kiasi kwamba akisema chochote basi tutapiga makofi?

Kama hajui basi ningependa kumwambia CDM siyo taasisi yake anaweza kufukuzwa vile vile akaiacha.

Ila swali langu kwako mie kama mie naenda kupiga wapi kura ya kutokuwa na imani na mwenyekiti?

Ninachompendea Dr.Slaa anasimamia uamuzi wake.Na akiondoka hakika Mbowe ajue atabaki na yale makabrasha yake ampelekee Mtei.Ila ka.a atatuelewa akamwambie Mtei Taifa kwanza chama baadaye.Chama kwanza Lowassa baadaye.

Kama Mbowe hajui CDM ina nafasi gani kwa watanzania ni bora ajiuzulu apishe wengine.

Ni mmachame mwenzangu kwa hili sitomuunga mkono kamwe.

Kaka ni bora Taifa kuliko chama.Chama kitakufa lakini si Taifa.Ni Chama kwanza Lowassa baadaye.

Bila Lowassa CDM inaweza.
 
Unarudisha kadi wewe mmoja madiwani sabini wanachukua kadi...huma utakacho tupunguzia....huenda na wewe ukawa kama zitto tu tena itakuwa bora kwetu

mkuu kama hii habari ni ya kweli mtakua sasa mmeanza kuvimbiwa!! huyu jamaa si wenyewe ndo mlimuandika kwenye ile list of shame?
 
Back
Top Bottom