Mbeya long time kitambo

HII NDIO ILIKUWA MBEYA BWANA

1. Enzi hizo alikuwepo mtu anaitwa Jombi, kudhihirisha ubabe kwa wenzako lazima uwaambie Mimi ni "Jombi"

2. Kulikuwa na basi zinaitwa Kiswele..engine nyuma, Dar - Mby faster, Mafegi hii ilikuwa na vijihoni vya Ukweli,usisahau Mv Saratoga, Tunyande bus service, Zainabus

3. Kulikuwa na wavuta petroli, hawa jamaa walikuwa km 5 hivi, wachafu wanatembea pamoja mitaa ya BP uhindini wakiwa na makopo na vitambaa vilivyoloa petrol wanavuta.

4. kiwanja ngoma, hapa Soka lilipigwa bwana, timu yangu ya Mtaa Snow White chini ya Key, kina Baba Jeni. Basket ball ilikuwa pale Centre, tulikuwa na chama letu Mbeya Flames.

5. Town pale palikuwa na vichaa hatari kuna "Tiotio" huyu alikuwa anachapa ngeli balaa, Merry Kichaa alikuwa na alergy na watu weupe, akikuotea atakukimbizaa na stick utakula. Pale Mbeya Recto ndio ilikuwa km Makao makuu ya vichaa walikuwa kibao

5.Pale Bomani palikuwa na Mzee mmoja mfupi nakumbuka jina moja la Mwakifuna,nilifanya jitihada ili kumuona tu maana kutokumjua na kumuona ilikuwa ni weakness kubwa.

6. Kipindi hicho Disco lilikuwa Mount Livingstone na Rift valley, Soggy doggy enzi hizo akiitwa Wasape na Sugu- 2 Proud, hipop ilinoga bwana.

7. Mtakumbuka Mbeya tulikuwa na ukumbi Wa Sinema pale opposite na Ofisi za Posta Town, Muvy ya Hatya ilifunika sana enzi zile.

8. Miaka ile bwana mvua ilikuwa inapiga km gharika,sometimes ilikuwa inamwagwa barafu km ulaya,mlima Loleza ulikuwa ukifunikwa theluji kwa siku kadhaa. Radi sasa, hatariii mpaka nyumba ina Shake.

9. Siku ya Jumamosi ilikuwa ya kuosha mbwa,mbwa wote walikuwa wanapelekwa josho pale Mifugo,nyuma ya Kanisa la Roman,mkishamaliza kuogesha mnaanza kugombanisha Mbwa,mbwa Wa kizungu walikuwa wanaogopwa kupambanishwa na Wa kienyeji ikiaminika wananguvu balaa.

10. Uzunguni enzi hizo kulikuwa na matunda ya aina mbalimbali,watoto walikuwa wanatoka maeneo kadhaa ikiwemo Isanga kuja kuchuma maparachichi,mang'ang'a,mafyulizi,mapohora,mapera nk.

11. Mwanjelwa.enzi hizo iliitwa Doksi au Njelii, mitumba viwango,raba Kali,msela ukitupia vya doksi umemaliza.

12.Enzi zile ukisoma Sisimba na Azimio unafunika,Shule ya International ilikuwa Umoja primary school, waliosoma hapo hata kupishana nao unaogopa

13. Kuruka ukuta Wa Uwanja Wa Sokoine au kuingia uwanjani kupitia Bomba la maji ya mvua wakati Wa mechi ilikuwa ujanja balaa.

14. Ukisikia Shule za Sekondari Iyunga, Sangu, Loleza, Mbeya Day zilikuwa na kila aina ya sifa.Sangu kulikuwa na vichwa lazima uvitambue wababe km Simply na Kambosonic waliogopwa.

15. UMISETA sasa, dah, achaa..hapa Lutengano hapa Mwakaleli, boli lilitandazwa,kikinuka uwanjani ilikuwa km vita,makwanja na fimbo hujui vilipotokea,ukizubaa utakula mkono balaa

16. Kuna mdada walikuwa hatari alikuwa anatembeza kichapo kwa wanaume balaa walikuwa anatokea ilemi alifahamika kwa jina la Jeni.

17 Kuna jamaa alikuwa mtata sana mtaa Wa mafiati, makunguru, juakali alifahamika kwa jina la Daudi Masoke. Walikuwa balaa alikuwa anaiba Nyumba nzima hadi kitanda ulicholalia.

18. Ukisia mtaani Dunda, Kwendi, Shaban wanatembea mtaani wanaume wote kimya walikuwa hawaoni shida kukupiga dispiss ya tumbo. Wakitaka kupora walikuwa hawapati shida wanakuzunguka baada ya muda unaporwa ukipiga kelele hakuna Wa kukusaidia maana hadi wazazi wao walikuwa wanawaogopa.

