VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,140
- 18,004
Lowassa ni mwanasiasa mbobezi. Ni mwanasiasa aliyelelewa,kuiva na kujiimarisha ndani ya CCM. Ni kati ya wanasiasa ambao wamefanikiwa kuunda mfumo kupitia wafuasi na wanaowaunga mkono. Kama Mwenyekiti Mstaafu Kikwete alivyokiri,Lowassa si wa kubezwa.
Ingawa Lowassa anahusishwa na wizi na ufisadi,wapo wanaoamini ni msafi,mwema,imara na mwenye uwezo wa kuongoza. Wanamuunga mkono wapo vyama vyote. Ndiyo mfumo wenyewe alioujenga. Binafsi,nambeza kwa tahadhari kubwa. Simtenganishi na ufisadi hasa wa Richmond. Lakini,ana nguvu ya kimfumo.
TeamLowassa sasa ina mbinu ya ukimya. Kimyakimya. Hawajitaji kimahitaji na kuvuliwa taji. Wako kimya. TeamLowassa wamejipenyeza kwenye teuzi mbalimbali serikalini kimyakimya.
Kwa ilivyotapakaa TeamLowassa, isingewezekana teuzi ziwaruke wote viunzi!
Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
Ingawa Lowassa anahusishwa na wizi na ufisadi,wapo wanaoamini ni msafi,mwema,imara na mwenye uwezo wa kuongoza. Wanamuunga mkono wapo vyama vyote. Ndiyo mfumo wenyewe alioujenga. Binafsi,nambeza kwa tahadhari kubwa. Simtenganishi na ufisadi hasa wa Richmond. Lakini,ana nguvu ya kimfumo.
TeamLowassa sasa ina mbinu ya ukimya. Kimyakimya. Hawajitaji kimahitaji na kuvuliwa taji. Wako kimya. TeamLowassa wamejipenyeza kwenye teuzi mbalimbali serikalini kimyakimya.
Kwa ilivyotapakaa TeamLowassa, isingewezekana teuzi ziwaruke wote viunzi!
Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam