Mbeya imepotea na Mark Mwandosya?

Mbeya imepotea na Mark Mwandosya?

Sasa solution ni kuikataa CCM? Mbona aliyefanya hayo yuko huko huko upinzani?
Sio suruhu, lakini kwa namna moja au nyingine inawapa sababu wananchi kuuona mlango wa upinzani. Maana ccm hakuna hata upenyo wa kutokea.
 
Akina Mwakyembe wako wapi sasa?
Wangesaidia kazi za Mzee Mwandosya

Ni Kama nao hawapo huko, wakati furani walivuma sanaa
Mkuu samahani naomba nirekebishe neno uliloliandika "furani" usahihi wake ni "fulani" ila niwie radhi sina nia mbaya nimeona tuu, nahisi pengine ni mambo ya simu tuu au ulikuwa na haraka katika kuandika.
 
Kwan alikuwa profesa wa engineering MIT au hapa udsm katika nchi ambayo bajeti yake ya utafiti ni 1/5 ya bajeti ya Kenya ya utafiti? Kuwa mwanataaluma sio Ishu ktk nchi hii, ukitaka kufanya mabadiliko ya kweli inabidi uingie kwenye siasa ili wababaishaji wote wasipate fursa ya kutuongoza. Baada ya Mwalimu Nyerere, ungetegemea tupate vichwa kweli kutuongoza, lakini wapi.
Mwalimu ndio wa kwanza kuivuruga nchi.
 
muache mkuu,rais hata asipotupia jicho mkoa wetu tutaujenga sisi wenyew pamoja ni viongozi wetu na wasomi ambao wapo huku,kinachotakiwa ni sisi wenyew kuamua wala si mpaka serikali au rais aje kutufanyia au sijui NHC waje wajenge nyumba zao no.mkoa tu wenyew una potential kubwa pia kuliendesha na kuingizia mapato taifa so bado mkoa wa mbeya una nafasi kubwa kujiendeleza wenyew.
kama mlishindwa miaka yote mtawezaleo?
 
Mkuu yule ni jembe letu wana Mbeya, tumpe moyo ili asaidie kupigania maendeleo ya Mbeya yote.
Katika muda wote huu, mimi sijaona mtu waa kuvaa viatu vyake.
hana lolote tatizo ukipenda chongo utaita kengeza
 
Hii haitasaidia, kwa sababu sehemu mnayoichagua bado siyo sehemu sahihi!

Wale mnaowalaumu kwa kukwamisha miradi ya Mbeya ndiyo vinara wa upinzani sasa hivi!

Siku upinzani ukiingia ikulu kama mnavyodhani, usitegemee hao viongozi watabadilika maana hiyo ndiyo hulka yao ya kila siku!

Kinachotakiwa kwenu kama wenyeji wa Mbeya ni kuwa na mikakati ya kisiasa na mna kila sababu ya kufanikiwa kwa sababu mna kila kitu cha kuwafanya mfanikiwe!

Siasa ni mikakati, na mikakati inaanzia kwa viongozi wenu wa majimbo watakaoiwakilisha Mbeya kitaifa.

Mtumieni Mwandosya kama mlezi wa kisiasa, ili sehemu alipoishia aweze kuendeleza mwingine lakini siyo kuanza upya.
Nakubaliana na wewe mkuu.
Mawaxiri Wakuu walioitesa Mbeya sasa hivi wako CHADEMA.

Hakuna cha kuwategemea hao, vijana wa CHADEMA Mbeya walione hilo.
 
kama mlishindwa miaka yote mtawezaleo?
yeah leo,tunaweza mkuu kutokana na kuwa mabadiliko,na zama au aina ya watu walokuwepo....so nafasi na muda bado vipo,kwa kizazi chetu tupo vizur..kinachokwamisha inawezekana kuwa ni mambo ya siasa na uhasama baina ya watu na watu,ila nguvu kazi ipo ya kutosha mkoani humo.
 
1011273_10204474974252892_1059767986913548766_n.jpg

Mkuu matatizo ya Mark Mwandosya na Mkoa wa Mbeya yalianza na Mtandao wa Kikwete.
Kosa ilikuwa kuwa wa tatu katika kinyang'nyiro cha urais mwaka 2005.

