Mbeya: Utitiri wa redio ni kero nyingine

Mbeya: Utitiri wa redio ni kero nyingine

N'yadikwa

JF-Expert Member
Joined
Aug 10, 2014
Posts
7,993
Reaction score
12,044
Nasema ni kero kwa sababu hizo Fm Radios Mbeya zina watangazaji wasiozingatia weledi na hawana ubunifu, watangazaji wanabanyanga sana Kiswahili, sijui ndo wamiliki kushindwa kuwalipa?

Kwa ufupi redio za Mbeya hazina mvuto kiasi kwamba wananchi wengi wanapendelea kusikiliza radio za nje KV Ebony FM na za Dar.

Redio za Mbeya zenye nafuu ni kama tatu tu nje ya karibia redio 13, nazo ni UU-FM, Bomba Fm na Mbeya Fm.

Orodha ya redio Mbeya:
1 Mbeya Fm
2. Ushindi Fm
3. Ilasi Fm
4. Highlands Fm
5. Kyela Fm
6. Sweet Fm
7. Generation Fm
8. Baraka Fm
9. Chai Fm
10. Bomba Fm
11. Kuna moja ipo Uyole mpya
12. Mpanji Fm
13. Orodha ingali inaendelea...

Hebu kuweni wabunifu, ajirini vijana wenye weledi na sifa za utangazaji. Mnachosha na hamsikiliziki na watu makini.

Nimefanya huu utafiti kitambo sasa.

By n'yadikwa
 
Naikumbuka chai fm pale tukuyu ilianza kama Efm ya hapa dar ni miziki tu ful time, saahii vipi wameanza kuboronga?
 
Inapofika muda wa habari sijui inakuwaje, taifa linapokuja na malengo ya kuwa taarifa ya habari ya saa mbili tu iwe moja wanaopinga watafakari upya,
Mtu wa Kyela anapata taarifa za kyela, wa Mbeya mjini naye hivyo hivyo ila inapofika suala la kitaifa ni vyema tukaliangalia kwa jicho chanya. Mapungufu yanayotazamiwa yatafutiwe 6fumbuzi ili taarifa ya habari kwa taifa zima iwe moja ifikapo SAA MBILI USIKU TU..... taarifa za habari ziwepo za stesheni husika kwa masaa tofauti
 
Nadhani muwasilishaji, ameshindwa kujipanga ana lalamika tu. Ukidhindwa so uweke CD?
 
Dodoma yale yale tu

A fm
Abm fm
Nyemo fm
Kifimbo fm
Dodoma fm
Impact fm
Mwangaza fm
Uzima fm
Ras fm

Vingine nimevisahau. Wajitahidi kuwa wabunifu, saiv kila redio wanataka watangaze kama Clouds wanavotangaza.
 
Ule muswada wa habari unataka wote wawe na degree,hapo ndo radio nyingi zitafungwa
 
Naomba tafsiri ya neno utitiri, mi navyojua ni wadudu wadogo flani ivi.
 
Inapofika muda wa habari sijui inakuwaje, taifa linapokuja na malengo ya kuwa taarifa ya habari ya saa mbili tu iwe moja wanaopinga watafakari upya,
Mtu wa Kyela anapata taarifa za kyela, wa Mbeya mjini naye hivyo hivyo ila inapofika suala la kitaifa ni vyema tukaliangalia kwa jicho chanya. Mapungufu yanayotazamiwa yatafutiwe 6fumbuzi ili taarifa ya habari kwa taifa zima iwe moja ifikapo SAA MBILI USIKU TU..... taarifa za habari ziwepo za stesheni husika kwa masaa tofauti

Sio kwa shirika hili letu la TBC. Acha kujifanya unauzalendo kuliko wote waliokataa kujiunga habari ya saa 2. Ukitaka ushahidi angalia kinachoendelea mida hii TBC- Live Bunge.
 
Mbeya Mbona cha mtoto? Arusha vi redio vimefika mia. Vyote vinatangaza yale yale, vijitoto vya kike vinavyopigwa miti hovyo mjini, halafu havijui chochote kile.
 
Inapofika muda wa habari sijui inakuwaje, taifa linapokuja na malengo ya kuwa taarifa ya habari ya saa mbili tu iwe moja wanaopinga watafakari upya,
Mtu wa Kyela anapata taarifa za kyela, wa Mbeya mjini naye hivyo hivyo ila inapofika suala la kitaifa ni vyema tukaliangalia kwa jicho chanya. Mapungufu yanayotazamiwa yatafutiwe 6fumbuzi ili taarifa ya habari kwa taifa zima iwe moja ifikapo SAA MBILI USIKU TU..... taarifa za habari ziwepo za stesheni husika kwa masaa tofauti

HOja yako ina mashiko.
 
Ule muswada wa habari unataka wote wawe na degree,hapo ndo radio nyingi zitafungwa

Hicho kipengele kitafaa sana wasikiondoe maana hiyo tasnia imevamiwa sana na makanjanja ndo maana waandishi wanadharauliwa japo kazi yao ni muhimu sana.
CC: Dotto mnzava,Pasco.
 
Mkuu kuna kiredio hapa Arusha kinaitwa mj fm watangazaji wake sjui walipatikanaje, wanaweza kuwa wanatangaza hari yenye simanzi kubwa lakini wakawa wanacheka, ni ujinga ujinga tu
 
Inapofika muda wa habari sijui inakuwaje, taifa linapokuja na malengo ya kuwa taarifa ya habari ya saa mbili tu iwe moja wanaopinga watafakari upya,
Mtu wa Kyela anapata taarifa za kyela, wa Mbeya mjini naye hivyo hivyo ila inapofika suala la kitaifa ni vyema tukaliangalia kwa jicho chanya. Mapungufu yanayotazamiwa yatafutiwe 6fumbuzi ili taarifa ya habari kwa taifa zima iwe moja ifikapo SAA MBILI USIKU TU..... taarifa za habari ziwepo za stesheni husika kwa masaa tofauti

Mawazo ya kitoto na yakufikilika. Ni sawa na kusema wote sisi tuwe dini moja eti kwasababu Mungu ni mmoja. Mungu na kutuumba kote kule bado swala la kuabudu katuachia tuchague na maisha yanasonga. Ukiichoka dini unahamia nyingne tu ambayo ni bora zaid kwako. Kwa mfano mimi tangu Tido aondoke tbc niliacha kuitazama, na sijutii afu leo king'amuzi changu unichagulie taarifa ya habari. Semeni tu kwamba ishu hapo ni kutaka kuikwamua tbc kiuchumi ili iweze kupata wazamin wa kutosha. Walibugi wenyewe
 
Mbeya Mbona cha mtoto? Arusha vi redio vimefika mia. Vyote vinatangaza yale yale, vijitoto vya kike vinavyopigwa miti hovyo mjini, halafu havijui chochote kile.

Duh mia mkuu,basi mmetisha tutajie alau 10 mkuu
 
Back
Top Bottom