Mbowe ameshakosa sifa ya ubunge mahakamani!

Mbowe ameshakosa sifa ya ubunge mahakamani!

Hilo gari likipita sehemu na Wananchi kuliona, watakuwa wanamkumbuka Mbowe na Kusahau Magamba
 
Ni kwamba Mbowe hajapoteza sifa za kugombea ubunge kwasababu hajatumikia kifungo. Soma tena hapo juu,ni mpaka utumikie kifungo kisichopungua miezi 6 ndiyo utapoteza hiyo sifa.

Ila mkuu si huwa wanadai kama umekutwa na hatia. Maana kulikua na adhabu mbili ya kulipa faini au kifungo. Kwa maana hiyo ni kwamba hizo zote ni adhabu na pia umekutwa na hatia. Hapo hakuna tofauti na kufungwa jela mwaka mmoja
 
Baada ya mahakama ya Hai kumuhukumu Mwenyekiti wa CHADEMA-Taifa, Freeman Mbowe kifungo cha mwaka mmoja au kulipa milioni moja baada ya kumshambulia msimamizi wa kituo cha uchaguzi kwenye jimbo la hai, sasa inaonekana uamuzi huo wa mahakama umemnyima usingizi kwani utamnyima fursa ya kuchaguliwa kuwa ama mbunge au rais. Hivyo amekata rufaa mahakama kuu kupinga uamuzi huo.

Kwa akili tu ya kawaida mtu yeyote angekata Rufaa kwa kesi kama hii regardless his political ambition. Kwa hiyo hapa rufaa hajakata kwa sababu ya Ubunge au Urais bali kusafisha jina lake!! Hukumu kama hiyo inaweza kukufanya hata ushindwe kusafiri nje ya nchi!! Hata hivyo hiyo hukumu inaonekana ni politically motivated ......!!
 
Hivi mbona mu wavivu wa kufikiria?Katiba inazungumzia hukumu ya kifungo,Mbowe ametoa faini.
Mzee sio suala la kufukiria hii taaluma na mimi si mwanasheria. Wanasheria wamekwisha tolea maelezo tena ya kuridhisha sioni sababu ya wewe kutoa lugha kali kiasi hiki.
 
Kamanda mbowe hana litakalomzuia kugombea kwa sababu (i) Hajafanya kosa lolote linaloambatana na kukosa uaminifu (ii) kukwepa kodi (iii) kuvunja maadili ya uongozi wa umma.

Hata mtikila aligombea uraisi 2005 japo alikuwa ametoka kufungwa miezi 6 jela, na wagombea wenzake walipomuwekea pingamizi, jaji Makame alitengua pingamizi kwa sababu havikuangukia kwenye makundi hayo.

Sasa kama CCM walikuwa wanaivuta kesi miaka mitano toka 2010 ili waje wamuwekee pingamizi wamechemsha.
 
Mkuu;

Kwa kukusaidia zaidi, Katiba imeenda mbele zaidi kwenye kifungu cha 67(7)(b) na kusema,

‘’ikiwa mtu atapewa adhabu ya kufungwa gerezani ikifahamika kuwa adhabu hiyo ya kifungo imetolewa badala ya adhabu ya kutozwa faini au imetolewa kwa sababu mtu huyo ameshindwa kulipa faini aliyoamriwa kulipa, basi muda wa kifungo cha namna hiyo hautahesabiwa’’.

Nadhani kwa sasa umeelewa!

Mi naona kama bado sijaelewa, Mh. MBOWE kahukumiwa kwenda jela mwaka mmoja au kulipa faini, nilivyoelewa mm ni kwamba hakuhukumiwa kulipa faini ili kama akishindwa ndio afungwe, bali atachaguwa yy moja ya hukumu mbili hizo kwakuwa zote kahukumiwa nazo.
 
