Mbowe ameshakosa sifa ya ubunge mahakamani!

Mbowe ameshakosa sifa ya ubunge mahakamani!

Kumbe aliyeshikishwa adabu na Mh Mbowe alikuwa muangalizi wa ndani kutokea BAKWATA?
 
Ya chenge haikuwa criminal case ilikuwa ni traffic case
Sheria inasema:

Ibara ya 67
(2) Mtu hatakuwa na sifa za kustahili kuchaguliwa au kuteuliwa kuwa Mbunge-
(c) ikiwa mtu huyo amehukumiwa na Mahakama yoyote katika Jamhuri ya Muungano na kupewa adhabu ya kifo au ya kufungwa gerezani kwa muda unaozidi miezi sita kwa kukutwa na hatia ya kosa lolote, vyovyote linavyoitwa


Wapi imetaja criminal?



 
Mkurugenzi wa Kampuni ya Excellence Attorneys Mwanasheria, Alex Mgongolwa akinukuu Katiba ya Tanzania Ibara ya 67 (1)(c); 67(2) (c na d) alisema hukumu hiyo haiwezi kumzuia kugombea ubunge kwa sababu hakwenda jela na kosa lake halihusu kukosa utovu wa uaminifu, kukwepa kodi wala kuvunja Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma.

Hukumu hiyo iliibua mjadala mkali kwenye mitandao ya kijamii juu ya uwezekano wa kumzuia Mbowe ambaye pia ni Kiongozi wa Upinzani Bungeni kuwania tena ubunge au urais katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba.

Anaendelea..Suala hilo linafanana na lililotokea katika mchakato wa uteuzi wa wagombea urais mwaka 2005 wakati aliyekuwa mgombea urais wa DP, Mchungaji Christopher Mtikila na mgombea mwenza wake, Saidi Soud Said walipowekewa pingamizi kutokana na kutumikia kifungo jela, Mtikila akitumikia mwaka mmoja kwa kosa la uchochezi, Said akitumikia chuo cha mafunzo kwa kosa la biashara ya vitambaa. Hata hivyo, pingamizi hilo lilitupwa na aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji Lewis Makame (marehemu) baada ya kusikiliza utetezi wa Mtikila na Said, kuwa makosa waliyofungwa kwayo hayakuwa ya kukwepa kodi, kukosa uaminifu wala kukiuka maadili ya viongozi wa umma.

Hata Hivyo Mhe. Freeman Mbowe, kiongozi anayezijua shida za wananchi wa jimbo lake, na kuzitatua, bila kuwapangia na kuwalisha ahadi, kiongozi anayefanya jambo sio kwa maslahi yake, wala masilahi ya kisiasa, Jana Alikabidhi gari la taka jipya kabisa kwa halmashauri ya Hai

11401072_691376090967811_2192159437958911348_n.jpg
 
Alishinda rufaa iliyofuta ile adhabu japo alikuwa amekwisha toka kwa msamaha wa rais. Sasa Mbowe aanze mchakato wa rufaa leo nadhani itasikilizwa August na maamuzi yatatoka January. UKAWA ingejipanga tu kumsimamisha mgombe mwingine hapo Hai na Mbowe akimshika mkono hata Mbuzi anashinda.

Hivi mbona mu wavivu wa kufikiria?Katiba inazungumzia hukumu ya kifungo,Mbowe ametoa faini.
 
