Dr Slaa ameongea katika level ya form two. Nilitaka aseme yafuatayo
-kama mitambo ililetwa ama haikuletwa maana mitambo ipo ubungo na Obama aliizindua na kuisifia je nani mwenye mitambo? maana anasema hakuna kampuni kama Dowans wala Richmund-anadai tunawalipa fedha nyingi je tunamlipa nani?
-Je si mitambo hiyohiyo zitto alishauri serekali iinunue serekali ikakataa?
-anasema shule za kata hazitadumu si kweli mbona nazifahamu nyingi tu na zimejengwa kwa uimara mkubwa ? je hizo shule ndio zinamtoa kwenye siasa? hizo shule imara kulko nyingi za binafsi .
-Anadai lowassa kazamisha fedha za maji za world bank ,kwa nini hakuchukuliwa hatua?Issue hiyo ipo katika ripoti gani? anadai yeye ndio alishiriki zaidi katika wazo la shule za kata akiwa anatafiti afrika mashariki na indonesia je hiyominaondoaje sifa yake ya kuzisimamia.je kwani tunapomsifu kiongozi mf nyerere tunadhani anachoagiza ni mawazo yake ama ya wataalam wake ?aache chuki iliyopitiliza. namdharau sana huyu bwana.
-Amesema ametishwa sana baada ya kutoka CDM mbona hakuelezea akabaki kuelezea kutishwa kwake na Rosta kipindi akiwa mbunge mbona vitisho vya sasa hasemi?
-Mbona hamhusishi Mbowe kwenye malalamiko yake ni nani anaowalalamikia?hana mpangilio wa mawazo