Anaendelea..Suala hilo linafanana na lililotokea katika mchakato wa uteuzi wa wagombea urais mwaka 2005 wakati aliyekuwa mgombea urais wa DP, Mchungaji Christopher Mtikila na mgombea mwenza wake, Saidi Soud Said walipowekewa pingamizi kutokana na kutumikia kifungo jela, Mtikila akitumikia mwaka mmoja kwa kosa la uchochezi, Said akitumikia chuo cha mafunzo kwa kosa la biashara ya vitambaa. Hata hivyo, pingamizi hilo lilitupwa na aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji Lewis Makame (marehemu) baada ya kusikiliza utetezi wa Mtikila na Said, kuwa makosa waliyofungwa kwayo hayakuwa ya kukwepa kodi, kukosa uaminifu wala kukiuka maadili ya viongozi wa umma.
Nina wasiwasi na mkuu wa NEC wa sasa maana viwango vya 'kutumiwa' vinatofautiana!

 

Kumekuwa na mjadala mkubwa tangu jana baada ya hukumu ya Hakimu Mkazi wa Wilaya ya Hai, Denis Mpelembwa kuhusu kesi ya jinai na. 73 ya mwaka 2011.

Mjadala uliokuwa unaendelea kwenye mitandao ya kijamii zikiwemo forums kama Jamii Forums na kwingine ambako wanachama wanajadili masuala serious ya kisiasa, kijamii na kiuchumi, imeleta hali ya utata kuhusu sifa za kugombea ubunge.

Vyombo vya habari baadhi vikitumia anonymous sources, wanasheria bila hata ya kufanya citations either ya vifungu vya katiba, sheria za nchi au precedence zilizowekwa na kesi zingine za namna hiyo, vimekwenda hatua ya kuandika kuwa Mwenyekiti Mbowe amepoteza sifa za kugombea uchaguzi kwa sababu ya hukumu hiyo.

Vyombo vya habari makini vimefanya uchambuzi kwa kunukuu wanasheria ambao wamefanya citations na kutoa precedence zilizowahi kutokea.

Mathalani katika Gazeti la Mwananchi wakitumia kichwa cha habari "Hukumu ya Hakimu Mkazi; Mbowe azua utata wa sifa ya kugombea; Mbowe ahukumiwa, utata wa sifa ya kugombea waibuka - Kitaifa wameandika;

"Hata hivyo, Mwanasheria, Alex Mgongolwa akinukuu Katiba ya Tanzania Ibara ya 67 (1)(c); 67(2) (c na d) alisema hukumu hiyo haiwezi kumzuia kugombea ubunge kwa sababu hakwenda jela na kosa lake halihusu kukosa utovu wa uaminifu, kukwepa kodi wala kuvunja Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma.

"Suala hilo linafanana na lililotokea katika mchakato wa uteuzi wa wagombea urais mwaka 2005 wakati aliyekuwa mgombea urais wa DP, Mchungaji Christopher Mtikila na mgombea mwenza wake, Saidi Soud Said walipowekewa pingamizi kutokana na kutumikia kifungo jela, Mtikila akitumikia mwaka mmoja kwa kosa la uchochezi,

Said akitumikia chuo cha mafunzo kwa kosa la biashara ya vitambaa. Hata hivyo, pingamizi hilo lilitupwa na aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji Lewis Makame (marehemu) baada ya kusikiliza utetezi wa Mtikila na Said, kuwa makosa waliyofungwa kwayo hayakuwa ya kukwepa kodi, kukosa uaminifu wala kukiuka maadili ya viongozi wa umma."


Kesi hiyo ya Hai, inatukumbusha kesi ya aliyekuwa Mbunge wa Bukoba Mjini, Wilfred Lwakatare ambaye mwaka 2006 alishtakiwa na baadae kuhukumiwa kwa kosa la namna hiyo, kisha akawa na sifa za kugombea ubunge mwaka 2010 katika jimbo hilo.

Tutawapatia taarifa kamili juu ya hatua ambazo wanasheria wa chama wanachukua baada ya kupewa maelekezo juu ya kesi hiyo.

Kwa sasa kauli aliyotoa Mwenyekiti wa Chama jana baada ya hukumu hiyo, zinapaswa kuwatia ari wapiganaji kusonga mbele kuendelea na majukumu ya kupigania haki kila mahali, wakijipanga kuiondoa CCM madarakani.

Kwa wale wanaoweza kusoma, ni vyema wakapitia Katiba ya Tanzania, Chapter 3, Part II, Section 67(2).

"Akizungumza nje ya chumba cha Mahakama hiyo, Mbowe aliwatoa hofu wanachama wa Chadema kwamba wasikatishwe tamaa na hukumu hiyo ambayo alisema alitegemea ingekuwa hivyo.“Mnanipa pole ya nini? Kuna msiba hapa? Tupeane hongera. Sikutarajia cha tofauti na hiki kilichofanyika. Hakinivunji nguvu, bali kinaniimarisha katika mapambano,” alisema.

“Haki katika nchi hii itapiganiwa kwa watu wengine kuumia na wengine kuokoka. Nimesota mahakamani miaka mitano badala ya kufanya kazi ya wananchi. Hainivunji moyo,” alisema na kuongeza:

“Hainivunji moyo katika azma yangu ya kuikomboa nchi hii na ukombozi uko jirani. Mahakama ya nchi hii vimekuwa ni vyombo vya kutoa dhuluma kwa wananchi japo siyo mahakimu wote. Lakini iko siku Mahakama zitakuwa ni sehemu ya kutolea haki, kutenda haki na haki ionekane imetendeka. Mapambano yanaendelea na nawaomba msiwe wanyonge,” alisisitiza.

“Sitaki kuizungumzia Mahakama katika hatua ya sasa lakini ndani ya Mahakama kuna watu wanaotenda haki na ndani ya Mahakama kuna watu wasiotenda haki,” alisema Mbowe.

Alisema kesi hiyo haikustahili kuiendesha kwa miaka mitano na kwamba kodi za wananchi zinateketea pamoja na muda, akisema haiwezekani nchi ikaendeshwa katika utaratibu huo.

“Kama mimi mbunge, Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, mtunga sheria wa nchi hii naweza kusoteshwa mahakamani miaka mitano, mwananchi wa kawaida atafanywaje?” alihoji Mbowe."

Makene

 
Dj mbowe hawezi kugombea tena,anafikiri siasa ni ngumi kashazoea fujo na vurugu,atiwe ndani tu nchi iwe na aman
 
Mbowe amekuwa akifanya jinai nyingi sana yafaa sasa afungwe jela kabisa siyo kutozwa faini.
 
Kumchapa makofi mtendaji wa umma (msimamizi wa kituo cha uchaguzi) mzembe na mpuuzi sio tuu kuwa hakumkoseshi sifa za uongozi Mbowe au kiongozi yeyote bali kunamwongezea sifa zaidi kuwa huyo ni kiongozi makini na anayechukua maamuzi sahihi kwa wakati muafaka.
Hukumu hii itakuwa rejea kwa uchaguzi mkuu wa oktoba pale ambapo wasimamizi wa vituo wataleta masihara. Tutawachapa makofi sana ili wakaonyeshe mashavu yaliyovimba kwa wake/waume zao ili watimize wajibu wao na hukumu ya mwaka jela au faini ya milioni moja tunachangishana kulipa lakini haki inakuwa imetendeka ipasavyo.
Hii ni hukumu imetuondoa woga. Wito kwa wale tutakao tembeza makofi, judo na kareti, mahakamani hakuna haja ya kukana shtaka maana linaweza kutupotezea muda ni kukiri na kulipa faini na kuendelea na shughuli zingine huku mgombea aliyeshinda kihalali akitangazwa mshindi.
Mbowe kila siku unakuja na fundisho jipya, hakika hili nalo ni fundisho. HONGERA.
 
Kamanda mbowe hana litakalomzuia kugombea kwa sababu (i) Hajafanya kosa lolote linaloambatana na kukosa uaminifu (ii) kukwepa kodi (iii) kuvunja maadili ya uongozi wa umma.

Hata mtikila aligombea uraisi 2005 japo alikuwa ametoka kufungwa miezi 6 jela, na wagombea wenzake walipomuwekea pingamizi, jaji Makame alitengua pingamizi kwa sababu havikuangukia kwenye makundi hayo.

Sasa kama CCM walikuwa wanaivuta kesi miaka mitano toka 2010 ili waje wamuwekee pingamizi wamechemsha.
Nafahamu CHADEMA ina mwanasheria wake ambaye hutoa matamko pindi kunapokuwa na masuala hayo ya kisheria. Nakumbuka katika ile kesi ya Zitto alijitokeza mapema na kusema kwa hukumu ile Zitto kajivua uanachama. Na kwa hili basi Tundu Lissu atoe tamko manake linamhusu Mwenyekiti wa Chama
 
Back
Top Bottom