Mbeya long time kitambo

Mbeya long time kitambo

Kulikuwa na kucheza madoyomba, kudaka Magh'ela kuna yanayouma tulikuwa tunayaita polisi(yalikuwa na rangi nyeupe na nyeusi) yale mekundu tulikuwa tunaamini hayaumi lakini sometimes unajichanganya unajikuta unapigwa mishale ya maana
 
Duh, hakika bujibuji unaijua Mbeya! Umenikumbusha mbali sana. Enzi hizo nachezea timu ya Black Town then nikahamia Jogoo basha zote za Br ya 3.Zote ligi Ilikuwa kiwanja ngoma.
Pia namkumbuka Dr. Kasimbazi alikuwa na gonna lake pale Friends Corner bar, hatareee. Mzëe akishalewa anatoka machafu na gari yake Toyota datsun single cabin huyoo anarudi zake rufaa hospital kazini kwake. Mchana kweupee keshalewa.
Wale wavuta petrol Walikuwa ndugu 3,walikuwa balaa wakishavuta. Mjini sokomatola na mtaani kwao karibu na uwanja ngoma hakukaliki. Walikuwa na misauti minene balaa!Duh,mleta post hii umenikumbusha mbali sana.
 
Nonde Machinjioni
Huyo pusher alijulikana kwa jina la Mwasimba aka Shetani. Alimuoa dada mmoja anaitwa Christina Waya. Huyu dada alikuwa classmate wangu Itiji primary school miaka ya 1987-90 alipompatia mimba na kukatisha masomo darasa la 4. Akamchukua Jumla na kuwa Mkewe. Jamaa alikuwa mbabe balaa hadi polisi Walikuwa wanapata wakati mgumu kumkamata kwa biashara yake ya bangi mitaa ya Nonde.
 
Bujibuji ni Dokta Harison Mwakyembe chunguzeni mtaniambia
😀😀😀😀😀😀😀 nouma sana yani kabudi naye ndani huu mtandao never die i love mbeya first time 2013 july
 
Huyo pusher alijulikana kwa jina la Mwasimba aka Shetani. Alimuoa dada mmoja anaitwa Christina Waya. Huyu dada alikuwa classmate wangu Itiji primary school miaka ya 1987-90 alipompatia mimba na kukatisha masomo darasa la 4. Akamchukua Jumla na kuwa Mkewe. Jamaa alikuwa mbabe balaa hadi polisi Walikuwa wanapata wakati mgumu kumkamata kwa biashara yake ya bangi mitaa ya Nonde.
Jiwegangi kwa miaka hiyo Itiji bila shaka walimu wafutao utakuwa unawakumbuka vizuri Bwalya, Mwakajila, Ndowa, Kyusa, Kalinga, Manase, Mwanakaya n.k.
 
Kuna jamaa alikuwa anaitwa Bob G alikuwa mzee wa magendo kutoka nchi mbalimbali hasa malawi. Alikuwa na cruiser wakati kipindi hicho polisi wana hyundai. Aisee Hatari mno. Nasikia jamaa alikuwa anafukuzwa na polisi akamwagaga rambo ya shilingi mia mia pale uyole watu wakaingia barabarani polisi wakashindwa kupita.
Kuna jamaa walikua wanaiba ng'ombe hata 30 na wanawaswaga barabani wakiwa na gobole na polisi wanagwaya. I miss that Mbeya
Na Bob Edgar
Mi si wa mbeya ila nilisoma mbeya, Bujii umewasahau na MTC ? Wale wanachuo wakorofi?
 
a6c73e94f7cf88fde7738355946e1da0.jpg
Maili tano hapo karibu na mwansekwa
 
Hapo jirani na kwenu, kwa kina Makolija walikuwa na Linolino hapo kwa kina Max Nanyaro walikuwa na Nishio
Makunguru zilikuwepo daladala za mama Monica aliziandika"nashangaa gari" rout ni standkuu to uyole
 
hakika unaifaham mbeya na watu wake....mimi miaka hyo nilikuwa natafutia riziki pale iringa/makambako na kuna muda nilifata mizigo ama kupeleka bidhaa kwenda mbeya kwa kwel ilikuwa mbeya kweli.......
Mtoa uzi nimemkubali sana , nilifika mbeya kwa mara ya kwanza nikiwa kijana miaka ya tisini. Then kuanzia mwaka 2009 nikarudi rasmi kama mwajiriwa kwa kuhamishiwa huku mpaka leo na makazi yangu ni uyole njia panda. Amenipa historia nzuri sana ya Mbeya na mengi nilikuwa siyafahamu. Hongera sana kwa mtoa mada.
 
