Mbona mapato ya kila mwezi hatusomewi?

Mbona mapato ya kila mwezi hatusomewi?

Nadhani wameamua kufuata utaratibu wa mahesabu, kila baada ya miezi 3 yanatakiwa kusomwa mapato na matumizi, kama ilivyo kwenye serikali za mitaa.
 
Sasa kama ni hivyo si watangaze! Tatizo liko wapi
Wakitangaza ww unapata faida gani? Wameamua kuripoti kwa mwajiri wao na yeye akiamua kutangaza ni yeye. Kazi ya tra siyo kutangaza mapato bali ni kuassess kukusanya na kuwasilisha serikalini.
 
Nadhani wameamua kufuata utaratibu wa mahesabu, kila baada ya miezi 3 yanatakiwa kusomwa mapato na matumizi, kama ilivyo kwenye serikali za mitaa
Sasa si waseme, tatizo ni nini? Au mpaka watumbuliwe
 
Ni lazima kwa kuwa fedha ni zetu ila wao wanazikusanya kwa niaba yetu. Kwa kuwa kila mtanzania hulipa kodi akiwa peke yake kwa ivo ni LAZIMA wanaozikusanya kutoa hesabu ya jumla ya fedha wanazozikusanya kwa kila mwezi!
Benki kuu na TRA wanatangaza mapato kwenye website yao. Nendeni mkasome acheni uvivu.
 
Wakitangaza ww unapata faida gani? Wameamua kuripoti kwa mwajiri wao na yeye akiamua kutangaza ni yeye. Kazi ya tra siyo kutangaza mapato bali ni kuassess kukusanya na kuwasilisha serikalini.
Hivi hizi shule huwa mnasomea kwenye miembe? Kwani mbona mwanzoni walikuwa wanatangaza? Wewe ulipata faida gani
 
tatizo press conference waandishi mnazitaka ili mpate pesa za kutoa habari,
kama unataka kujua mapato kawaulize makao makuu yao.?
Mwanzo wakati taarifa za kila mwezi zinasomwa.TRA walikuwa wanatoa hela kwa waandishi wa habari?
 
Nadhani wameamua kufuata utaratibu wa mahesabu, kila baada ya miezi 3 yanatakiwa kusomwa mapato na matumizi, kama ilivyo kwenye serikali za mitaa.
Kwa hiyo mwanzoni walikuwa hawafuati taratibu za ki mahesabu? Mbona mnakuja na majibu mepesi utafikiri hamkwenda shule!
 
Kama walivyoanzisha bila kushauriana na yeyote na ndivyo wamesitisha bila kushirikiana na yeyote,huo utaratibu haupo kisheria kwa hiyo hatuna haki ya kuhoji
Kiki imebuma hii.tukubali utaratibu huu ulianzishwa kwa sifa.
 
Kipindi kile watu walikuwa wanalipa na madeni ya nyuma wakajua makusanyo yatakuwa hvyohvyo kila siku.Sasa wamemaliza kulipa madeni,makusanyo ya kila mwezi na biashara mbaya ambayo wamesababisha wao wenyewe.Makusanyo ni aibu kutaja hadharani kama kipindi kile
 
Mbona mwanzoni tulikuwa tunatangaziwa, hizo website hazikuwepo?
Zilikuwepo, sasa kwanini media zisitangaze mpaka waitiwe press conference? Kwanini wasidakue data na kuandika magazetini?
Kwanini msilaumu media, mlaumu serikali?
 
Zilikuwepo, sasa kwanini media zisitangaze mpaka waitiwe press conference? Kwanini wasidakue data na kuandika magazetini?
Kwanini msilaumu media, mlaumu serikali
Wewe umeona hapo tumelaumu au tunauliza?
 
Back
Top Bottom