19. Ukisikia obamka yaani ilikuwa full kwa watoto Wa mafiati, sinde, ilemi, isanga, ilolo ni sehemu ya kuchomea viazi mtoto walikuwa radhi asile nyumbani aende njelii kuokota viazi ili akachome obamka.

20. Uswahili tabu fresh food iligeuzwa jina na kuitwa Chakula barafu kiss vyakula vinahifadhiwa kwenye friiza. Expire date ya chakula hasa maziwa ilikuwa furaha kwa watoto Wa uswahili. Zaidi panaitwa city pub/century plaza.

21. Doxi waliwauzia wanyia blauzi na kuwaambia mashati. Ndio kisasi kikarudishwa unyiani na kuwaambia wamachinga Wa nguo Tumugoge tumuleshe...(tumuue tumuache).

NAIKUMBUKA MBEYA YA ZAMANI..


NAMBA 13. Ndiyo inathibitisha Mbeya unayozungumzia sio ya ZAMANI!! ,Zamani SOKOINE STADIUM uliitwa MAPINDUZI STADIUM na bado zamani MAPINDUZI haukuwepo pale kulikuwa na miti, pembeni kulikuwa na uwanja mdogo mzuri sisi watoto wa wakati huo tukicheza chandimu. Vichaa alikuwepo PRISON aka UGUMBA HUYO BALAA ! Alikuwepo ALOYCE kazi yake kuimba hana ugomvi na mtu, alikuwepo KANJINGALA anatembea akigonga chuma huku akicheza na kunengua kiuno !!! wengine kina Mwakityaka, Marry nk. lakini Bujibuji usijali inawezekana zamani hiyo unayoizungumzia inalingana na kipindi ulicho kuwepo !! AMANI IWE NASI !
 
NAMBA 13. Ndiyo inathibitisha Mbeya unayozungumzia sio ya ZAMANI!! ,Zamani SOKOINE STADIUM uliitwa MAPINDUZI STADIUM na bado zamani MAPINDUZI haukuwepo pale kulikuwa na miti, pembeni kulikuwa na uwanja mdogo mzuri sisi watoto wa wakati huo tukicheza chandimu. Vichaa alikuwepo PRISON aka UGUMBA HUYO BALAA ! Alikuwepo ALOYCE kazi yake kuimba hana ugomvi na mtu, alikuwepo KANJINGALA anatembea akigonga chuma huku akicheza na kunengua kiuno !!! wengine kina Mwakityaka, Marry nk. lakini Bujibuji usijali inawezekana zamani hiyo unayoizungumzia inalingana na kipindi ulicho kuwepo !! AMANI IWE NASI !
Prison alikuwa Na miguu mmoja mfupi kidogo, ana shabaha sana ya mawe.
Uwanja wa mapinduzi ulijengwa na Kila mtu hata wafungwa walishiriki ujenzi.
Kabla hapajawa na uwanja, palikuwa na uwanja wa golf wa Mbeya Club.
Tatizo ni kwamba history was not written, tuendelelee kuandika historia kwa ajili ya kizazi kijacho
 
Mwasimba was nonde ndo alikuwa founder was kuuza bangi na alikuwa mtemi balsa had I mapolisi walikuwa wanachezea vichapo kama kawa!
 
Prison alikuwa Na miguu mmoja mfupi kidogo, ana shabaha sana ya mawe.
Uwanja wa mapinduzi ulijengwa na Kila mtu hata wafungwa walishiriki ujenzi.
Kabla hapajawa na uwanja, palikuwa na uwanja wa golf wa Mbeya Club.
Tatizo ni kwamba history was not written, tuendelelee kuandika historia kwa ajili ya kizazi kijacho
Sahihi Bujibuji tuendelee kukumbushana naamini mungu akijalia tilukijaona onana WOTE tutasema aaah kumbe wewe!!!
 
Kullikuwa na Mama Mmoja Kichaa pale Sokoni wahuni walikuwa wanamdandia Usiku akitoka matembezini...Kuna siku moja Usiku wa kama saa nne hivi nilimkuta Njemba moja limemkunja huyu Mama wa watu pale karibu na Uwanja wa Sokoine nyuma kidogo ya Shule ya sisimba!!!Mama wa watu alukuwa katulia tu...
 