HII NDIO ILIKUWA MBEYA BWANA

1. Enzi hizo alikuwepo mtu anaitwa Jombi, kudhihirisha ubabe kwa wenzako lazima uwaambie Mimi ni "Jombi"

2. Kulikuwa na basi zinaitwa Kiswele..engine nyuma, Dar - Mby faster, Mafegi hii ilikuwa na vijihoni vya Ukweli,usisahau Mv Saratoga, Tunyande bus service, Zainabus

3. Kulikuwa na wavuta petroli, hawa jamaa walikuwa km 5 hivi, wachafu wanatembea pamoja mitaa ya BP uhindini wakiwa na makopo na vitambaa vilivyoloa petrol wanavuta.

4. kiwanja ngoma, hapa Soka lilipigwa bwana, timu yangu ya Mtaa Snow White chini ya Key, kina Baba Jeni. Basket ball ilikuwa pale Centre, tulikuwa na chama letu Mbeya Flames.

5. Town pale palikuwa na vichaa hatari kuna "Tiotio" huyu alikuwa anachapa ngeli balaa, Merry Kichaa alikuwa na alergy na watu weupe, akikuotea atakukimbizaa na stick utakula. Pale Mbeya Recto ndio ilikuwa km Makao makuu ya vichaa walikuwa kibao

5.Pale Bomani palikuwa na Mzee mmoja mfupi nakumbuka jina moja la Mwakifuna,nilifanya jitihada ili kumuona tu maana kutokumjua na kumuona ilikuwa ni weakness kubwa.

6. Kipindi hicho Disco lilikuwa Mount Livingstone na Rift valley, Soggy doggy enzi hizo akiitwa Wasape na Sugu- 2 Proud, hipop ilinoga bwana.

7. Mtakumbuka Mbeya tulikuwa na ukumbi Wa Sinema pale opposite na Ofisi za Posta Town, Muvy ya Hatya ilifunika sana enzi zile.

8. Miaka ile bwana mvua ilikuwa inapiga km gharika,sometimes ilikuwa inamwagwa barafu km ulaya,mlima Loleza ulikuwa ukifunikwa theluji kwa siku kadhaa. Radi sasa, hatariii mpaka nyumba ina Shake.

9. Siku ya Jumamosi ilikuwa ya kuosha mbwa,mbwa wote walikuwa wanapelekwa josho pale Mifugo,nyuma ya Kanisa la Roman,mkishamaliza kuogesha mnaanza kugombanisha Mbwa,mbwa Wa kizungu walikuwa wanaogopwa kupambanishwa na Wa kienyeji ikiaminika wananguvu balaa.

10. Uzunguni enzi hizo kulikuwa na matunda ya aina mbalimbali,watoto walikuwa wanatoka maeneo kadhaa ikiwemo Isanga kuja kuchuma maparachichi,mang'ang'a,mafyulizi,mapohora,mapera nk.

11. Mwanjelwa.enzi hizo iliitwa Doksi au Njelii, mitumba viwango,raba Kali,msela ukitupia vya doksi umemaliza.

12.Enzi zile ukisoma Sisimba na Azimio unafunika,Shule ya International ilikuwa Umoja primary school, waliosoma hapo hata kupishana nao unaogopa

13. Kuruka ukuta Wa Uwanja Wa Sokoine au kuingia uwanjani kupitia Bomba la maji ya mvua wakati Wa mechi ilikuwa ujanja balaa.

14. Ukisikia Shule za Sekondari Iyunga, Sangu, Loleza, Mbeya Day zilikuwa na kila aina ya sifa.Sangu kulikuwa na vichwa lazima uvitambue wababe km Simply na Kambosonic waliogopwa.

15. UMISETA sasa, dah, achaa..hapa Lutengano hapa Mwakaleli, boli lilitandazwa,kikinuka uwanjani ilikuwa km vita,makwanja na fimbo hujui vilipotokea,ukizubaa utakula mkono balaa

16. Kuna mdada walikuwa hatari alikuwa anatembeza kichapo kwa wanaume balaa walikuwa anatokea ilemi alifahamika kwa jina la Jeni.