Jamaa alipgwa vita na Lowasa , alipigwa vita na Mkuu wa Mkoa Mwakipesile, alipigwa vita na hata CCM yenyewe mpaka ikawa mbaya.
Watu wa Mbeya nawafahamu, vijana kuingia kushabikia CHADEMA ilikuwa a direct reaction kwa nguli wao kupigwa vita vya wazi wazi.
Nakumbuka Waziri Mkuu Lowasa wakati huo alipotembelea Mbeya, Mwandosya aliimbiwa "Raisi...raisi....raisi..." na vijana wa Mbeya mjini.
Kitendo hicho kilimuudhi sana Lowasa, lakini hiyo ilielezea jinsi Mwandosya alivokubalika sana mkoani Mbeya, tena na makabila yote mkoani.

The powers that be wakati huo waliamua kumdhibiti Mwandosya kisiasa.
Kugombea NEC mwaka 2007 walimwekea kijana mdogo anaitwa Thomas Mwang'onda, mtoto wa kigogo wa sekta ya intellijensia, Abson Mwang'onda.

Fedha nyingi sana zilitumika kumnadi Thomas, kiasi kufikia bilioni moja.
Lakini kijana Thomas aliangukia pua!
Mwandosya aliwahi kulalamika katika kitabu kimoja jinsi alivyokuwa akipigwa rafu, na serikali yake, na chama chake CCM!
Hatuwezi kuunganisha , lakini mara Mwandosya aliyekuwa akionekana fit na anafanya mazoezi kila alipopata wasaa mitaani, akaanza kuugua.
Wengine wanadai aliwekewa sumu kama ile ya Dr Harrison Mwakyembe, lakini hilo halijathibitishwa.

Kugombe tena mwaka 2015 ilikuwa just going through the motions, Mwandosya alisha umizwa vibaya.
Mwishoni alipoishiwa nguvu masikini Mwandosya akaamua kurudi kupumzika kijijini kwake Lufilyo, Zaidi ya kilometa 100 toka hata mjini tukuyu.

Kwa maoni yangu serikali ya CCM ndiyo iliyo utoa mkoa wa Mbeya kwenda CHADEMA, kwa kumdhibiti kipenzi cha wana Mbeya, Prof Mark mwandosya.
Mategemeo ni ingalau Mheshimiwa John Pombe Magufuli atupie jicho mkoa huu wenye potential kubwa sana,
Hiyo picha inanichanganya sana. Naona kama kuna Nyerere wawili. Kuna huyo mzee nyuma ya Nyerere na kaunda suti yake nyeupe amesimama kama askari mguu sawa tafikiri naye ni Nyerere ila anaonekana kuwa mwoga sana maana anaonekana kunyenyekea kupita kiasi hata kama yuko nyuma ya Nyerere. Picha inaongea
 
1011273_10204474974252892_1059767986913548766_n.jpg

Mkuu matatizo ya Mark Mwandosya na Mkoa wa Mbeya yalianza na Mtandao wa Kikwete.
Kosa ilikuwa kuwa wa tatu katika kinyang'nyiro cha urais mwaka 2005.

Jamaa alipgwa vita na Lowasa , alipigwa vita na Mkuu wa Mkoa Mwakipesile, alipigwa vita na hata CCM yenyewe mpaka ikawa mbaya.
Watu wa Mbeya nawafahamu, vijana kuingia kushabikia CHADEMA ilikuwa a direct reaction kwa nguli wao kupigwa vita vya wazi wazi.
Nakumbuka Waziri Mkuu Lowasa wakati huo alipotembelea Mbeya, Mwandosya aliimbiwa "Raisi...raisi....raisi..." na vijana wa Mbeya mjini.
Kitendo hicho kilimuudhi sana Lowasa, lakini hiyo ilielezea jinsi Mwandosya alivokubalika sana mkoani Mbeya, tena na makabila yote mkoani.

The powers that be wakati huo waliamua kumdhibiti Mwandosya kisiasa.
Kugombea NEC mwaka 2007 walimwekea kijana mdogo anaitwa Thomas Mwang'onda, mtoto wa kigogo wa sekta ya intellijensia, Abson Mwang'onda.

