Mbeya yachafuka polisi wapambana na wamachinga

Mbeya yachafuka polisi wapambana na wamachinga

Nani mwenye ufahamu wa kutosha ayaonaye haya yanaendelea chini ya utawala wake asiseme kitu au asichukue hatua, akakaa kimya, wanachi wako wanapata majeraha makubwa namna hii kisa tu anayepatwa na ada hii hana maslahi na utawala wao!!!!!!
 
Chadema wakichukuwa nchi machinga wataruhusiwa kila mtaa..

Unafuka wewe unaleta utani wakati wananchi wanauwawa we jamaaa una rohio ya kishetani kabisa watu kama nyie hamtakiwi
tz hivi ungekuwa na ndugu zako huko na hali hii ilivyo ungeendelea kufuka namna hii...
 
how does chadema come in here? Hivi wewe una roho ya binadamu wewe? Kwanini comments zako hata siku moja either haziko neutral au zina mushkeli tu na lazima ziingize topics au information ambayo haijulikani hata ilipotokea...hebu uwe unarudi nyuma na kujiuliza imani uliyo nayo kama unaionyesha hata kimatendo au imani ni tofauti na matendo na uchungu anaopata binadamu yeyote kwako hauna maana!

kudos!!!!
 
'you can fool some people for sometime but you can not fool all the people, all the time, get up stand up! stand up for your right', by Bob Marley.

Nasikia Mbeya hakupitiki mwenye taarifa zaidi atujuze


BREAKING NUUZ: Polisi wapiga Risasi wananchi Mbeya washindwa tuliza Vurugu.. Sasa zimefika uyole wananchi wanashusha Bendera za CCM



kijana.jpg

majeruhi wa risasi za polisi katika vurugu za Mwanjelwa leo hii akiwa kapigwa kichwani. Hadi sasa kuna majeruhi wanne wa risasi, wawili kichwani, mmoja kwenye paja na mwingine mkononi
mzee.jpg

Mmoja wa majeruhi wa risasi za polisi katika vurugu za Mwanjelwa leo, Abel Mwalukali akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Rufaa Mbeya baada ya kupigwa risasi kwenye mkono.
VIJANA.jpg

Hali Badi ni Mbaya sana Kumefuka

Breaking Nuuuz: Machafuko Makubwa Mwanjelwa Mkoani Mbeya Polisi na Machinga wapigana vikali



mwanjelwa+11.11.11-5.jpg

Polisi wakijaribu Kuzuia Ghasia katika eneo hilo na kufukuza Wamachinga
mwanjelwa+11.11.11-2.jpg

Baadhi ya wananchi wakiwa wameokoka katika eneo hilo
mwanjelwa+11.11.11-4.jpg

Wamachinga Mbali mbali wakikimbia katika eneo la tukio wakati wa machafuko hayo yamepamba moto
mwanjelwa+11.11.11-7.jpg


Watu Mbali Mbali wakiwa wanakimbia ili kujiokoa na Hatari katika eneo hilo


Picha zote na Mpiga picha wetu maalum​



 
Well done Mbeya! This is good class to slow learning ccm and this is just the begining.
 
Wakuu nimesahau kidogo ile taharuki kubwa iliyotokea kule mwanza kandoro alikuwa yupo rock city wakati ule au alikuwa ameshaondoka maana huenda hii jinamizi la machinga linamwandama na huenda likamwondoa kabisa madarakani
 
Nimesoma michango mingi sana katika hii nyuzi, inavyoonekana wengi wetu tupo kisiasa zaidi! sawa inawezekana ni mzizi wa kila kitu sikatai, lakini KANDORO kusafisha jiji ni sahihi ila nafikiri mbinu aliyoitumia si sahihi. Kuna mmoja humu kaongelea ushawishi wa kukaa na wahusika na kuwaonyesha madhara na faida wa kusudio. Nafikiri hii mbinu KANDORO hakuitumia. Pili alitakiwa ajue anapowatoa wanachinga anawapelea wapi na ni kwavipi hilo eneo jipya atakalowapeleka wanunuzi watavutiwaje kupafikia.
Labda niongelee kwamba Watanzania hatuna tabia ya Usafi na utaratibu, si sahihi wafanyabiashara kufanya biashara zao kila sehemu, kwanza inasababisha uchafu. Kwa ambao mmebahatika kutembelea nchi za wenzetu mtakubaliana na mimi.Mimi nasema wazo si baya katu ila mbinu iliyotumika ndiyo haikufaa. Kandoro amesahau tabia yametokana na mazoea ya siku nyingi yanahitaji busara kumuelimisha mtu afahamu