17 Kuna jamaa alikuwa mtata sana mtaa Wa mafiati, makunguru, juakali alifahamika kwa jina la Daudi Masoke. Walikuwa balaa alikuwa anaiba Nyumba nzima hadi kitanda ulicholalia.

18. Ukisia mtaani Dunda, Kwendi, Shaban wanatembea mtaani wanaume wote kimya walikuwa hawaoni shida kukupiga dispiss ya tumbo. Wakitaka kupora walikuwa hawapati shida wanakuzunguka baada ya muda unaporwa ukipiga kelele hakuna Wa kukusaidia maana hadi wazazi wao walikuwa wanawaogopa.

19. Ukisikia obamka yaani ilikuwa full kwa watoto Wa mafiati, sinde, ilemi, isanga, ilolo ni sehemu ya kuchomea viazi mtoto walikuwa radhi asile nyumbani aende njelii kuokota viazi ili akachome obamka.

20. Uswahili tabu fresh food iligeuzwa jina na kuitwa Chakula barafu kiss vyakula vinahifadhiwa kwenye friiza. Expire date ya chakula hasa maziwa ilikuwa furaha kwa watoto Wa uswahili. Zaidi panaitwa city pub/century plaza.

21. Doxi waliwauzia wanyia blauzi na kuwaambia mashati. Ndio kisasi kikarudishwa unyiani na kuwaambia wamachinga Wa nguo Tumugoge tumuleshe...(tumuue tumuache).

NAIKUMBUKA MBEYA YA ZAMANI..
Bujibuji ukifika Mbeya tuwasiliane, nina miaka saba sasa na nimekukubali sana, ninajua bahadhi ya vitu ila ulivyoongea ni kumbukumbuku tosha kwa bahadi yetu sisi wakuja hapa. Ila wababe na wachakarikaji bado wapo na Jiji linasonga mbele. Fursa bado zipo nyingi kwa upande wa kilimo
 
Kulikuwa na watoto fulani wa Ilolo walikuwa mapacha wanasoma Mbeya Day miaka 1996 to 1999 hakika walikuwa wakali
 
Pale Sangu Sekondari ...kwenye miti kulikuwa na kichaka kinaitwa kaburi la Bob Marley watu wamekula sana ganja pale....lkn leo hii baadhi yao ni watu wakubwa sana hapa chini ya jua......
nimefursiku hizi utakwenda
Disco mount Livingston tulikua tunaita "shimoni" umaarufu ulipungua baada ya kufungua Royal pamodz
HII NDIO ILIKUWA MBEYA BWANA

1. Enzi hizo alikuwepo mtu anaitwa Jombi, kudhihirisha ubabe kwa wenzako lazima uwaambie Mimi ni "Jombi"

2. Kulikuwa na basi zinaitwa Kiswele..engine nyuma, Dar - Mby faster, Mafegi hii ilikuwa na vijihoni vya Ukweli,usisahau Mv Saratoga, Tunyande bus service, Zainabus

3. Kulikuwa na wavuta petroli, hawa jamaa walikuwa km 5 hivi, wachafu wanatembea pamoja mitaa ya BP uhindini wakiwa na makopo na vitambaa vilivyoloa petrol wanavuta.

4. kiwanja ngoma, hapa Soka lilipigwa bwana, timu yangu ya Mtaa Snow White chini ya Key, kina Baba Jeni. Basket ball ilikuwa pale Centre, tulikuwa na chama letu Mbeya Flames.

5. Town pale palikuwa na vichaa hatari kuna "Tiotio" huyu alikuwa anachapa ngeli balaa, Merry Kichaa alikuwa na alergy na watu weupe, akikuotea atakukimbizaa na stick utakula. Pale Mbeya Recto ndio ilikuwa km Makao makuu ya vichaa walikuwa kibao

5.Pale Bomani palikuwa na Mzee mmoja mfupi nakumbuka jina moja la Mwakifuna,nilifanya jitihada ili kumuona tu maana kutokumjua na kumuona ilikuwa ni weakness kubwa.

