Umenifurahisha mahali nilipokuwa nimekasirika.Anyway hiyo kura unaipigia wapi?Mie ni mwanachama wa kawaida kabisa.Na ninasemea moyo wangu sababu naipenda sana nchi yangu.
Nimesikitishwa na baadhi ya mawazo ya wabunge wa CDM ya kumkaribisha Lowassa,hivi CDM imekuwa depsrate kiasi cha kutafuta mafisadi kuwa wagombea wa urais?
Hivi CDM hakuna presidential material mpaka tupate pumba toka CCM?Maan bora pumba ya mahindi ya mpunganile inayotumika kuchomea matofali huko kwetu.
Hivi Mbowe anajua ukaribisho wake maana yake nini kwa chama na watanzania?
Hivi Mbowe ametuona watanzania wapumbavu mno kiasi kwamba akisema chochote basi tutapiga makofi?
Kama hajui basi ningependa kumwambia CDM siyo taasisi yake anaweza kufukuzwa vile vile akaiacha.
Ila swali langu kwako mie kama mie naenda kupiga wapi kura ya kutokuwa na imani na mwenyekiti?
Ninachompendea Dr.Slaa anasimamia uamuzi wake.Na akiondoka hakika Mbowe ajue atabaki na yale makabrasha yake ampelekee Mtei.Ila ka.a atatuelewa akamwambie Mtei Taifa kwanza chama baadaye.Chama kwanza Lowassa baadaye.
Kama Mbowe hajui CDM ina nafasi gani kwa watanzania ni bora ajiuzulu apishe wengine.
Ni mmachame mwenzangu kwa hili sitomuunga mkono kamwe.
Kaka ni bora Taifa kuliko chama.Chama kitakufa lakini si Taifa.Ni Chama kwanza Lowassa baadaye.
Bila Lowassa CDM inaweza.