Mwanongwa
Senior Member
- Feb 15, 2023
- 169
- 198
Wananchi wanaotumia Barabara ya Mbeya - Chunya wamelitaka Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani, askari wake kuacha kuchukua rushwa na badala yake wasimamie sheria.
Wananchi hao wamelalamikia kitendo cha mabasi ya Mbeya -Chunya kuzidisha abiria kinyume cha utaratibu.
Mabasi yanayotoka Mbeya Mjini kwenda Wilayani Chunya yamekuwa na utaratibu wa kuzidisha abiria na pindi abiria wanapolalamika wamekuwa wakitolewa kauli chafu na makondakta wa mabasi hayo.
Mabasi aina ya Coastal yana uwezo wa kubeba abiria 29 lakini yamekuwa yakibeba abiria zaidi ya 40.
Askari wa kituo cha ukaguzi cha Isanga Mbeya Mjini na Kawetele Mbeya Vijijini wamekuwa wakichukua rushwa na kuruhusu gari hizo kuendelea na safari.
Kwa mfano siku ya leo tarehe 21 Machi 2023 basi aina ya Coastal (WASAFI) lilizidisha abiria likitokea Mbeya Mjini kwenda Chunya lilipofika kwenye vituo hivyo vya ukaguzi konda alishuka na kwenda kwa askari ambao walikuwa wanasimama ubavuni mwa gari na kuwapatia elfu mbili mbili.
Hali hiyo imekuwa kero kwa wasafiri maana imekuwa ikihatarisha usalama wao na ikumbukwe kuwa barabar hiyo ndiyo yenye kona Kali ambazo kwasasa mkoa umezigeuza kuwa vivutio.
Mabasi hayo hayaanzi safari pale stand ya Airport ya zamani mpaka wahakikishe yamejaa, huku kwenye eneo ambalo wanatakiwa kukaa abiria wa nne wanalazimisha wakae watano.
Tukiachana na mwendo kasi na ubovu wa vyombo vya usafi, chanzo kingine cha ajali ni gari kuzidisha mzigo/abiria tofauti na uwezo wake.
Wananchi hao wamelalamikia kitendo cha mabasi ya Mbeya -Chunya kuzidisha abiria kinyume cha utaratibu.
Mabasi yanayotoka Mbeya Mjini kwenda Wilayani Chunya yamekuwa na utaratibu wa kuzidisha abiria na pindi abiria wanapolalamika wamekuwa wakitolewa kauli chafu na makondakta wa mabasi hayo.
Mabasi aina ya Coastal yana uwezo wa kubeba abiria 29 lakini yamekuwa yakibeba abiria zaidi ya 40.
Askari wa kituo cha ukaguzi cha Isanga Mbeya Mjini na Kawetele Mbeya Vijijini wamekuwa wakichukua rushwa na kuruhusu gari hizo kuendelea na safari.
Kwa mfano siku ya leo tarehe 21 Machi 2023 basi aina ya Coastal (WASAFI) lilizidisha abiria likitokea Mbeya Mjini kwenda Chunya lilipofika kwenye vituo hivyo vya ukaguzi konda alishuka na kwenda kwa askari ambao walikuwa wanasimama ubavuni mwa gari na kuwapatia elfu mbili mbili.
Hali hiyo imekuwa kero kwa wasafiri maana imekuwa ikihatarisha usalama wao na ikumbukwe kuwa barabar hiyo ndiyo yenye kona Kali ambazo kwasasa mkoa umezigeuza kuwa vivutio.
Mabasi hayo hayaanzi safari pale stand ya Airport ya zamani mpaka wahakikishe yamejaa, huku kwenye eneo ambalo wanatakiwa kukaa abiria wa nne wanalazimisha wakae watano.
Tukiachana na mwendo kasi na ubovu wa vyombo vya usafi, chanzo kingine cha ajali ni gari kuzidisha mzigo/abiria tofauti na uwezo wake.