6. Kipindi hicho Disco lilikuwa Mount Livingstone na Rift valley, Soggy doggy enzi hizo akiitwa Wasape na Sugu- 2 Proud, hipop ilinoga bwana.

7. Mtakumbuka Mbeya tulikuwa na ukumbi Wa Sinema pale opposite na Ofisi za Posta Town, Muvy ya Hatya ilifunika sana enzi zile.

8. Miaka ile bwana mvua ilikuwa inapiga km gharika,sometimes ilikuwa inamwagwa barafu km ulaya,mlima Loleza ulikuwa ukifunikwa theluji kwa siku kadhaa. Radi sasa, hatariii mpaka nyumba ina Shake.

9. Siku ya Jumamosi ilikuwa ya kuosha mbwa,mbwa wote walikuwa wanapelekwa josho pale Mifugo,nyuma ya Kanisa la Roman,mkishamaliza kuogesha mnaanza kugombanisha Mbwa,mbwa Wa kizungu walikuwa wanaogopwa kupambanishwa na Wa kienyeji ikiaminika wananguvu balaa.

10. Uzunguni enzi hizo kulikuwa na matunda ya aina mbalimbali,watoto walikuwa wanatoka maeneo kadhaa ikiwemo Isanga kuja kuchuma maparachichi,mang'ang'a,mafyulizi,mapohora,mapera nk.

11. Mwanjelwa.enzi hizo iliitwa Doksi au Njelii, mitumba viwango,raba Kali,msela ukitupia vya doksi umemaliza.

12.Enzi zile ukisoma Sisimba na Azimio unafunika,Shule ya International ilikuwa Umoja primary school, waliosoma hapo hata kupishana nao unaogopa

13. Kuruka ukuta Wa Uwanja Wa Sokoine au kuingia uwanjani kupitia Bomba la maji ya mvua wakati Wa mechi ilikuwa ujanja balaa.

14. Ukisikia Shule za Sekondari Iyunga, Sangu, Loleza, Mbeya Day zilikuwa na kila aina ya sifa.Sangu kulikuwa na vichwa lazima uvitambue wababe km Simply na Kambosonic waliogopwa.

15. UMISETA sasa, dah, achaa..hapa Lutengano hapa Mwakaleli, boli lilitandazwa,kikinuka uwanjani ilikuwa km vita,makwanja na fimbo hujui vilipotokea,ukizubaa utakula mkono balaa

16. Kuna mdada walikuwa hatari alikuwa anatembeza kichapo kwa wanaume balaa walikuwa anatokea ilemi alifahamika kwa jina la Jeni.

17 Kuna jamaa alikuwa mtata sana mtaa Wa mafiati, makunguru, juakali alifahamika kwa jina la Daudi Masoke. Walikuwa balaa alikuwa anaiba Nyumba nzima hadi kitanda ulicholalia.

18. Ukisia mtaani Dunda, Kwendi, Shaban wanatembea mtaani wanaume wote kimya walikuwa hawaoni shida kukupiga dispiss ya tumbo. Wakitaka kupora walikuwa hawapati shida wanakuzunguka baada ya muda unaporwa ukipiga kelele hakuna Wa kukusaidia maana hadi wazazi wao walikuwa wanawaogopa.

19. Ukisikia obamka yaani ilikuwa full kwa watoto Wa mafiati, sinde, ilemi, isanga, ilolo ni sehemu ya kuchomea viazi mtoto walikuwa radhi asile nyumbani aende njelii kuokota viazi ili akachome obamka.

20. Uswahili tabu fresh food iligeuzwa jina na kuitwa Chakula barafu kiss vyakula vinahifadhiwa kwenye friiza. Expire date ya chakula hasa maziwa ilikuwa furaha kwa watoto Wa uswahili. Zaidi panaitwa city pub/century plaza.

21. Doxi waliwauzia wanyia blauzi na kuwaambia mashati. Ndio kisasi kikarudishwa unyiani na kuwaambia wamachinga Wa nguo Tumugoge tumuleshe...(tumuue tumuache).

NAIKUMBUKA MBEYA YA ZAMANI..
Nimeipenda avatar yako na imenikumbusha hiyo picha ya mhusika mkuu wa picha moja ya kinaijera ikiitwa AGUMBA. Karibu sana Mbeya mkuu
 
Back
Top Bottom