Rare Sapphire

JF-Expert Member
Jul 24, 2021
576
1,626
Juzi tarehe 2/2/2023 Mjumbe wa Shina namba 9 Mbezi Beach B Bw. Daudi anasema alipigiwa simu akiambiwa kuna mtu ambaye amefia kokoni, ambapo alipofika eneo la tukio akakuta kichwa cha mwanaume huyo kimetenganishwa na kiwiliwili.

Tukio hilo linaonekana kufanywa siku mbili au tatu kabla kutokana na mwili kutoa harufu ambapo Bw. Daudi aliwapigia simu polisi na serikali za mitaa Mbezi A (tukio limetokea katikati ya Mbezi Beach A na B) na kusimamia mwili huo mpaka polisi walipofika.

Bwana Daudi aendelea kueleza tukio hilo siyo la kwanza, kulishatokea tukio jingine maeneo ya kwa Rwakatare, lakini pia hapo ulipokutwa mwili wa mwanaume walishawahi kukuta mwili mwingine wa mwanamke ambaye mwili wake naye ulikutwa umeshaharibika sana ambapo ilibidi wamzike hapo hapo, na kusema kuwa eneo hilo ni hatarishi hasa wakati wa usiku, na wezi wa nyaya za TTCL wamewahi kutumia eneo hilo kama kichaka chao.

Bw. Daudi na mashuhuda wengine wameiomba serikali kukata miti eneo hilo, msitu ufyekwe ili kuwa salama kwa wakazi hao kutokana na matukio hayo ya kikatili pamoja na mto kusafishwa ili maji yaweze kupita vizuri yasiharibu makazi ya watu pindi mvua zinaponyesha.



Wasafi Media
 
Ukisikia polisi mtu kapewa kesi ya kichwa (kesi ya mauaji) ndio matukio kama haya ambayo polisi haijisumbui kuyachunguza ila wanakaa nayo kiporo.. Siku msipoenda sawa unapewa kesi ya mauaji

Au umenunua simu kwa mtu iliyoibwa, wakikukamata baada ya ku track simu. Unaoneshwa na ilo file. Lazima ukue mdogo na utatoa pesa nzuri tuu ili utoke.
 
Ukisikia polisi mtu kapewa kesi ya kichwa (kesi ya mauaji) ndio matukio kama haya ambayo polisi haijisumbui kuyachunguza ila wanakaa nayo kiporo.. Siku msipoenda sawa unapewa kesi ya mauaji
Kwa hiyo hili sasa ni kama gown anasubiri kuvalishwa mtu.
 
Poleni mno kwa wafiwa ni ngumu mno maana justice kwa wahanga hawa kupatikana itakua shida sana, this train stop KWA IGP office, jeshi la police inabidi livunjwe lote na liundwe upya, jeshi letu linatakiwa liwe la kisasa na liendane na technology ya dunia ya sasa, eti unaaambiwa mwili uliharibika sana ikabidi UZIKWE pale pale, hii ni NOOOOOO, police hawawezi kutambua mwili ilikuwepo kwenye crime scene kwa muda gani, police hawezi kutambua na kuko comfirm kama mhanga aliuliwa sehemu nyingine na Kuja kutupwa pale, toka Professor Shaba atangulie kwenye haki nchi haina pathologist!,(huyu alishawahi kumtambua marehemu kwa kutumia fuvu tu),police hatuna investigative foresinc dept, tulichokua nacho ni ffu ya kukimbizana na wapinzani mitaani, na mchango wa wana jf humu ni wa kushangaza, no hard questions kwa police, why waliruhusu mwili kuzikwa pale bila ya kukusanya evidence?,tunakimbilia kwenye simple solutions eti kata miti pale!!!,nchi yetu bado na ni bado sana, wako wapi wale wastaafu wa foresinc investigations ili wawe wanapeleleza case kama hizi au ❄ cases?
 
