Mbowe ameshakosa sifa ya ubunge mahakamani!

Mbowe ameshakosa sifa ya ubunge mahakamani!

Chenge alihukumiwa kufungwa miaka mitatu au kutoa faini, na alitoa faini, hakupoteza ubunge.

Soma hapa:
Hatima ya Ubunge wa Chenge baada ya hukumu

Kama sheria ilitekelezwa hivyo kwa Chenge, inapaswa kutekelezwa hivyo kwa wote.

Tatizo ni uwezo mdogo wa ubongo wako. Tofautisha kati ya CRIMINAL CASE na TRAFFIC CASE. ndio utajua kati ya kesi hizi ipi inamnyima mtu haki za kugombea.
 
Tatizo ni uwezo mdogo wa ubongo wako. Tofautisha kati ya CRIMINAL CASE na TRAFFIC CASE. ndio utajua kati ya kesi hizi ipi inamnyima mtu haki za kugombea.
Sheria inasema:

Ibara ya 67
(2) Mtu hatakuwa na sifa za kustahili kuchaguliwa au kuteuliwa kuwa Mbunge-
(c) ikiwa mtu huyo amehukumiwa na Mahakama yoyote katika Jamhuri ya Muungano na kupewa adhabu ya kifo au ya kufungwa gerezani kwa muda unaozidi miezi sita kwa kukutwa na hatia ya kosa lolote, vyovyote linavyoitwa





 
Ahsante mkuu kwa kudadavua zaidi.....Mbowe amelipa faini....hii ina maana kuwa kipindi chake cha kutumikia adhabu kwa mwaka mmoja inahesabiwa. Kama hivyo ndivyo je anayo haki kikatiba ya kuchagua na kuchaguliwa katika nafasi yoyote kitaifa. Naamini hutakwazwa na maswali yangu

Kamuulize Rage atakwambia
 
Tatizo ni uwezo mdogo wa ubongo wako. Tofautisha kati ya CRIMINAL CASE na TRAFFIC CASE. ndio utajua kati ya kesi hizi ipi inamnyima mtu haki za kugombea.
Wewe mwenye uwezo mkubwa wa ubongo tuwekee vifungu hivyo vya sheria.
 
Wewe ndio umeongea point.
Kosa la kuhukumiwa kwa kutokuwa mwaminifu ndio lingemzuia,ila la kumshikisha adabu mwizi sio kikwazo.
Precedence ya mtikila Yeye alienda jela 1 year kwa uchochezi. Hakuwa na faini. Na aligombe urais. What matters, kwa katiba ya sasa.. mtikila hakufungwa jela/ wala mbowe hakuhukumiwa kwa utovu wa uaminifu; kwa kukwepa kodi wala kwa kuvunja maadili ya viongozi wa umma. precedence ya mtikila kwa lugha nyepesi ilitengeneza sheria ambayo inabidi ifuatwe kisheria inaitwa case law
 
Utata wa kupoteza sifa ya kugombea

Hukumu hiyo iliibua mjadala mkali kwenye mitandao ya kijamii juu ya uwezekano wa kumzuia Mbowe ambaye pia ni Kiongozi wa Upinzani Bungeni kuwania tena ubunge au urais katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba.

Hata hivyo, Mwanasheria, Alex Mgongolwa akinukuu Katiba ya Tanzania Ibara ya 67 (1)(c); 67(2) (c na d) alisema hukumu hiyo haiwezi kumzuia kugombea ubunge kwa sababu hakwenda jela na kosa lake halihusu kukosa utovu wa uaminifu, kukwepa kodi wala kuvunja Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma.

Suala hilo linafanana na lililotokea katika mchakato wa uteuzi wa wagombea urais mwaka 2005 wakati aliyekuwa mgombea urais wa DP, Mchungaji Christopher Mtikila na mgombea mwenza wake, Saidi Soud Said walipowekewa pingamizi kutokana na kutumikia kifungo jela, Mtikila akitumikia mwaka mmoja kwa kosa la uchochezi, Said akitumikia chuo cha mafunzo kwa kosa la biashara ya vitambaa. Hata hivyo, pingamizi hilo lilitupwa na aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji Lewis Makame (marehemu) baada ya kusikiliza utetezi wa Mtikila na Said, kuwa makosa waliyofungwa kwayo hayakuwa ya kukwepa kodi, kukosa uaminifu wala kukiuka maadili ya viongozi wa umma.

Mashtaka

Mbowe alikuwa anakabiliwa na mashtaka ya kumfanyia shambulio la kawaida, mwangalizi wa ndani wa Uchaguzi Mkuu Oktoba 31, 2010, Nassir Yamin katika kituo cha kupigia kura kilichokuwa katika Zahanati ya Lambo.

Yamin alikuwa ni mwangalizi wa kutoka Baraza Kuu la Waislamu wa Tanzania (Bakwata).

Akitoa hukumu hiyo, Hakimu Mpelembwa ambaye amehamishiwa Bukoba, alisema kitendo kilichofanywa na Mbowe hakikubaliki na kinapaswa kukemewa.
“Kitendo alichokifanya mshtakiwa akiwa Mwenyekiti wa Taifa wa Chadema na Mbunge wa Jimbo la Hai ambaye alipaswa kuwa kioo cha jamii hakikubaliki na lazima kikemewe,” alisema

Source.Mwananchi.
 
ahsante mkuu kwa kudadavua zaidi.....mbowe amelipa faini....hii ina maana kuwa kipindi chake cha kutumikia adhabu kwa mwaka mmoja inahesabiwa. Kama hivyo ndivyo je anayo haki kikatiba ya kuchagua na kuchaguliwa katika nafasi yoyote kitaifa. Naamini hutakwazwa na maswali yangu
laws of criems act!
--bado hujamwelewa.
 
Acha kudanganya wasiofuatilia sakata hili, alishtakiwa kwa kumshambulia MWANAGALIZI WA NDANI wa Uchaguzi Mkuu Oktoba 31, 2010, NASSIR YAMIN katika kituo cha kupigia kura kilichokuwa katika Zahanati ya Lambo. YAMIN alikuwa ni mwangalizi wa kutoka Baraza Kuu la Waslamu wa Tanzania (BAKWATA). Huo ndiyo ukweli na siyo ujinga wako unaotaka kutuaminisha.

Mkuu mbona mapovu tena imekuwaje?
 
kesi imekaa miaka sita mahakani hujashtuka tu hakimu alikuwa na lengo gani? kitu kingine cha kushangaza siku hizi majaji ni wana ccm unatengemea nn kwenye hukumu kama hii?
 
Muwe mnaomba msaada kwa fani ambazo siyo zenu.

Hapa issue siyo kuhukumiwa au kufungwa bali atapoteza haki iwapo hukumu yake imesababishwa na makosa matatu,
1.utovu wa uaminifu
2.kukwepa kodi
3.kuvunja sheria ya Madili ya Viongozi wa Umma.

Mbowe hajahukumiwa kwa kosa lolote kati ya hayo kwa hiyo bado ana haki ya kugombea nafasi yeyote ile hata bila kukata rufaa.

Sawa sawa kabisa. Hiyo ni namba 3 ndio inayombana.
 
Hivi jamani tuwe wakweli kwa vichwa vya sheria vilivyopo cdm,mnaamini kuwa hilo swala ndio wangeliwacha lipite tu kwa sababu mbowe kaachiwa huru? Hilo lilishaangaliwa na kujua nini madhara yake.
 
Sio kufungwa gerezani bali ni KUHUKUMIWA kufungwa gerezani kwa kipindi cha zaidi ya miezi sita. Haijalishi kama ataingia jela au la hata kama atalipa faini ya kiwango cha adhabu hiyo bado hana sifa. Kibaya zaidi hakukata rufaa bali amelipa faini fasta hilo ndio tatizo sasa.

Nani kakwambia hakukata rufaa? Wewe na Lisu nani anaijua sheria kuliko mwenzake?au ulitaka kila kitu wakwambie kwa kuwa hutaki mbowe agombee jimbo la hai?
 
Back
Top Bottom