Kullikuwa na Mama Mmoja Kichaa pale Sokoni wahuni walikuwa wanamdandia Usiku akitoka matembezini...Kuna siku moja Usiku wa kama saa nne hivi nilimkuta Njemba moja limemkunja huyu Mama wa watu pale karibu na Uwanja wa Sokoine nyuma kidogo ya Shule ya sisimba!!!Mama wa watu alukuwa katulia tu...
Aiiiiii mamaaaaa nakufaaaaaa, Piere Liquid atapaki kuwa juu
 
Mbeya city mimi nakumbuka ligi ya magari ya kwenda Tunduma kipindi hicho ni hiace ndio zilizotawala. Hiace zilizotamba sana kwa mbio zilikuwa ni Bambucha,Umeme, High Bury, Loita, Mkulu na Mwambambe.

Kuna hiace ilikuwa inaitwa Bambucha kutoka Soko Matola hii ilikuwa inaendeshwa na kaka mkubwa Andrea.

Huyu alikuwa mbabe alipokuwa akifika stend kuuu wahuni wote walikuwa wanakimbia huyu alikuwa mbabe haswa vijana wa Soko matola mpaka Stendi walikuwa wakimuogopa.
 
Kweli umekaa mby .....watoto wa malakasuka na bebby shangazi walisumbua sana .....pia kulikuwa na mtemi mmoja anatokea Isanga akiitwa brigadia mwakayugu .....by the way uwanja ngoma nimecheza soka nikichezea timu ya forest .....mambo yalikuwa mswano kipindi hicho
Daa!! Nonde bwana- machinjioni. Ajira ya vijana wengi. Nyama choma kwa matoki kwa wingiii!! Daaa!!! Mimi kwangu miaka ya 1973 na kuendelea. Nimesoma Mbeya day. Kimpumu original, ubwala bwa misi, Majengo bwana na Ghana!! Acha tu.
 
Nimekaa mbeya 1995 mpaka 1997 Nilikuwa nakaa sokomataloa kalibu na kiwanja mpaka au Olofea,Nilikuwa na Duka langu pale lilikuwa linagonga Reggae sana walikuwa wanapaita kwa Marasta. Ndipo nilipojuana na Ngwisa alikuwa Jamaa Yangu sana.Hata lile sakata la polisi kupiga mabomu Nyumbani kwao nilikuwepo.na kulikuwa na Jamaa mmoja anaitwa BEST au Ipiyana alikuwa anajua sana miziki ya reggea sijui mzima,baadaye nikawa na Duka jingine Rejco kalibu na nonde hapo ndipo nilipojuana na Mwasimba naye alikuwa anakuja kusikiliza reggae,nimeangalia sana Video magorofani
 
HII NDIO ILIKUWA MBEYA BWANA

1. Enzi hizo alikuwepo mtu anaitwa Jombi, kudhihirisha ubabe kwa wenzako lazima uwaambie Mimi ni "Jombi"

2. Kulikuwa na basi zinaitwa Kiswele..engine nyuma, Dar - Mby faster, Mafegi hii ilikuwa na vijihoni vya Ukweli,usisahau Mv Saratoga, Tunyande bus service, Zainabus

3. Kulikuwa na wavuta petroli, hawa jamaa walikuwa km 5 hivi, wachafu wanatembea pamoja mitaa ya BP uhindini wakiwa na makopo na vitambaa vilivyoloa petrol wanavuta.

4. kiwanja ngoma, hapa Soka lilipigwa bwana, timu yangu ya Mtaa Snow White chini ya Key, kina Baba Jeni. Basket ball ilikuwa pale Centre, tulikuwa na chama letu Mbeya Flames.

5. Town pale palikuwa na vichaa hatari kuna "Tiotio" huyu alikuwa anachapa ngeli balaa, Merry Kichaa alikuwa na alergy na watu weupe, akikuotea atakukimbizaa na stick utakula. Pale Mbeya Recto ndio ilikuwa km Makao makuu ya vichaa walikuwa kibao

5.Pale Bomani palikuwa na Mzee mmoja mfupi nakumbuka jina moja la Mwakifuna,nilifanya jitihada ili kumuona tu maana kutokumjua na kumuona ilikuwa ni weakness kubwa.

6. Kipindi hicho Disco lilikuwa Mount Livingstone na Rift valley, Soggy doggy enzi hizo akiitwa Wasape na Sugu- 2 Proud, hipop ilinoga bwana.

7. Mtakumbuka Mbeya tulikuwa na ukumbi Wa Sinema pale opposite na Ofisi za Posta Town, Muvy ya Hatya ilifunika sana enzi zile.

8. Miaka ile bwana mvua ilikuwa inapiga km gharika,sometimes ilikuwa inamwagwa barafu km ulaya,mlima Loleza ulikuwa ukifunikwa theluji kwa siku kadhaa. Radi sasa, hatariii mpaka nyumba ina Shake.

