Mbeya ni jiji lenye barabara mbovu kuliko zote Tanzania

Sep 10, 2023
20
65
Nimekuwa mkazi wa Mbeya kwa kipindi cha zaidi ya miaka minne sasa, lakini kati ya majiji yote niliyowahi kutembea katika kipindi chote, sijawahi kuona jiji lenye barabara mbovu kama Mbeya. Kuna barabara za lami zimekuwa na mashimo makubwa kwa zaidi ya miaka miwili, na ni barabara zenye umuhimu sana, kama vile barabara za kuingia na kutoka soko la Soweto, barabara ya Isyesye, Ituha, Makunguru, Veta ya Machinjioni, Block T, barabara za Stand ya Nane, na barabara ya kuingia na kutoka Stand ya Dadadala Airport ya zamani. Zote hizi ni mbovu kwa kipindi kirefu, na hii inaleta changamoto kubwa kwa wakazi wa maeneo haya.

Kwa muda sasa, tumekuwa tukishuhudia hali ya barabara hizi ikizidi kudorora. Hali hiyo imesababisha matatizo mengi, ikiwa ni pamoja na:

1. Usalama wa Watumiaji wa Barabara: Barabara hizi zina mashimo na sehemu zilizoharibika, na hivyo kuongeza hatari ya ajali na majeruhi kwa watu wanaotumia barabara hizi.

2. Uharibifu wa Magari: Kutokana na ubovu wa barabara, magari mengi yameharibika na wamiliki wamekuwa wakilazimika kutumia gharama kubwa kwa ajili ya matengenezo.

3. Usafirishaji na Biashara: Barabara hizi zina jukumu muhimu katika usafirishaji wa bidhaa na shughuli za biashara katika eneo letu. Ubovu wa barabara umesababisha usumbufu mkubwa katika shughuli hizi za kiuchumi.

Kwa sasa, kwa baadhi ya maeneo, kama vile Isyesye, inawalazimu vijana wa maeneo hayo kufanya kazi ya kujaza kifusi kwenye mashimo ili kusaidia watumiaji wa barabara hizo.

Tunatambua kwamba kurekebisha barabara kunaweza kuwa na gharama kubwa, lakini serikali yetu ya eneo au mamlaka ya barabara inapaswa kutoa kipaumbele kwa suala hili na kuanzisha hatua za haraka kurekebisha barabara hizi. Pia, tunaomba kuwe na uwazi katika matumizi ya fedha za umma kwa miradi ya miundombinu ya barabara.
 
Kabwe mashine za mpunga je?? Kuko kama dampo kipindi chamvuaa hakupitiki alafu angaliankweny pato la taifa mkoa unachangia kias gan

MFANO BARABARA ZA NDANI YA MKOA UNATOA KM 20 NKITAJA MAENO YANAYO HITAJI BARABARA SIDHAN KAMA ZITAFIKA POPOTE.

1 IYUNGA KWENDA LUMBIRA MPAKA IWAMBI
2.NJIA PANDA MAPELELE MPAKA VETA
3.KIWIRA MOTEL JUHUD MPAKA MAPELE MWISHO.
3 SOKO DOGO KUTOKEA MLIMA ISANGA.
4.NJIA PANDA KAROBE MPAKA BWALA MAJI MACHAFU
5.NJIA PANDA MBEMBELA MPAKA HALENGO KUTOKEA IKUTI.
6.GHANA MPAKA NZOO KUPITIA IZIWA.
7. IGANZO KUPITIA IGODIMA MPAKA MCHINJION.
HIZO NI CHACHE NA BADO WANALALAMIKA
BAJAJ ZIMEJAA MAIN ROAD ZITAENDA WAPI WAKAT MKOA UNA BARANARA MOJA YA TANZ ZAMBIA .

NASUBIR SIJUI TULIA ATAWAMBIA NINI WATU 2025 WA MITAAAN MANA WAO HIYO NJIA NNE HAIWAHUSU.
 
Si wanaje ga barabara 4 kutoka Nsalaga Hadi airport pia wanajen ga ya mchepuko kule Uyolr Hadi Senjele
 
Wapi Majengo/ghana/mabatini/machinjioni/kule chini makaburini wapi tena kuleee aah jina limenitoka.
 
Nimekuwa mkazi wa Mbeya kwa kipindi cha zaidi ya miaka minne sasa, lakini kati ya majiji yote niliyowahi kutembea katika kipindi chote, sijawahi kuona jiji lenye barabara mbovu kama Mbeya. Kuna barabara za lami zimekuwa na mashimo makubwa kwa zaidi ya miaka miwili, na ni barabara zenye umuhimu sana, kama vile barabara za kuingia na kutoka soko la Soweto, barabara ya Isyesye, Ituha, Makunguru, Veta ya Machinjioni, Block T, barabara za Stand ya Nane, na barabara ya kuingia na kutoka Stand ya Dadadala Airport ya zamani. Zote hizi ni mbovu kwa kipindi kirefu, na hii inaleta changamoto kubwa kwa wakazi wa maeneo haya.

Kwa muda sasa, tumekuwa tukishuhudia hali ya barabara hizi ikizidi kudorora. Hali hiyo imesababisha matatizo mengi, ikiwa ni pamoja na:

1. Usalama wa Watumiaji wa Barabara: Barabara hizi zina mashimo na sehemu zilizoharibika, na hivyo kuongeza hatari ya ajali na majeruhi kwa watu wanaotumia barabara hizi.

