Mbugi
JF-Expert Member
- Jan 7, 2011
- 1,488
- 258
Hali halisi matatizo kama haya yataendelea kuwepo endapo viongozi wetu watakuwa si wepesi wa kusoma alama za nyakati, kwa mtazamo wangu tatizo lipo katika kwa viongozi wetu kujaribu kuleta mabadiliko pasipo kuangalia mazingira, ikiwa ni pamoja na kupata ushauri wa kutosha kwa vyombo vyote yaani wadau wenyewe, usalama wa taifa, viongozi ktk maana ya wawakilishi wa wananchi. pili badonaona lipo tatizo la msingi ktk mahusiano yaliyopo kwa serikali za mitaa na serikali kuu hasa pale inapojitokeza s/kuu kutoa mipango ya jumlajumla/maamuzi ya jumla ktk kuzitaka serikali za mitaa kufanyia kazi pasipo kuzingatia mazingira, utayari wa halmashauri ktk kutekeleza ikiwepo maandalizi ya kutosha kabla na hata baada ya utekelezaji. Mwanya huu unonekana zaidi kama tukio la leo mby ambapo machinga wanondoshwa kwa maamuzi yanayosimamiwa na mkoa wangari hajafanya maandalizi ya kutosha wapi wahusika waende/ na mbaya zaidi kwa nguvu pasipo uwepo wa mashauriano wa kutosha kwa pande mbili, mfano ni namna tu masoko yalivyoungua lakini pasipo majibu ya kutosha na namna uongozi wetu wa mkoa ulivyochukua hautua kwa upande mmoja, na fursa/nafasi waliyoitoa kwa wajasilimali walioathirika ktk kipindi hiki kabla hata ya kufikia hatua ya timuatimua, na hasa ukizingatia most of chinga wa leo ni wale waliounguliwa mali zao kwa mfululizo.
lakini pia hali inazidi kuwa mbaya zaidi inapoonekana zoezi linaandamana na sura ya kuwakomoa kwa zana ya kwamba wamechagua opposition, sasa wakione ni jambo jingine baya, kuchaguliwa kwa sugu hakuna tatizo anastahili apewe nafasi, kwa maslahi ya mbeya kama ambavyo tunawaasa cdm kutambua umuhimu wa kuheshimu maamuzi ya vikao na kushauriana na serikali kwa njia inayofaa badala ya maandamano/kauli chochezi kama kuwataka wananchi kupiga mawe polisi/mgambo wa jiji wanapotaka kutekeleza wajibu wao.
lakini pia hali inazidi kuwa mbaya zaidi inapoonekana zoezi linaandamana na sura ya kuwakomoa kwa zana ya kwamba wamechagua opposition, sasa wakione ni jambo jingine baya, kuchaguliwa kwa sugu hakuna tatizo anastahili apewe nafasi, kwa maslahi ya mbeya kama ambavyo tunawaasa cdm kutambua umuhimu wa kuheshimu maamuzi ya vikao na kushauriana na serikali kwa njia inayofaa badala ya maandamano/kauli chochezi kama kuwataka wananchi kupiga mawe polisi/mgambo wa jiji wanapotaka kutekeleza wajibu wao.