Mbowe ameshakosa sifa ya ubunge mahakamani!

Mbowe ameshakosa sifa ya ubunge mahakamani!

Mkuu ungeendelea tu kututafsiria......lugha ya sheria nayo ni tabu
Mkuu;

Kwa kukusaidia zaidi, Katiba imeenda mbele zaidi kwenye kifungu cha 67(7)(b) na kusema,

''ikiwa mtu atapewa adhabu ya kufungwa gerezani ikifahamika kuwa adhabu hiyo ya kifungo imetolewa badala ya adhabu ya kutozwa faini au imetolewa kwa sababu mtu huyo ameshindwa kulipa faini aliyoamriwa kulipa, basi muda wa kifungo cha namna hiyo hautahesabiwa''.

Nadhani kwa sasa umeelewa!
 
Mkuu;

Kwa kukusaidia zaidi, Katiba imeenda mbele zaidi kwenye kifungu cha 67(7)(b) na kusema,

‘’ikiwa mtu atapewa adhabu ya kufungwa gerezani ikifahamika kuwa adhabu hiyo ya kifungo imetolewa badala ya adhabu ya kutozwa faini au imetolewa kwa sababu mtu huyo ameshindwa kulipa faini aliyoamriwa kulipa, basi muda wa kifungo cha namna hiyo hautahesabiwa’’.

Nadhani kwa sasa umeelewa!

Ahsante mkuu kwa kudadavua zaidi.....Mbowe amelipa faini....hii ina maana kuwa kipindi chake cha kutumikia adhabu kwa mwaka mmoja inahesabiwa. Kama hivyo ndivyo je anayo haki kikatiba ya kuchagua na kuchaguliwa katika nafasi yoyote kitaifa. Naamini hutakwazwa na maswali yangu
 
Mkuu ungeendelea tu kututafsiria......lugha ya sheria nayo ni tabu

Ni kwamba Mbowe hajapoteza sifa za kugombea ubunge kwasababu hajatumikia kifungo. Soma tena hapo juu,ni mpaka utumikie kifungo kisichopungua miezi 6 ndiyo utapoteza hiyo sifa.
 
Ni kwamba Mbowe hajapoteza sifa za kugombea ubunge kwasababu hajatumikia kifungo. Soma tena hapo juu,ni mpaka utumikie kifungo kisichopungua miezi 6 ndiyo utapoteza hiyo sifa.

Ahsante mkuu
 
Ahsante mkuu kwa kudadavua zaidi.....Mbowe amelipa faini....hii ina maana kuwa kipindi chake cha kutumikia adhabu kwa mwaka mmoja inahesabiwa. Kama hivyo ndivyo je anayo haki kikatiba ya kuchagua na kuchaguliwa katika nafasi yoyote kitaifa. Naamini hutakwazwa na maswali yangu
Mkuu;
Hili ni jukwaa la elimu na kupashana habari. Hakuna sababu ya kukwazika katika kuelimishana na kupashana habari.

Kwa sababu hukumu ya Mbowe ilikuwa ni kifungo au faini basi kwa sasa Mbowe yuko huru kugombea Ubunge baada ya kulipa faini kama maelezo yanavyoeleza.
Thanks.
 
ila kwa ubovu wa katiba yetu sidhani kama haijavuja sehemu ngoja tuone kwani tuna wanasheria waliobobea .niliona yule jamaa wa mzumbe mwenye miaka 33 alipotaka uraisi aliinanga katiba yetu pia
 
Andrew Chenge alipatiakana na kosa la kuendesha gari bila bima na pia reckless driving kitendo kichosababisha kuua wasichana wawili hapo hapo.

Mahakama ilimutia hatiani na kumuhukum kifungo gerezani au kulipa faini ya Tsh 500,000/-.

Chenge alilipa faini hiyo na hadi leo ni Mbunge wa bunge la JMT.
 
Atakosa sifa endapo kosa alilotenda ni moja kati ya haya kwa mijubu wa Katiba ya Jmahuri ya Muungano wa Tanzania Ibara ya 67(1)(c) na 67 (2)(cna d)
1.utovu wa uaminifu
2.kukwepa kodi
3.kuvunja sheria ya Madili ya Viongozi wa Umma.
 
Sidhani kwa sababu mwka juzi mbunge wa Mbarali( CCM) alihukumiwa kifungo au faini kwa kumpiga mkt wa kijiji alilipa faini na anaendelea kuwa mbunge.
Patamu hapo, ngoja tuone double standard za ccm, hakimu anahukumu huku ana kadi ya ccm mfukoni
 
Mbunge wa Tabora Mh. Hadeni Ragembona alifungwa jela kabisa na kisha baada ya hapo akachaguliwa kuwa Mbunge
 
Alishinda rufaa iliyofuta ile adhabu japo alikuwa amekwisha toka kwa msamaha wa rais. Sasa Mbowe aanze mchakato wa rufaa leo nadhani itasikilizwa August na maamuzi yatatoka January. UKAWA ingejipanga tu kumsimamisha mgombe mwingine hapo Hai na Mbowe akimshika mkono hata Mbuzi anashinda.

Kosa alilo hukumiwa nalo hata asipokata rufaa kisheria halimzuii kugombea ubunge kamwe. Unakumbuka kesi ya Mtikila na mgombea mwenza wake pale walipokua wanagombea uraisi wakawekewa pingamizi na ccm pale nec chini ya Jaji Makame? Mtikila alikaa gerezan miezi6 na mgombea mwenza kwa mwaka1 lkn bdo Nec chini ya Makame ikaona kosa lililowahukumu bdo halimzuii kugombea uraisi.
 
Hiyo Sheria kandamizi inawaondolea fursa watu kwa mfano mandela asingekuwa rais Kama south africa wangekuwa na huo upuuzi.
 
kwani Chnge alipotakiwa kufungwa au kulipa faini na akalipa faini alikosa sifa ya kugombea ubunge?
 
Ni baada ya kutiwa hatiani na kupewa adhabu ya kifungo cha mwaka mmoja au faini mahakamani jana.

Mbona mbunge wenu Rage alitumikia kifungo jera zaidi ya hiyo miezi?
 
Kosa alilo hukumiwa nalo hata asipokata rufaa kisheria halimzuii kugombea ubunge kamwe. Unakumbuka kesi ya Mtikila na mgombea mwenza wake pale walipokua wanagombea uraisi wakawekewa pingamizi na ccm pale nec chini ya Jaji Makame? Mtikila alikaa gerezan miezi6 na mgombea mwenza kwa mwaka1 lkn bdo Nec chini ya Makame ikaona kosa lililowahukumu bdo halimzuii kugombea uraisi.

Kama ni hivyo ni heri pia kwa afya ya demokrasia, Mbowe ni kiongozi thabiti na kwakweli busara zake zimesaidia sana kudhibiti mihemuko ya vijana wake hasa katika bunge hili.
 
Back
Top Bottom