Mbele ya Urusi, Marekani lazima ale kona!

Mbele ya Urusi, Marekani lazima ale kona!

Urusi ni mziki mwingine bhana,kwa marekani inajiona ni taifa kubwa lisilowezekana kwa chochote ila atafakari tu kua ubabe ukizidi watu wanamchoka
 
Putin hatamwacha mtu salama, maandishi ya kanga tutayasoma sana kipindi cha utawala wa mawigi, au alijua anaongelea facebook
kuna machine inaitwa B 265 krasnodar ipo majini inawasubiri..muuda imejichimbia Mediterranean sea
 
Nina uhakika SAA hii Trump atakuwa anajutia mkwara wake wa kuitishia urusi kuwa ijiandae maana ataishambulia Syria kwa makombora mazuri, mapya na janja!! (nice, new and smart)). Saa hii anajiuliza nisiposhambulia kama nilivyoahidi dunia yote wataniona mwoga! na nikishambulia maana yake nitegemee urusi kujibu mapigo kwa nguvu zote kama walivyoonya!!
Kitakachotokea ni marekani kutafuta upenyo wa kula kona kistaarabu kwa kuja na ngonjera hii: "Tumethibitisha kuwa hakuna silaha za kemikali alizotumia Syria kwa hiyo ule mpango wa kuishambulia tumeusitisha". Kwa namna hiyo atakuwa amekula kona kiaina!!!
Mshirika wake namba moja uingereza keshaonyesha dalili za kuingia mitini tayari na amesema itabidi marekani iwe na uthibitisho kwanza!!
Timu trump jiandaeni kisaikologia kumwona kinara wenu akila kona!! Kwanza alisema masaa 48 na yameisha!! Mdogo wake ufaransa akasema masaa 72 watakuwa wameshambulia nayo yanaishia!!! Timu trump jiandaeni kwa fedheha!!! Huwezi kumtishia nyau Putin!!
mapanki kamalizana nae kwani
 
mapanki kamalizana nae kwani
Kwa mapanki alikula kona pia!! Alimtishia kwa kuamru kikosi cha meli za kivita ziende huko pwani ya Korea, Kiduku akamwambia zikivuka mstari Fulani nitazizamisha!! Trump akakumbuka jinsi NK ilivyozamisha manoari ya kivita ya Korea kaskazini Mara tu ilipovuka mpaka na kuingia kwenye maji yake akaona heri aibu kuliko fedheha meli zake zikala kona mpaka leo!!!
SAA hii kim kamwalika Trump kwenye mazungumzo kama "wanaume" wawili na si kama mvulana na mwanaume!!
 
Kabsa kiongozi mm nahisi kuna baadhi yetu wanahisi kuwa Syria hawaishi binadamu kama sisi na wenye damu na malengo kama yetu. Inasikitisha kuona watoto wasiokuwa na hatia wakiangamia..
Labda huyo Trump ndo anafikiri Syria hawaishi watu!! Anapotishia kushambulia unafikiri atashambulia na kuua mbu au?
 
Sasa kwanin atweet kuichapa Syria huku akijua aliye nyuma ya Assad?

Hv hata kama ni kweli Assad ametumia sumu, solution ni kuingia vitan kuua maelfu ya watu?
Halafu haiingii akilini kutumia silaha za sumu kwa MTU uliyemshinda tayari na anakimbia! Silaha za sumu siku zote ni silaha ya mwisho kwa MTU aliyeshindwa vita! Kwa mantiki hiyo kama kweli kuna silaha za sumu zimetumika basi wale waasi ndo wamezitumia ili kumchafua Syria!!
 
Halafu haiingii akilini kutumia silaha za sumu kwa MTU uliyemshinda tayari na anakimbia! Silaha za sumu siku zote ni silaha ya mwisho kwa MTU aliyeshindwa vita! Kwa mantiki hiyo kama kweli kuna silaha za sumu zimetumika basi wale waasi ndo wamezitumia ili kumchafua Syria!!
Kweli mkuu, Dunia yetu hii sijui itabadilika lini? Hata kufufuka kwa Yesu walisema wanafunzi wake wamemwiba..

