Ni leo nimepata kuona habari mitandaoni na magazetini kuwa Mh mbowe katoa kauli ya kumkaribisha Aliyekuwa waziri mkuu wa zamani Edward Lowasa kujiunga na chama chetu pendwa chadema.
Awalli sikutaka kuamini na bado sijaamini kuhusu hizi fununu,na kama ni kweli, namtaka Mh Aikael Freeman mbowe atoe maelezo fasaha amemkaribisha lowasa aje kufanya nini? Sote tunamjua Lowasa na tuhuma nzito za kifisadi, tuna mfahamu vizuri Lowasa na kundi lake la mbwa mwizi linalomzunguka.
B inafsi simkatai lowasa kama binadamu bali napinga tabia yake ya uwizi rushwa, uroho na ubinafsi.
Natahadharisha kusema kuwa CHADEMA tunaipenda toka moyoni ndio maana hatutingishiki na sunami za ccm kwa kuwa tunaamini Chadema ni chama safi na chenye uhakika wa kutuletea mabadtiko chanya kwa taifa. Kwa nilivyoona kauli hizi ni dhahiri chama kinaenda kuanguka kwa kuwakatisha tamaa wananchi.
Lowasa ni nani ktk chadema, cjama kimeimarika vya kutosha nila uwepo wa lowasa, nini mnachotegemea kwa Lowasa kwa sasa, ccm imemuona hafai ikamtema wewe unamkaribisha bila hata aibu, unataka kutuaminisha kuwa nyie ni maswahaba? Kama ndivyo iweje ccm tuinyoshee mkono?
Mh Mbowe umetukera sana sinaamani kabisa hadi uje utupe ufafanuzi zaidi nini maana yake.