67.-(1) Bila ya kuathiri masharti yaliyomo katika ibara hii, mtu
yeyote atakuwa na sifa za kustahili kuchaguliwa au kuteuliwa
kuwa Mbunge endapo-
(a) ni raia wa Jamhuri ya Muungano aliyetimiza umri wa
miaka ishirini na moja, na ambaye anajua kusoma na
kuandika katika Kiswahili au Kiingereza;
(b) ni mwanachama na ni mgombea aliyependekezwa na
chama cha siasa;
(c) katika kipindi cha miaka mitano kabla ya tarehe ya
Uchaguzi hakuwahi kutiwa hatiani katika mahakama
yoyote kwa kosa lolote la kukwepa kulipa kodi yoyote
ya Serikali.
(2) Mtu hatakuwa na sifa za kustahili kuchaguliwa au kuteuliwa
kuwa Mbunge-
(a) ikiwa mtu huyo anao au kwa hiari yake amejipatia
uraia wa nchi nyingine yote; au
(b) ikiwa kwa mujibu wa sheria inayotumika katika
Jamhuri ya Muungano imethibitishwa rasmi kwamba
mtu huyo ana ugonjwa wa akili; au
(c) ikiwa mtu huyo amehukumiwa na Mahakama yoyote
katika Jamhuri ya Muungano na kupewa adhabu ya
kifo au ya kufungwa gerezani kwa muda unaozidi
miezi sita kwa kukutwa na hatia ya kosa lolote,
vyovyote linavyoitwa, linaloambatana na utovu wa
uaminifu; au
(d) ikiwa katika kipindi cha miaka mitano kabla ya tarehe
ya Uchaguzi Mkuu amepata kuhukumiwa na kupewa
adhabu ya kifungo kwa kosa linaloambatana na utovu
wa uaminifu au kwa kuvunja sheria ya Maadili ya
Viongozi wa Umma;
(e) bila ya kuingilia haki na uhuru wa mtu kuwa na maoni
yake, kuamini dini atakayo, kushirikiana na wengine
na kushiriki shughuli za umma kwa mujibu wa sheria
za nchi, ikiwa mtu huyo si mwanachama na mgombea
aliyependekezwa na chama cha siasa;
(f) ikiwa mtu huyo ana masilahi yoyote katika mkataba wa
Serikali wa aina yoyote aliyowekewa miiko maalum
kwa mujibu wa sheria iliyotungwa na Bunge, na iwapo
amekiuka miiko hiyo;
(g) ikiwa mtu huyo ameshika madaraka ya afisa
mwandamizi katika utumishi wa Serikali ya Jamhuri ya
Muungano, isipokuwa madaraka ambayo Rais aweza
au anatakiwa kukabidhi kwa Mbunge kwa mujibu wa
Katiba hii au sheria iliyotungwa na Bunge;
(h) ikiwa kwa mujibu wa sheria iliyotungwa na Bunge
Katiba