67.-(1) Bila ya kuathiri masharti yaliyomo katika ibara hii, mtu
yeyote atakuwa na sifa za kustahili kuchaguliwa au kuteuliwa
kuwa Mbunge endapo-
(a) ni raia wa Jamhuri ya Muungano aliyetimiza umri wa
miaka ishirini na moja, na ambaye anajua kusoma na
kuandika katika Kiswahili au Kiingereza;
(b) ni mwanachama na ni mgombea aliyependekezwa na
chama cha siasa;
(c) katika kipindi cha miaka mitano kabla ya tarehe ya
Uchaguzi hakuwahi kutiwa hatiani katika mahakama
yoyote kwa kosa lolote la kukwepa kulipa kodi yoyote
ya Serikali.
(2) Mtu hatakuwa na sifa za kustahili kuchaguliwa au kuteuliwa
kuwa Mbunge-
(a) ikiwa mtu huyo anao au kwa hiari yake amejipatia
uraia wa nchi nyingine yote; au
(b) ikiwa kwa mujibu wa sheria inayotumika katika
Jamhuri ya Muungano imethibitishwa rasmi kwamba
mtu huyo ana ugonjwa wa akili; au
(c) ikiwa mtu huyo amehukumiwa na Mahakama yoyote
katika Jamhuri ya Muungano na kupewa adhabu ya
kifo au ya kufungwa gerezani kwa muda unaozidi
miezi sita kwa kukutwa na hatia ya kosa lolote,
vyovyote linavyoitwa, linaloambatana na utovu wa
uaminifu; au
(d) ikiwa katika kipindi cha miaka mitano kabla ya tarehe
ya Uchaguzi Mkuu amepata kuhukumiwa na kupewa
adhabu ya kifungo kwa kosa linaloambatana na utovu
wa uaminifu au kwa kuvunja sheria ya Maadili ya
Viongozi wa Umma;
(e) bila ya kuingilia haki na uhuru wa mtu kuwa na maoni
yake, kuamini dini atakayo, kushirikiana na wengine
na kushiriki shughuli za umma kwa mujibu wa sheria
za nchi, ikiwa mtu huyo si mwanachama na mgombea
aliyependekezwa na chama cha siasa;
(f) ikiwa mtu huyo ana masilahi yoyote katika mkataba wa
Serikali wa aina yoyote aliyowekewa miiko maalum
kwa mujibu wa sheria iliyotungwa na Bunge, na iwapo
amekiuka miiko hiyo;
(g) ikiwa mtu huyo ameshika madaraka ya afisa
mwandamizi katika utumishi wa Serikali ya Jamhuri ya
Muungano, isipokuwa madaraka ambayo Rais aweza
au anatakiwa kukabidhi kwa Mbunge kwa mujibu wa
Katiba hii au sheria iliyotungwa na Bunge;
(h) ikiwa kwa mujibu wa sheria iliyotungwa na Bunge
Katiba
 
Sawa sawa kabisa. Hiyo ni namba 3 ndio inayombana.
Nakushauri uwe unafanya homework kabla ya kurukia issue hakuna mtu wa kukutafunia kila kitu,

tafuta maadili ya kiongozi wa umma ni yapi na kiongozi wa umma ni nani.
 
Magamba bhana Yaani yanajiona yatatawala milele yamepigwa upofu hata October hayaioni,tutayachinja hakika.
 
Unachagua ninani wa kujibu?, kafungue jukwaa lako na familia yako.

Swali halikuelekezwa kwako......kama ukiamua kutukana ama kutumia lugha yoyote inayokupendeza ruksaaa
 
Ni baada ya kutiwa hatiani na kupewa adhabu ya kifungo cha mwaka mmoja au faini mahakamani jana.

Hii ni mbinu kama alivyofanyiwa marehemu Chacha Wangwe na kuhukumiwa kifungo cha mwaka mmoja karibia na uchaguzi wa mwaka 2005. Hata hivyo alishinda rufaa yake ikaonekana kuwa alipewa adhabu kubwa sana.
 
Hili gari limenunuliwa kwa ruzuku ya ufipa, hii SACCOS ni balaa.
 
Conviction ni conviction tu haijalishi umelipa fine au umehukumiwa kifungo kwa hiyo mwenyekiti wetu imekula kwake labda akate rufaa haraka na rufaa yenyewe itolewe maamuzi kabla ya uchaguzi
Watu mnapenda ligi sana someni sheria sio kila hukumu inamzuia mtu kugombea.
 
CCM inatapatapa na kwa mara nyingine imeangukia pua
 
Back
Top Bottom