Mbowe akiwa na vijana wake wa CHAUMMA

Mbowe akiwa na vijana wake wa CHAUMMA

Mwenyekiti wazamani wa CHADEMA Freeman Mbowe akiwa na vijana na makada wa zamani wa CHADEMA ambapo walihamia kwenye chama Cha CHAUMMA .

Vijana wanajichekesha tu wenyewee
Hawa wanamheshimu sana Mbowe hata kama yuko Chadema. Na mwenyewe anawaheshimu sana maana walimpigania sana wakati akiwa jela na wakati wa uchaguzi. Wanaipenda bado Chadema ndio maana huwasikii wakiwatukana viongozi wake pamoja na figisu kibao walizofanyiwa na wanazoendelea kufanyiwa. Ni wapinzani damu damu.

Amandla...
 
WanaCHADEMA haitawasaidia kitu kumtukana Mbowe. Siasa za nchi hii hazitabiriki. Mwaka 2001 kina Lipumba na CUF yake walikuwa wa moto mno wakipambana na IGP katili Mahita kiasi kwamba Lipumba alikuwa anakutana na vipigo vitakatifu ila Lipumba huyohuyo akautangazia umma kuwa aliwasihi waislamu wenzake wamchague JK mwaka 2010 huku yeye pia mgombea urais.

Miaka 5 baadae yaani 2015 katibu mkuu bora wa muda wote CHADEMA Padri aliyeasi, Dr Slaa aliamua kujiweka kando na CHADEMA ambapo baadae alipata ulaji kwenye serikali ya JPM.

Nimetoa mifano miwili kuonyesha kuwa unaweza kumtukana Mbowe kumbe msaliti wenu anaweza kuwa Heche au Lissu. Cha muhimu mheshimiane.
 
Back
Top Bottom