9. Siku ya Jumamosi ilikuwa ya kuosha mbwa,mbwa wote walikuwa wanapelekwa josho pale Mifugo,nyuma ya Kanisa la Roman,mkishamaliza kuogesha mnaanza kugombanisha Mbwa,mbwa Wa kizungu walikuwa wanaogopwa kupambanishwa na Wa kienyeji ikiaminika wananguvu balaa.

10. Uzunguni enzi hizo kulikuwa na matunda ya aina mbalimbali,watoto walikuwa wanatoka maeneo kadhaa ikiwemo Isanga kuja kuchuma maparachichi,mang'ang'a,mafyulizi,mapohora,mapera nk.

11. Mwanjelwa.enzi hizo iliitwa Doksi au Njelii, mitumba viwango,raba Kali,msela ukitupia vya doksi umemaliza.

12.Enzi zile ukisoma Sisimba na Azimio unafunika,Shule ya International ilikuwa Umoja primary school, waliosoma hapo hata kupishana nao unaogopa

13. Kuruka ukuta Wa Uwanja Wa Sokoine au kuingia uwanjani kupitia Bomba la maji ya mvua wakati Wa mechi ilikuwa ujanja balaa.

14. Ukisikia Shule za Sekondari Iyunga, Sangu, Loleza, Mbeya Day zilikuwa na kila aina ya sifa.Sangu kulikuwa na vichwa lazima uvitambue wababe km Simply na Kambosonic waliogopwa.

15. UMISETA sasa, dah, achaa..hapa Lutengano hapa Mwakaleli, boli lilitandazwa,kikinuka uwanjani ilikuwa km vita,makwanja na fimbo hujui vilipotokea,ukizubaa utakula mkono balaa

16. Kuna mdada walikuwa hatari alikuwa anatembeza kichapo kwa wanaume balaa walikuwa anatokea ilemi alifahamika kwa jina la Jeni.

17 Kuna jamaa alikuwa mtata sana mtaa Wa mafiati, makunguru, juakali alifahamika kwa jina la Daudi Masoke. Walikuwa balaa alikuwa anaiba Nyumba nzima hadi kitanda ulicholalia.

18. Ukisia mtaani Dunda, Kwendi, Shaban wanatembea mtaani wanaume wote kimya walikuwa hawaoni shida kukupiga dispiss ya tumbo. Wakitaka kupora walikuwa hawapati shida wanakuzunguka baada ya muda unaporwa ukipiga kelele hakuna Wa kukusaidia maana hadi wazazi wao walikuwa wanawaogopa.

19. Ukisikia obamka yaani ilikuwa full kwa watoto Wa mafiati, sinde, ilemi, isanga, ilolo ni sehemu ya kuchomea viazi mtoto walikuwa radhi asile nyumbani aende njelii kuokota viazi ili akachome obamka.

20. Uswahili tabu fresh food iligeuzwa jina na kuitwa Chakula barafu kiss vyakula vinahifadhiwa kwenye friiza. Expire date ya chakula hasa maziwa ilikuwa furaha kwa watoto Wa uswahili. Zaidi panaitwa city pub/century plaza.

21. Doxi waliwauzia wanyia blauzi na kuwaambia mashati. Ndio kisasi kikarudishwa unyiani na kuwaambia wamachinga Wa nguo Tumugoge tumuleshe...(tumuue tumuache).

NAIKUMBUKA MBEYA YA ZAMANI..
Umesahau Mabati kiwanda cha miwa na vitindi , Kilabu cha Mwakyela pale Nonde , Kilabu cha Maendeleo kule Ghana juu , Kwa Mwalalika mashine maarufu ya kukoboa mpunga , Mtemi Mwasimba bangi zikipanda anaenda milima ya Nonde kupandisha Bendera yake alafu ikifika saa sita usiku anaenda kuishusha , Mbeya kuna makaburi maarufu ya Sabasaba na Nonde , Pombe maarufu ni Chimpumu ukinywa leo yakibaki machicha kesha unachemsha maji alafu unamimina mziki unaendelea kwa kutumia mlija unaitwa mkenge , Kilabu Maarufu kutoka kwa mkoloni kilitwa REGCO pembeni kulikua na soko Maarufu liliitwa Soko la Majengo , ukicha shule ya Sisimba na Azimia huku Majengo kulikuwa na shule ya Majengo na ghana kuna shule ya Mbata , matunda ya mbeya masasati , mbulu , numbu , katapela , mang'ang'a, fyulisi , ..... vitongoji maarufu ni Nonde , ghana , majengo , Uhindini , Kwa Mama John, Mwanjelwa a.k.a Njelii , vilio msibani si mchezo .....
 
Back
Top Bottom