Mbowe ameshakosa sifa ya ubunge mahakamani!

Mbowe ameshakosa sifa ya ubunge mahakamani!

alimshambulia wakala wa CCM baada ya kuiba kura uchaguzi uliopita.ila sio lazima awe mbunge
Acha kudanganya wasiofuatilia sakata hili, alishtakiwa kwa kumshambulia MWANAGALIZI WA NDANI wa Uchaguzi Mkuu Oktoba 31, 2010, NASSIR YAMIN katika kituo cha kupigia kura kilichokuwa katika Zahanati ya Lambo. YAMIN alikuwa ni mwangalizi wa kutoka Baraza Kuu la Waslamu wa Tanzania (BAKWATA). Huo ndiyo ukweli na siyo ujinga wako unaotaka kutuaminisha.
 
Baada ya mahakama ya Hai kumuhukumu Mwenyekiti wa CHADEMA-Taifa, Freeman Mbowe kifungo cha mwaka mmoja au kulipa milioni moja baada ya kumshambulia msimamizi wa kituo cha uchaguzi kwenye jimbo la hai, sasa inaonekana uamuzi huo wa mahakama umemnyima usingizi kwani utamnyima fursa ya kuchaguliwa kuwa ama mbunge au rais. Hivyo amekata rufaa mahakama kuu kupinga uamuzi huo.

Cdm ni nyumba ya wanasheria,hivyo kabla yako kulisema hilo tayari walishaliona
 
Wataalamu wa sheria watusaidie kulifafanua hili. Sheria inamzuia mtu aliyetumikia kifungo, sijui hapa kwa mtu aliyelipa faini inakuwaje!
cc: Petro Mselewa

sikweli kwa mujibu wa katiba yetu kufungwa sio kitu kinachoweza mzuia mtu kugombea ubunge. bali kama akifungwa kwa kosa la kutokuwa muaminifu au kukwepa kodi ama kukiuka sheria ya maadili ya viongozi wa umma.
 
Hata asipokata rufaa bado hakuna sheria za kumzuia kugombea kwa kosa la kumkata makofi mtendaji mpuuzi. Kosa hilo halijaainishwa na Katiba yetu kama kosa la kumnyima mtu uongozi maana halihusiani na makosa ya rushwa au maadili.
 
Baada ya mahakama ya Hai kumuhukumu Mwenyekiti wa CHADEMA-Taifa, Freeman Mbowe kifungo cha mwaka mmoja au kulipa milioni moja baada ya kumshambulia msimamizi wa kituo cha uchaguzi kwenye jimbo la hai, sasa inaonekana uamuzi huo wa mahakama umemnyima usingizi kwani utamnyima fursa ya kuchaguliwa kuwa ama mbunge au rais. Hivyo amekata rufaa mahakama kuu kupinga uamuzi huo.

hata kama asingekata rufaa bado anaruhusiwa kugombea ubunge....
 
Ni baada ya kutiwa hatiani na kupewa adhabu ya kifungo cha mwaka mmoja au faini mahakamani jana.
Ushabiki wa kitoto namna hii haufai kwenye jukwaa la vichwa komavu.Huu ni ufahamu wa kusikia mithili ya ndege.kifungu tajwa kimespecify adhabu.wew umesikia hukumu tu unakurupuka na kithread chako.ignorance is sin......just confess now........!!
 
Andrew Chenge alipatiakana na kosa la kuendesha gari bila bima na pia reckless driving kitendo kichosababisha kuua wasichana wawili hapo hapo.

Mahakama ilimutia hatiani na kumuhukum kifungo gerezani au kulipa faini ya Tsh 500,000/-.

Chenge alilipa faini hiyo na hadi leo ni Mbunge wa bunge la JMT.

Nafikiri kuna maelezo mazuri tu ya kisheria yametolewa kufafanua kuwa Mbowe hazuiliwi kugombea ubunge kisheria. Hayo ya Chenge unayaleta bila sababu kwa maana hayana msaada wowote kwenye muktadha huu. Hukumu yake na muda wa kuchaguliwa vinapishana zaidi ya mwaka. Chill tu Mbowe atagombea ubunge.
 