Fedha nyingi sana zilitumika kumnadi Thomas, kiasi kufikia bilioni moja.
Lakini kijana Thomas aliangukia pua!
Mwandosya aliwahi kulalamika katika kitabu kimoja jinsi alivyokuwa akipigwa rafu, na serikali yake, na chama chake CCM!
Hatuwezi kuunganisha , lakini mara Mwandosya aliyekuwa akionekana fit na anafanya mazoezi kila alipopata wasaa mitaani, akaanza kuugua.
Wengine wanadai aliwekewa sumu kama ile ya Dr Harrison Mwakyembe, lakini hilo halijathibitishwa.

Kugombe tena mwaka 2015 ilikuwa just going through the motions, Mwandosya alisha umizwa vibaya.
Mwishoni alipoishiwa nguvu masikini Mwandosya akaamua kurudi kupumzika kijijini kwake Lufilyo, Zaidi ya kilometa 100 toka hata mjini tukuyu.

Kwa maoni yangu serikali ya CCM ndiyo iliyo utoa mkoa wa Mbeya kwenda CHADEMA, kwa kumdhibiti kipenzi cha wana Mbeya, Prof Mark mwandosya.
Mategemeo ni ingalau Mheshimiwa John Pombe Magufuli atupie jicho mkoa huu wenye potential kubwa sana,

Mkuu, kwahiyo unasema kinachomtokea EDO Lowasaaa hivi sasa ni nguvu ya "KARMA" ??.. Kama ni hivyo wacha hiyo dhambi imtafune mpaka aishe kabisa hahahaha
 
Akina Mwakyembe wako wapi sasa?
Wangesaidia kazi za Mzee Mwandosya

Ni Kama nao hawapo huko, wakati furani walivuma sanaa
Huyo Mwakyembe ni mbaya zaidi ya koboko,ana unafiki wa waziwazi sidhani kama anaonekana hata huko mbeya
 
yeah leo,tunaweza mkuu kutokana na kuwa mabadiliko,na zama au aina ya watu walokuwepo....so nafasi na muda bado vipo,kwa kizazi chetu tupo vizur..kinachokwamisha inawezekana kuwa ni mambo ya siasa na uhasama baina ya watu na watu,ila nguvu kazi ipo ya kutosha mkoani humo.
mimi namheshimu prof kwa elimu yake na umri lakini kwa mchango wake kimaendeleo ukweli hakuna alichokifanya ukiondoa uwanja wa ndege naamini na huo ulikuwa mradi wa kitaifa.prof alipendwa na aloheshimiwa na wananchi lakini yeye alodharau uomgozi wote wa wilaya na mkoa.akiwa waziri hakuweza kuhudhuria kikao chochote cha RDC wala cha DDC hata kwenye chama hakuhudhuria kikao chochote cha wilaya hata mkoa sasa hawa watu wanaodai alipigania maendeleo ya mbeya kwa vipi ndipo ninapojiuliza sisi wanambeya tunatakiwa kuwa makini tunapochagua viongozi wetu si mwakyembe wala.mtu ambaye vikao vya kiwilaya na kimkoa waliokuwa wakihudhuria na kuchangia hoja hadi sasa ni mhe mwanjelwa na mlugo
 
Tuko pamoja mkuu.
Mwanzoni nilitegemea ile misa ya kuwashukuru wanambeya iliyofanywa na wakina Mwakyembe na Mwandosya baada ya kutoka Apollo ingekuwa na matokeo chanya kwa mkoa wa Mbeya.

Lakini hali imekuwa ni tofauti na matarajio ya wengi. Kwani waliofanya siasa za kimafia kwa icons wa Mbeya, leo wanapata uungwaji mkono na baadhi ya viongozi kutoka Mbeya!

Hili jambo linastaajabisha sana, hasa kwa viongozi wanaofahamu nafasi zao za kisiasa katika nchi hii!

Jifunzeni kwa mkoa wa Shinyanga na kanda ya ziwa kwa ujumla, mwaka 2010 wabunge wengi wa upinzani walitoka huko na kura nyingi za urais kwa upande wa upinzani zilitoka kanda ya ziwa lakini wabunge wa viti maalum wengi walitoka kwa wenye chama!

Hilo siyo jambo la kushangaza kwani inafahamika ubinafsi ni hulka yao, lakini 2015 Shinyanga, Simiyu na Mwanza hawakufanya ajizi na 2020 hawataambulia hata udiwani!

