Mbowe amkaribisha rasmi Lowassa CHADEMA

Mbowe amkaribisha rasmi Lowassa CHADEMA

Kama maneno haya ni ya kweli basi Chadema nao wanaenda kusambaratika kama ilivyo CCM, Mbowe kwa kumkaribisha maalun huyu Chadema inagawanyika sasa hivi. Mlisema ananuka rushwa leo mmempaka pafyumu gani hadi anukie vizuri? Eti eti mnamwambia ni chama cha watanzania wote basi wakaribisheni akina Chenge, Prof Muhongo, Karamagi, Ngeleja, Rostam na wengine kwa kuwa Chadema ni chama cha Watanzania wote Mbowe please usituharibie chama.

Kwani lowassa kuchukua kadi ya chadema na kua mwanachama wa chadema tatizo nn?mbona mnacomplicte ujinga tu?
 
Lowassa kuingia CDM si shida, ili awe mwanachama wa kawaida kama wengine, na si kwa sababu ya kutaka uongozi.
 
Chadema wakimpitisha lowasa kua mgombea wao basi washaau kura yangu...sasa qakiingia madarakani uyo rostam atashugulikiwa vipi..unafki..na yy lowasa je.. bora umpigie kura lowasa akiwa Ccm kwa kua uko ndo penye sifa zake..huku ni kumpenda Mungu huku ukijilinda na Waganga wa jadi
 
Mwache Aje Ila Awe Mwanachama Wa Kawaida Na Atubu Na Aungame Dhambi Zake Atasamehewa
 
Kwa Tangazo hilo, kama kichwa cha habari cha Gazeti la Tanzania Daima , kinavyoonesha leo, Chadema imegeuka kambi rasmi ya mafisadi waroho wa madaraka....huko wanaenda kwa ajili MOJA TU, kugombea nafasi za Uongozi....hakuna UKOMBOZI, Maslahi yanatawala
 
Mie sioni haja ya kuwa na hasira. Ooh! Ntarudisha kadi kwa manufaa ya nani sasa? Hivi hayo mnayowaza mnadhani wao hawajalitazama hilo??!! Wapeni nafasi ya kujieleza kwann wanampokea Lowassa !!!

Mimi naona shida yao itakuwa ni kuongeza mtaji wa wapiga kura na si vinginevyo na mtu mwenyewe waliyemuona kuwa anaweza akaja na mtaji mkubwa wa wapiga kura ni Lowassa.
 
Kumbuka ndio huyo mungu tulikesha tukimwomba na lowassa akakatwa na ccm lakini kabla walitukebehi kama wewe unachofanya sasa hivi na pesa yote waliotumia lakini bado akashinda aliyetumia hata 10mil haifiki

Ulikesha wewe kumuomba huyo mungu wako, mimi mpaka leo namuomba MUNGU wangu alete mabadiliko TZ
 
Masikiniii Slaa, ndiyo basi tena maana nakuhurumia utaweka wapi sura yako ikiwa Mbowe na Mtei wameshaamua kumuuzia chama fisadi Lowasa!
 
Mimi naona shida yao itakuwa ni kuongeza mtaji wa wapiga kura na si vinginevyo na mtu mwenyewe waliyemuona kuwa anaweza akaja na mtaji mkubwa wa wapiga kura ni Lowassa.

Sasa bila wingi wa kura utapataje ushindi, maana mnajua kabisa CCM wanavyopataga kidogo halaf wanaiba kuongezea ziwe nyingi....
 
Mwenyekiti wa CHADEMA taifa mh. Freemam Mbowe amemkaribisha Lowassa kujiunga na CHADEMA hakibagui mtu ili mradi tu afuate kanuni na taratibu za chama.

Source: Tanzania Daima, Mwananchi

Haki ya mama hiki chama cha Mbowe ni cha malaghai!!
 
Mzee Mtei na Ndesamburo wana imani kwa lowasa kuliko babu Slaa

SLAA ni muiIRAQ asili yake ni kutoka Eritrea , mmeru na mchaga ni mtu na binamu yake. Dr SLAA sio mla rushwa hali luwasa ni Mr 20%, hapo mchaga atamkaribisha nani
 
mbowe mwaka huu unafiki wenu wa mwembeyaga watanzania wataujua raismi ,kuwa nyie ni wanafiki,mlimuvua nguo lowasa mchana kweupe leo hii mnamkalibisha kweli ,siasa ni ujinga mtupu,
 
Wapinzani/wanamabadiliko wawe wakweli kwa nafsi zao,tokeni nje ya box.CCM ni mfumo,hiyo ndo tatizo letu.Tunataka kubadili mfumo huu wa ukoloni mweusi.Shida siyo watu. Dr J.Pombe,Mh Lowasa,Mh Samia Suluhu si tatizo,shida ni CCM.Nje ya CCM hao ni watu safi.
Kama Lowasa anaweza kuleta ushindi akigombea kupitia upinzani kwa kuwa anao wapenzi/wapiga kura wengi,CDM Hanna budi kumkaribisha ili tuweze kubadili CCM.Lowasa haji kwa taratibu na kanuni toka nyumbani kwake,ATANADI SERA za Chama husika.Acheni uhafidhina wa kivyama,tusikaririshwe matukio.Siasa na mfumo unaoishi,hubadilika kutegemeana na mahali & wakati. Tujadili katika ukweli,tuache kutegemea miujiza.
 
SLAA ni muiIRAQ asili yake ni kutoka Eritrea , mmeru na mchaga ni mtu na binamu yake. Dr SLAA sio mla rushwa hali luwasa ni Mr 20%, hapo mchaga atamkaribisha nani

slaa alimvua ngua na kunchafua lowasa mchana kweupe mwembeyanga leo hii eti anamkalibisha nafsi inamsuta,japo apendi lakini atafanyaje yupo kwenye saccss ya watu,pole sana kibabu SLAA,UNAFIKI UNAMWISHO NA YAMEMKUTA SASA,WATANZNAIA TUMJUE HUYU BABU NI WA AINA GANI,

 
jamani kama mlifwatilia taarifa ya mzee Wa zamani Wa ccm mngeelewa vizuri kashfa ya lowasa imetokana na nn ndo mngeelewa ni fisadi au la
 
Ulikesha wewe kumuomba huyo mungu wako, mimi mpaka leo namuomba MUNGU wangu alete mabadiliko TZ
Wangu nilimwomba na majibu akawa kama nilivyoomba jina la fisadi likakatwa, mabadiliko hayawezi kuletwa na fisadi lowassa na team yake ya akina Rostam, mengi, karamagi, chenge, Tibaijuka. Mabadiliko ya kweli yataletwa na kizazi cha viongozi wasiokula rushwa na wasio na tamaa ya madaraka. Naomba uendelee kuomba mabadaliko ili tupate viongozi wasio na uchu wa madaraka kama lowassa.
 
Back
Top Bottom