Mbeya: Jiji au Kijiji kikubwa?

Mbeya: Jiji au Kijiji kikubwa?

Mbeya ni mkoa unaolisha nchi nzima kwa hiyo ni mkoa wa kilimo haswaa...hivo ni sahihi kabisa kuita "Kijiji Kikubwa"
Km ukikumbuka pia unaweza kuita Kijiji Kikubwa cha kijani"
 
Tumia akili kidogo umepewa bure na Mungu.

Umefika Mbeya sehemu gani? Umetembelea maeneo gani? Yataje japo machache tu. Unaweza kufikia Uyole na ukaishia huko na ikawa ndiyo picha yako kamili ya Mbeya. Ni sawa na kufikia Buguruni kwa Mnyamani useme umefika Dar umekuta hali si nzuri. Au umefika kwa Mrombo Arusha na ikawa ndiyo picha ya Arusha nzima kwako.

Nimesema tumia akili kidogo. Umepewa bure hujanunua. Ili eneo litangazwe kuwa jiji lazima likidhi vigezo fulani. Mbeya ilikidhi siku nyingi mno. Unavijua vigezo hivyo? Sema kipi kimepwaya kwa Mbeya. Usidhani mtu anaamka usiku na kusema eneo fulani ni jiji. Sio kwa majiji tu, hata miji midogo ina vigezo vyake kadhaa.

Hujiulizi kwa nini miji mingine mingi tu sio majiji? Vigezo na masharti kuzingatiwa.
Mbeya mlipendelewa sana kuitwa jiji. Yaani hivyo virestaurant sasa. Unachoka mwenyewe. Mbeya hamna hata sehemu ya kuangalia movie. Jiji halina supermarket!!!!!
 
Watu wa Mbeya jifunzeni kuambiwa ukweli. Huu mji bado sana jamani. Lengo la kuwaambia hivi ni kutaka mbadilike. Hivi zaidi ya baridi, kuna nini kingine? Haya naomba mnielekeze nitapata wapi biriani leo kwa mfano? Nataka kula biriani Leo hapa Mbeya
 
wana Mbeya mimi nawashauri muichuke hii criticism ya huyu member kama springboard ya kuwa prove watu wrong in the long run.

nawajua Wanyaki kibao wapo Dar wana mijengo ya kufa mtu na wanakula bata kama lote, lakini ukienda kwao Mbeya nyumba zao ni za matofali mabichi - afu katikati ya mji!

pale mlimani (UDSM) enzi zile mlikuwa na umoja wenu mkiuita "UWAMBE" - uliwasaidia nini? mimi nilidhani madhumuni ya kuwa na umoja wa jinsi ile ni pamoja na kushirikiana katika kupanga mikakati ya namna bora ya kuuendeleza mkoa wenu. au ulikuwa ni umoja wa kukutana tu na kunywa bia pamoja?

niwajuavyo shemeji zangu wana Mbeya, hali ya sasa ya lile jiji lenu haifanani na hadhi mliyo nayo. mimi nawashauri tu kuwa badala ya kuipinga hii mada ya mdau, ifanyieni kazi. kumbukeni ile hadithi ya yule kijana mdogo ambaye kwenye familia yake alionekana hana akili darasani kuliko dada/kaka zake lakini kutokana na kukerwa na madharau ya nduguze akazama mzigoni akapiga kitabu cha kufa mtu, hatimae akawa professor na kuwa tegemeo la ndugu zake wale wale walokuwa wakimdharau.

a word to the wise - this!
 
Watu wa Mbeya jifunzeni kuambiwa ukweli. Huu mji bado sana jamani. Lengo la kuwaambia hivi ni kutaka mbadilike. Hivi zaidi ya baridi, kuna nini kingine? Haya naomba mnielekeze nitapata wapi biriani leo kwa mfano? Nataka kula biriani Leo hapa Mbeya
Labda biriani ya mindizi ya kuchoma na moshi mkaa
 
Nimefika Mbeya nimechoka mwenyewe. Nyumba nyingi siyo nzuri. Chakula kwenye migahawa usiseme. Yaani hamna kitu kwa kweli. Kazi ya ziada inahitajika. Bado saaana
Upo sahihi, sijavutiwa na Ujiji wa Mbeya, hakuna uzuri na mvuto kama litakiwavyo kuitwa jiji, yaani Mbeya ukilinganisha na Moro, Moro Kuzuri
 
Nacho kiona hapa ni utamaduni ndio Shida. Sisi tulio kulia mbeya tukienda sehemu zingine tunapata pia Shida ya vya kula. Mafano wengine wanaweka viungo vingi sana wakati kwangu mm hilo ni shida sana.
Nyumba nzuri Mbeya ziko pembezoni
 
Nimekumbuka tu wimbo uitwao Mambo ya Fedha wa Mhe Sugu Mbuge wa Mbeya Mjini kamstari kamoja "Ukiwa na Kitu Bongo ni kama NewYork" ",Mbona Unashangaa Mambo ya Fedha", Mambo ya Fedha"( wakati mwingine najichek mfukoni na sh ngap afu naamua kukausha tu , ksha naendelea panga nyanya zangu hapa kijijin Doma, Tchao,Muuza Nyanya
 
Back
Top Bottom