Poleni mno kwa wafiwa ni ngumu mno maana justice kwa wahanga hawa kupatikana itakua shida sana, this train stop KWA IGP office, jeshi la police inabidi livunjwe lote na liundwe upya, jeshi letu linatakiwa liwe la kisasa na liendane na technology ya dunia ya sasa, eti unaaambiwa mwili uliharibika sana ikabidi UZIKWE pale pale, hii ni NOOOOOO, police hawawezi kutambua mwili ilikuwepo kwenye crime scene kwa muda gani, police hawezi kutambua na kuko comfirm kama mhanga aliuliwa sehemu nyingine na Kuja kutupwa pale, toka Professor Shaba atangulie kwenye haki nchi haina pathologist!,(huyu alishawahi kumtambua marehemu kwa kutumia fuvu tu),police hatuna investigative foresinc dept, tulichokua nacho ni ffu ya kukimbizana na wapinzani mitaani, na mchango wa wana jf humu ni wa kushangaza, no hard questions kwa police, why waliruhusu mwili kuzikwa pale bila ya kukusanya evidence?,tunakimbilia kwenye simple solutions eti kata miti pale!!!,nchi yetu bado na ni bado sana, wako wapi wale wastaafu wa foresinc investigations ili wawe wanapeleleza case kama hizi au ❄ cases?
Livunjwe lote na liundwe upya🙄 sjui huwa mnawaza nn , simple Tu hvyo unaingia Gharama za kuvunja .... Sio rahs kama unavyofkria , tatizo la nchi ni usimamizi mbovu wa Sheria na umaskini wa watu wake ikiwemo hao polisi .... Hayo ndo ya kuyafanyia kaz na sio kuvunja
 
Binadamu bila sheria na hofu ya MUNGU hata wanyama wana nafuu.
 
Livunjwe lote na liundwe upya🙄 sjui huwa mnawaza nn , simple Tu hvyo unaingia Gharama za kuvunja .... Sio rahs kama unavyofkria , tatizo la nchi ni usimamizi mbovu wa Sheria na umaskini wa watu wake ikiwemo hao polisi .... Hayo ndo ya kuyafanyia kaz na sio kuvunja
Mkuu kwani kuvunjwa na kuundwa upya gharama zake ni ndogo kuliko kutengeneza mikoa mingine, wizara yetu ya home affairs nitaigawa mara mbili, police (ulinzi wa raia),na home dept(uraia &immigrations),nitaajiri vijana fresh, graduates kama 1500, hawa nitawasambaza kwa kozi za mwaka 1 kwenye nchi za Botswana, canada, UK,na Sweden 🇸🇪 wakajifunze jinsi gani wenzetu wanaendesha jeshi lao la police (nitabadilisha na kuwa service sio force),usimamizi wa kisheria ni tatizo la kiwajibikaji na uelewa mdogo (elimu duni),nitatengeneza police service ndogo but well equipped na technology, police wetu hawajui wapi pa kuanzia linapotokea issue kama hii, hili tukio ni la foresinc cops ndio walitakiwa wawe pale, sio ile defender, na WHY hadi leo miili inaondolewa na defenders za wazi?,wapi pathology investigation vans??
 
Juzi tarehe 2/2/2023 Mjumbe wa Shina namba 9 Mbezi Beach B Bw. Daudi anasema alipigiwa simu akiambiwa kuna mtu ambaye amefia kokoni, ambapo alipofika eneo la tukio akakuta kichwa cha mwanaume huyo kimetenganishwa na kiwiliwili.

Tukio hilo linaonekana kufanywa siku mbili au tatu kabla kutokana na mwili kutoa harufu ambapo Bw. Daudi aliwapigia simu polisi na serikali za mitaa Mbezi A (tukio limetokea katikati ya Mbezi Beach A na B) na kusimamia mwili huo mpaka polisi walipofika.

Bwana Daudi aendelea kueleza tukio hilo siyo la kwanza, kulishatokea tukio jingine maeneo ya kwa Rwakatare, lakini pia hapo ulipokutwa mwili wa mwanaume walishawahi kukuta mwili mwingine wa mwanamke ambaye mwili wake naye ulikutwa umeshaharibika sana ambapo ilibidi wamzike hapo hapo, na kusema kuwa eneo hilo ni hatarishi hasa wakati wa usiku, na wezi wa nyaya za TTCL wamewahi kutumia eneo hilo kama kichaka chao.

Bw. Daudi na mashuhuda wengine wameiomba serikali kukata miti eneo hilo, msitu ufyekwe ili kuwa salama kwa wakazi hao kutokana na matukio hayo ya kikatili pamoja na mto kusafishwa ili maji yaweze kupita vizuri yasiharibu makazi ya watu pindi mvua zinaponyesha.

View attachment 2505370

Wasafi Media
Mungu ampokee mja wake.

Maoni ya wsnanchi kukata miti ili kuweka usslama ninayaona si sahihi.

Hapo ni kuweka doria na ulinzi shirikishi.

Mazingira tunayahitaji kuyalinda pia
 
Back
Top Bottom