Alishinda rufaa iliyofuta ile adhabu japo alikuwa amekwisha toka kwa msamaha wa rais. Sasa Mbowe aanze mchakato wa rufaa leo nadhani itasikilizwa August na maamuzi yatatoka January. UKAWA ingejipanga tu kumsimamisha mgombe mwingine hapo Hai na Mbowe akimshika mkono hata Mbuzi anashinda.

hata asipokata rufaa bado ana sifa za kugombea...
 
mbowe bado ana sifa za kugombea ubunge ama urais.kosa lililomtia hatiani halihusiani na kuzuiwa yeye kugombea ..
 
Mkuu;
Hili ni jukwaa la elimu na kupashana habari. Hakuna sababu ya kukwazika katika kuelimishana na kupashana habari.

Kwa sababu hukumu ya Mbowe ilikuwa ni kifungo au faini basi kwa sasa Mbowe yuko huru kugombea Ubunge baada ya kulipa faini kama maelezo yanavyoeleza.
Thanks.

Kifungu cha ajabu kabisa hiki! Kwa hiyo sisi masikini tusio na hela ukikatiwa kifungo cha zaidi ya miezi sita au faini na ukashindwa kulipa faini unaenda gerezani na hutokuwa na haki ya kugombea nafasi yoyote ya kitaifa maisha yako yote!? No, hiki kifungu kiliwekwa kuwalinda matajiri; tena ni cha kibaguzi.
 
Hata asipokata rufaa bado hakuna sheria za kumzuia kugombea kwa kosa la kumkata makofi mtendaji mpuuzi. Kosa hilo halijaainishwa na Katiba yetu kama kosa la kumnyima mtu uongozi maana halihusiani na makosa ya rushwa au maadili.

ni kweli mkuu....
 
Baada ya mahakama ya Hai kumuhukumu Mwenyekiti wa CHADEMA-Taifa, Freeman Mbowe kifungo cha mwaka mmoja au kulipa milioni moja baada ya kumshambulia msimamizi wa kituo cha uchaguzi kwenye jimbo la hai, sasa inaonekana uamuzi huo wa mahakama umemnyima usingizi kwani utamnyima fursa ya kuchaguliwa kuwa ama mbunge au rais. Hivyo amekata rufaa mahakama kuu kupinga uamuzi huo.

Kwa kuwa inasemekana hakuna hata shahidi mmoja wa upande wa mashtaka aliyetoa ushahidi Mbowe anaweza kuomba mahakama ya juu ipitie mwenendo wa kesi kwa hati ya dharura na uwezekano wa hiyo hukumu kubatilishwa ni mkubwa na hakimu kuonywa.
 
Kifungu cha ajabu kabisa hiki! Kwa hiyo sisi masikini tusio na hela ukikatiwa kifungo cha zaidi ya miezi sita au faini na ukashindwa kulipa faini unaenda gerezani na hutokuwa na haki ya kugombea nafasi yoyote ya kitaifa maisha yako yote!? No, hiki kifungu kiliwekwa kuwalinda matajiri; tena ni cha kibaguzi.
Mimi nadhani hoja siyo kifungu hiki bali ni kosa linalopelekea kuwepo kwa kifungu hiki.
 
Alishinda rufaa iliyofuta ile adhabu japo alikuwa amekwisha toka kwa msamaha wa rais. Sasa Mbowe aanze mchakato wa rufaa leo nadhani itasikilizwa August na maamuzi yatatoka January. UKAWA ingejipanga tu kumsimamisha mgombe mwingine hapo Hai na Mbowe akimshika mkono hata Mbuzi anashinda.

Rage alitoka jela kwa msamaha wa Rais kutokana na afya yake kutokuwa nzuri.
 
Rejea kesi ya mtemi Chenge pale kwa hakimu mkazi kinomdoni utaelewa mtu akilipa faini inamaanisha nini
 
Back
Top Bottom