Umesema sawa kabisa kuwa watanzania hatuna tabia ya kuzingatia usafi na taratibu, lakini Kandoro alitakiwa kutumia busara ktk namna ya kuwaondoa! Na bado ccm watapata shida mpaka watajifunza kuwa hizi ni nyakati nyingine!
 
1. Utashangaa kina mtoto wa mlimaji wanalaumu chadema badala ya kandoro???? ''' what a shame?
2. Kwa nini matatizo ya fujo na uonevu ni maeneo ya cdm zaidi????''' kuna mkono wa mtu!!'''
3. '''''''' waswahili wanasema usipoziba ufa utajenga ukuta!!!''''


mwisho wa chama cha magamba umekaribia sana...tena ...upo mlangoni...

peoples.....power!
Hata siku mwehu akinya karibu na geti la ikulu, watasema CDM.
 
Ahaa! Kumbe wewe Akili ukwaju!
Muulize pacha mwenzako kilichowafanya wapwa wake wawe walalamishi tuuuu!!!
kuanzia na ''wazee wao wa gerezani'' ni kitu gani.

Kichenchede!!
 
i cant believe tz sisi tuna aman hz vurugu si zetu, zimepandikizwa

kweli kuna watu wabishi hapa tz kusoma hujui hata picha tu au upovu ukiziwi


mpk sasa wamachinga wenzangu wapo kukinukisha
 
[SUB]kuna watu humu wanaliwa ndogo na yule mzee wa CCM asiye na meno ya mbele!!
mnamjua ee!! na mnawajua hao watu eee!![/SUB]
 
Kandoro na wenzake wote wanaoitwa wakuu wa mikoa na wilaya ni tatizo kubwa kwa usitawi wa demokrasia na maendeleo ya wananchi.
 
Yes muda wa kuchukua nchi ndio huu....Bado hali ni mbaya....so tusubirie tuone itakuwaje....Natamani kama nchi nzima iandamane maana nchi itachukuliwa kwa siku 5 maana wanachi wengi kuliko hao askari wao......
 
VURUGU MBEYA HATARI TUPU, POLISI NA RAIA WAHOFIA KUUWANA....................ONA PICHA HIZI KWA UFUPI
[h=3]HALI BADO SI SHWARI JIJI LA MBEYA MAPAMBANO BADO YANAENDELEA[/h]

[TABLE="class: tr-caption-container, align: center"]
[TR]
[TD] [/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="class: tr-caption"]Raia wema wakivukishwa barabara eneo la mapambano maeneo ya kabwe[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
[TABLE="class: tr-caption-container, align: center"]
[TR]
[TD] [/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="class: tr-caption"]Moja ya gari lililopasuliwa kioo na baruti[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
[TABLE="class: tr-caption-container, align: center"]
[TR]
[TD] [/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="class: tr-caption"]Wamachinga wakishangilia baada ya kuwazidi polisi nguvu[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
[TABLE="class: tr-caption-container, align: center"]
[TR]
[TD] [/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="class: tr-caption"]Nivurugu tupu maeneo ya soweto jijini mbeya[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
[TABLE="class: tr-caption-container, align: center"]
[TR]
[TD] [/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="class: tr-caption"]Wamachinga wakichochea moto wa matairi katikati ya barabara ya mbeya na tunduma[/TD]
[/TR]
[/TABLE]



[TABLE="class: tr-caption-container, align: center"]
[TR]
[TD] [/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="class: tr-caption"]Baadhi ya wamachinga wakiwa wamelipindua gari yaina ya toyota na kusimama juu yake huku wakitamka maneno makali kwa polisi na jiji la mbeya kwa kuwanyanyasa katika biashara zao


Wananchi wakisubiri mkutano na mkuu wa mkoa baada ya Serikali kusalimu amri.[/TD]
[/TR]
[/TABLE]

[TABLE="class: tr-caption-container, align: center"]
[TR]
[TD] [/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="class: tr-caption"]Moja ya mabango waliyobeba wamachinga hao[/TD]
[/TR]
[/TABLE]

[TABLE="class: tr-caption-container, align: center"]
[TR]
[TD] [/TD]
[/TR]
[TR="bgcolor: red"]
[TD="class: tr-caption"]Wamachinga wakiwazomea polisi eneo la kabwe[/TD]
[/TR]
[/TABLE]



[TABLE="class: tr-caption-container, align: center"]
[TR]
[TD] [/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="class: tr-caption"]Moja ya gari lililobinuliwa na kuwekwa katikati ya barabara ya mbeya tunduma[/TD]
[/TR]
[/TABLE]



[TABLE="class: tr-caption-container, align: center"]
[TR]
[TD] [/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="class: tr-caption"]Mmachinga akiwarushia jiwe kwa kutumia manati yaani ni hatari tupu[/TD]
[/TR]
[/TABLE]

[TABLE="class: tr-caption-container, align: center"]
[TR]
[TD] [/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="class: tr-caption"]Askari wa kutuliza fujo naye akiwarushia bomu la machozi wamachinga wanaoandamana[/TD]
[/TR]
[/TABLE]

[TABLE="class: tr-caption-container, align: center"]
[TR]
[TD] [/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="class: tr-caption"]Naye mwandishi wetu wa mbeya yetu Joseph Mwaisango alionja joto ya jiwe baada ya kutupwa ndani ya gari ya polisi kwa kosa la kupiga picha matukio hayo ya wamachinga na polisi baadaye aliachiwa na kuendelea na kazi yake[/TD]
[/TR]
[/TABLE]

[TABLE="class: tr-caption-container, align: center"]
[TR]
[TD] [/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="class: tr-caption"]RISASI ZA MOTO NAZO ZIMETUMIKA KATIKA TUKUKIO HILI[/TD]
[/TR]
[/TABLE]

[TABLE="class: tr-caption-container, align: center"]
[TR]
[TD] [/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="class: tr-caption"]MABOMU YA MACHOZI NDIYO USISEME KILA MAHALI YAMETAPAKAA[/TD]
[/TR]
[/TABLE]




[TABLE="class: tr-caption-container, align: center"]
[TR]
[TD] [/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="class: tr-caption"]Tazama mwenyewe ndugu yangu...............................................



VURUGU kubwa zimejitokeza jana eneo la Mwanjelwa Jijini Mbeya zikihusisha wafanyabiashara ndogondogo maarufu kama wamachinga na jeshi la polisi ambapo askari hao walitumia maguruneti ya machozi bila mafanikio.

Chanzo cha vurugu hizo kilielezwa kuwa ni kutokana na maamuzi ya uongozi wa Jiji hilokuwaondoa kwa nguvu wafanyabiashara hao eneo la Mwanjelwa huku baadhi yao wakiwa wahanga wa kuunguliwa masoko mawili yaliyoteketeza mitaji yao Jijini hapa.

Sakata hilo lililodumu kwa muda wa masaa Nane huku Jeshi la polisi likizidiwa nguvu na kuomba msaada wa askari wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kikosi cha Itende, hali bado iliendelea kuwa mbaya ambapo wamachinga hao kwa kushirikiana na watu waliojiita wanaharakati wakijihami kwa kutumia mawe na kuchoma moto magurudumu.

Vurugu hizo ambazo zilianza majira ya saa mbili asubuhi, zilisababisha biashara zote zlizopo eneo la Mwanjelwa, Soweto na Uyole kufungwa huku mtu mmoja akithibitika kupigwa risasikatika mguu wake na kupelekwa hospitali ya uhai iliyopo jijini hapa.

Aliyepigwa risasi na kusaidiwa na wananchi wenzake waliojitambulisha kuwa wanaharakati kupelekwa hospitalini alijitambulisha kwa jina la Gabriel Mwasomola.