Ngoja tusubili watakavyochapana!
 
Ukishabikia vita lazima uzingatie haki kwani kuna gharama ya maisha kibinaadamu hivo lazima pasiwe na makosa au vita iwe ni njia ya mwisho. Nugu @nkobhe255 umeonesha kuhama timu bila kujali bila kujali upande unao ushabikia unapigania haki au batili?
 
Ukishabikia vita lazima uzingatie haki kwani kuna gharama ya maisha kibinaadamu hivo lazima pasiwe na makosa au vita iwe ni njia ya mwisho. Nugu @nkobhe255 umeonesha kuhama timu bila kujali bila kujali upande unao ushabikia unapigania haki au batili?
Mkuu, hilo nalijua kuwa Wasyria wengi wameteseka kwa mda mrefu sana, lakini hata wakati wa WWI na WWII watu walikuwa na pande walizoziunga mkono japo zaidi ya watu 100 milion walikufa.

Hii thread inajikita kwenye tambo za mzee Mawigi kushambulia Syria at any time, lakini mpaka sasa sioni chochote kile, ndo nimemua kuhama ili kuunga mkono juhudi za Mbilikimo
 
Marekani wao ni maneno tu na hupenda kushambulia mataifa madogo pale mashariki ya kati lakini wanaume kama Russia hawezi kubishana nao kwani mwisho wake utakuwa mbaya kwa wamarekani
 
Bado nawaza jamii yetu haijiwezi, maana marekani amefadhili kila kitu yaani mgonjwa gharama yake ni kuamka na kukaa foleni kuchukua dawa yaani imepunguza mrundikano wa wagonjwa waliolazwa kwa kuzidiwa, sasa ikitokea kweli mtiti wa vita ukaanza na ukawa mgumu kwa marekani kaamua kujilinda kuhali na mali, kweli hizi dawa wengi watashindwa kuzimudu ndipo vita vitapiganwa syria, marekani na urusi vifo vitatokea huku.
tutajifunza kujitegemea na akili zitafunguka na kujenga viwanda vyetu na mnaojiita wasomi tz mtaacha taarabu na kujikita kwenye maendeleo ya kweli
 
tutajifunza kujitegemea na akili zitafunguka na kujenga viwanda vyetu na mnaojiita wasomi tz mtaacha taarabu na kujikita kwenye maendeleo ya kweli
Siyo leo, wasomi wa sasa wanaacha taaruma zao wanakimbilia kwenye siasa utafikiri taifa na maendeleo yanasonga mbele kwa siasa
 
Kama nilivyosema kwenye Uzi huu kuwa mzee mzima Trump lazima ale kona mbele ya Putin, sasa yametimia! keshakula kona tayari! Sasa hivi anasema hajawahi kusema ni lini ataishambulia Syria, wakati dunia nzima ilimsikia akisema atashambulia ndani ya masaa 48!!! Mzee mzima kula kona aibu!! Msikie Trump anavyosema sasa:
US President Donald Trump, who said on Wednesday that missiles were "coming", has now tweeted that he "never said when".
Watu husema ukiamua kuwa mwongo basi angalau uwe unakumbuka Yale uliyosema!!! Yule wa ufaransa alitoa Massa 72 na yameshapita kitambo!!!!
Trump anachoweza kufanya dhidi ya urusi ni kuiwekea vikwazo vya kiuchumi, lakini kwa habari ya ulingoni Urusi ni MAJI marefu sana!! hayaogeleki!!!
 
Mashambulizi ya kijeshi ni mbinu za kumpoteza adui. Trump katoa taadhali, majeshi ya Syria, Iran na Urusi wapo makini kwa sasa hivi. Zikipita siku Majeshi yatajisahau huo ndo wakati wa America kutuma Kombora. Mfano nzuri kutoka kwa Israel Mashambulizi yao huwa wanatulia utasikia alfajili uwanja wa ndege umeshambuliwa
 
Back
Top Bottom