Watanzania wana chama kimoja cha siasa ambacho ni CCM, hivi vingine ni vyama vya kikabila, kikanda na kidini. Nasema hivi kwa sababu CCM haina mwenyewe, bali ina wapangaji na hawa wapangaji wanaondoka kila baada ya miaka 10 ili kupisha wapangaji wengine.

Kwa hiyo leo kwa mwingine, kesho inaweza kuwa kwako. Kinachohitajika ndani ya CCM ni uvumilivu wa kisiasa basi.!!
Haifai hata kuchangamana nao!
Inafaa kuwapatia elimu na kuwafahamisha kile kinachoendelea kwenye siasa za Tanzania, kwani vijana wengi hawajitambui.
ID yako ime reflect matendo yako na mawazo yako
 
Jk alimchinjia baharini kama bwege vile...

profesa wa engineering kastaafishwa siasa na mtoto wa mjini
 
mimi namheshimu prof kwa elimu yake na umri lakini kwa mchango wake kimaendeleo ukweli hakuna alichokifanya ukiondoa uwanja wa ndege naamini na huo ulikuwa mradi wa kitaifa.prof alipendwa na aloheshimiwa na wananchi lakini yeye alodharau uomgozi wote wa wilaya na mkoa.akiwa waziri hakuweza kuhudhuria kikao chochote cha RDC wala cha DDC hata kwenye chama hakuhudhuria kikao chochote cha wilaya hata mkoa sasa hawa watu wanaodai alipigania maendeleo ya mbeya kwa vipi ndipo ninapojiuliza sisi wanambeya tunatakiwa kuwa makini tunapochagua viongozi wetu si mwakyembe wala.mtu ambaye vikao vya kiwilaya na kimkoa waliokuwa wakihudhuria na kuchangia hoja hadi sasa ni mhe mwanjelwa na mlugo
inawezekana,mkuu ila nadhani amejitaid au meng amewafanyia wananch wake huko jimbon kwake rungw masharik kw mkoa kiujumla huenda hajafanya san.mana vitu ving san mbeya bado!
 
Yaan kila nikiiangalia Kyela nasikia hasira sana! Utafikiri hatuna mbunge!! Ushindi wenyewe wa dhuluma mpaka watu wakapigwa mabomu ya machozu, basi hata ajiongeze halete maendeleo tusahau machungu ila hakuna kinachofanyika
 
Eti wengine wanasema mwa_kye_mbe yuko wapiii ????jimbo lenyewe la kyela limemshinda kweli atalimudu jiji la mbeya labda kwa unafiki
 
Mbeya naijua kuliko MTU yeyote yule, nimezaliwa Kyela - Mbeya nimesoma lyunga, badae lfunda na UDSM.
Acheni siasa Uchwara, tunapoitetea Mbeya ni yetu sisi.

Inauma sana kuna tuko nyuma Kisiasa, kijamii na Kiuchumi.
Sasa zenu hizo chafu hazitusaidii sisi.
CCM na makada wake wameivuruga Mbeya.

Mwakyembe aliaminika sana, Leo hii amelitelekeza jimbo la Kyela, Wilaya mzima inatimka vumbi, achilia mbali barabara inayoenda ltungi Port iliyojengwa na Nyerere.

Acheni siasa UCHWARA tunaumia
Njia panda ipinda hadi matema lamiii yenye kama kutumia mkorogo robo ni lami sehem kubwa ni vumbiii tyyuuuu ,,,toka boda hadiiii ziwani kwa mwamnyange uwiiiiiii ,,,Heshma ya kyela ni roads yenye vipara
 
ni kweli kwenye jimbo lake alipigania barabara ya lami ijengwe kwenda mwakaleli ambayo hadi sasa haijamalizika lakini uhasama aliojenga dhiidi ya rc mwakipesile ulikuwa mkubwa sana kisa kwanini mwakipesile alimpigania thomas awe mnec lakini ikumbukwe mwakipesile na thomas ni ndugu wa damu katika hali ya kawaida lazima angemuunga mkono thomas.kitu nilichjifunza watu hawa wanachuki zisizoisha.lakushangaza mwakipesile mwandosya mwakyembe wanao unasaba
 
Back
Top Bottom