Sanjari na hayo wanafunzi watatu wa shule ya Msingi Sinde iliyopo katikati ya Jiji hilo waliumizwa na kuzimia baada ya kupigwa na mabomu hayo huku zaidi ya wanafunzi 40 wameacha mtihani wa Taifa wa darasa la Nne baada ya kukimbia mabomu kuhofia maisha yao huku Mkuu wa shule hiyo Shadrack Mwakasyama akithibitisha kutokea kwa hali hiyo.

Baadhi ya wafanyabishara waliohojiwa walisema kuwa hali hiyo ilisababishwa na Mkurugenzi wa Jiji la Mbeya ambaye alitoa amri ya kuondolewa wafanyabiashara hao pasipo kuwatafutia sehemu nyingine za kufanyia biashara zao.

Mwenyekiti wa wafanyabiashara hao Patrik Mwasanguti alisema awali walipata maelekezo kutoka kwa Meya wa Jiji Athanas Kapunga kuwa walipaswa kuendelea kufanya biashara zao eneo hilo mpaka Novemba 9 mwaka huu ambapo Serikali ingekuwa imewatafutia eneo linguine lakini baada ya kupita tarehe hiyo hakuna kiongozi yeyote aliyejitokeza kuzungumz naye badala yake walishangaa kuanza kuondolewa kwa nguvu.

Katika vurugu hizo watu kadhaa walijeruhiwa na na kukamatwa huku baadhi wakisadikika kuwa walipoteza maisha wakiwemo raia na askari polisi.

Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa Mbeya Anacletus Malindisa alipotafutwa kwa njia ya simu yake ya kiganjani hakuweza kupokea simu hiyo na baadaye taarifa zilieleza kuwa alikuwa katika kikao cha Ulinzi na usalama cha mkoa wa Mbeya kilichokuwa kikiongozwa na Mkuu wa mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro ambaye alilazimika kuahirisha ziara yake katika wilaya ya Mbozi ili kunusuru vurugu hizo.

Mpaka tunaenda mitamboni, Serikali iliamua kusalimu amri na kuitisha mkutano mkubwa wa hadhara katika eneo la Kabwe kwa ajili ya kutafuta suluhu.

Wakati huohuo taarifa zilizagaa kuwa baadhi ya waandishi wa habari waliokuwa wa kwanza kuonekana katika tukio hilo kuwa walikuwa wameuawa na kwa kupigwa risasi na Polisi hali ambayo ilisababisha mgawanyiko mkubwa kati ya wanahabari.

Waandishi hao ni pamoja na mwandishi wa Tanzania Daima ambaye pia ni mmiliki wa Blog ya kalulunga.blogspot.com Gordon Kalulunga na mmiliki wa mbeyayetu.blogspot.com Joseph Mwaisango ambao wote walipotafutwa kwa njia ya simu walisema kuwa walikuwa salama licha ya kutokea taflani kidogo kati yao na baadhi ya Vigogo wa Jeshi hilo wilaya ya Mbeya katika kutekeleza majukumu ya[/TD]
[/TR]
[/TABLE]

















 
Chadema wakichukuwa nchi machinga wataruhusiwa kila mtaa..

How does Chadema come in here? hivi wewe una roho ya binadamu wewe? kwanini comments zako hata siku moja either haziko neutral au zina mushkeli tu na lazima ziingize topics au information ambayo haijulikani hata ilipotokea...hebu uwe unarudi nyuma na kujiuliza imani uliyo nayo kama unaionyesha hata kimatendo au imani ni tofauti na matendo na uchungu anaopata binadamu yeyote kwako hauna maana!
Unajua MaryGeorge watu wengine bila kuchomeka neno Chadema huwa hawana cha kujadili wanalazimisha hata pasipo lengo lake waanze kubishana.
 
natamani kulia ila moyo unaniuma c kwasababu mimi mtu wa mbeya hapana bali nimuonapo mzee kama huyu aliyepigwa risasi kichwani na mwengine na hata mtoto akikimbia kama kafungwa injini ya pikipiki kweli naumia sana leo ni kwetu mbeya na je kesho cjui kwa kina mangi na wasukuma na haata pia shemeji zangu wasambaa na wazigula.

Huku kutachimbika mapanga tushaana kuyanoa
 
Updates za Mbeya? maana tunaambiwa hadi jana saa nne usiku mabomu yalikuwa yanaendelea.
 
Back
Top Bottom