2. Uharibifu wa Magari: Kutokana na ubovu wa barabara, magari mengi yameharibika na wamiliki wamekuwa wakilazimika kutumia gharama kubwa kwa ajili ya matengenezo.

3. Usafirishaji na Biashara: Barabara hizi zina jukumu muhimu katika usafirishaji wa bidhaa na shughuli za biashara katika eneo letu. Ubovu wa barabara umesababisha usumbufu mkubwa katika shughuli hizi za kiuchumi.

Kwa sasa, kwa baadhi ya maeneo, kama vile Isyesye, inawalazimu vijana wa maeneo hayo kufanya kazi ya kujaza kifusi kwenye mashimo ili kusaidia watumiaji wa barabara hizo.

Tunatambua kwamba kurekebisha barabara kunaweza kuwa na gharama kubwa, lakini serikali yetu ya eneo au mamlaka ya barabara inapaswa kutoa kipaumbele kwa suala hili na kuanzisha hatua za haraka kurekebisha barabara hizi. Pia, tunaomba kuwe na uwazi katika matumizi ya fedha za umma kwa miradi ya miundombinu ya barabara.
Mbeya inabidi irudi kuwa manispaa
 
Hadi aibu aisee.barabar ya isyesye nlienda nkasema nchi yetu watu wanaichezea sana mashimo kama nn..iv inawezwkanaje hku iyunga nzovwe Hadi iwamb kusiwe na Barbara hata moja...no aibuu saana
 
Nimekuwa mkazi wa Mbeya kwa kipindi cha zaidi ya miaka minne sasa, lakini kati ya majiji yote niliyowahi kutembea katika kipindi chote, sijawahi kuona jiji lenye barabara mbovu kama Mbeya. Kuna barabara za lami zimekuwa na mashimo makubwa kwa zaidi ya miaka miwili, na ni barabara zenye umuhimu sana, kama vile barabara za kuingia na kutoka soko la Soweto, barabara ya Isyesye, Ituha, Makunguru, Veta ya Machinjioni, Block T, barabara za Stand ya Nane, na barabara ya kuingia na kutoka Stand ya Dadadala Airport ya zamani. Zote hizi ni mbovu kwa kipindi kirefu, na hii inaleta changamoto kubwa kwa wakazi wa maeneo haya.

Kwa muda sasa, tumekuwa tukishuhudia hali ya barabara hizi ikizidi kudorora. Hali hiyo imesababisha matatizo mengi, ikiwa ni pamoja na:

1. Usalama wa Watumiaji wa Barabara: Barabara hizi zina mashimo na sehemu zilizoharibika, na hivyo kuongeza hatari ya ajali na majeruhi kwa watu wanaotumia barabara hizi.

2. Uharibifu wa Magari: Kutokana na ubovu wa barabara, magari mengi yameharibika na wamiliki wamekuwa wakilazimika kutumia gharama kubwa kwa ajili ya matengenezo.

3. Usafirishaji na Biashara: Barabara hizi zina jukumu muhimu katika usafirishaji wa bidhaa na shughuli za biashara katika eneo letu. Ubovu wa barabara umesababisha usumbufu mkubwa katika shughuli hizi za kiuchumi.

Kwa sasa, kwa baadhi ya maeneo, kama vile Isyesye, inawalazimu vijana wa maeneo hayo kufanya kazi ya kujaza kifusi kwenye mashimo ili kusaidia watumiaji wa barabara hizo.

Tunatambua kwamba kurekebisha barabara kunaweza kuwa na gharama kubwa, lakini serikali yetu ya eneo au mamlaka ya barabara inapaswa kutoa kipaumbele kwa suala hili na kuanzisha hatua za haraka kurekebisha barabara hizi. Pia, tunaomba kuwe na uwazi katika matumizi ya fedha za umma kwa miradi ya miundombinu ya barabara.
Mbeya barabara nyingi zinajengwa chini ya kiwango sana. Ndio maana zinaharibika hata kabla ya mwaka mmoja. Refer barabara ya stand kuu kwenda Meta. Ilikabidhiwa mpya lakini kable ya miezi sita ikaanza kuonekana na mashimo.
Mimi nadhani Rushwa inalimaliza lile Jiji
 
kumchagua sugu kuliwacost sana kwa miaka kadhaa ile, tulia alipokuja naye hajafanya chochote labda kwasababu serikali haina hela. ila halistahili hata kuitwa jiji.
 
Yaan kama kuna wezekqna TARURA ya mbeya wasipewe hata kilometa moja kujenga mana wao ndo wanajenga mashimo sio barabara.

Na hata wakipewa watoe contactor ohoo ndo balaaa barabara ya crossway mpaka utokee isanga ina mshimo utazan kuna wat hjwa wanakuja kuchimba usiku. Wanarudia kila siku na sehem hizo hizo walizo rudia ndo zinaharibika
 
Nimekaa week 2 mbeya nimezunguka kote chunya, iyole, mbeya mjini, mpemba, tunduma kote huko sijaona dem mkali wote wabovu sijui tatizo nn.
 
Back
Top Bottom