Mcharo son
JF-Expert Member
- Mar 4, 2015
- 6,129
- 5,076
Mwendokasi imeshathibitisha kushindwa katika awamu za mwanzo ukiangalia usafiri wa shida wanaopata Kimara. Japo hapa siasa zitaletwa kutetea hoja, lakini ukweli ndio huo. Nashangaa jitihada zinazoendelea kuleta huo mwendokasi kwa wakazi wa Mbagala. Tayari kituo cha gerezani kinaimalishwa na kule Mbagala rangi3 ili kuegesha mabasi hayo. Sasa hii sijui ni kuweka sawa ili 2020 itumike kuombea kura/la kwa wakazi wa Mbagala. Harafu wakazi wa huko nawashangaa! yaani kimya wakati wanasogezewa janga. Sasa hivi usafiri Mbagala kuja mjini ni mzuri mara 10 ya ule wa Kimara na Mbezi.
Ningekuwa mimi kwenye kiti cha maamuzi NINGESIMAMISHA KWANZA HUU MRADI NA KUTAFAKARI NJIA NZURI ZAIDI YA USAFIRI WA MWENDOKASI ambao sio mwingine zaidi ya underground train( treni ya chini kwa chini kwa route ya Mbagala). Hata kama itachukua miaka kumi kukamilisha ni kheri kuliko mkurupuko huu.
Network ya mwendokasi jijini haifai hususani Mbagala kwa sababu: inasababisha uharibifu wa miundombinu ya barabara iliopo kwa kuchimba mashimo yalioinuka (matuta) kwenye barabara iliopo. hii inaongeza kwa uchakavu wa magari na ucheleweshaaji wa magari mengine yanayotumia njia hiyo mfano gari/roli litalazimika kusimama kila kituo watu wavuke. sasa kuna magari makubwa yanaitegemea Kilwa road kupeleka na kutoa bidhaa katika viwanda vilivyopo Mbagala na njia ya Kilwa road kwa ujumla.. Shughuli za viwandani zitacheleweshwa na mashimo haya mafundi watakubariana na mimi, kuwa gari lazima litaenda service mapema kulinganisha na yale yanayopita njia isiyokuwa na mashimo. Haya Ndio maandalizi ya kuelekea 2025 ya viwanda!
Ningekuwa mimi kwenye kiti cha maamuzi, fungu la kujenga mwendokasi Mbagala ningelitumia kutengeneza njia au barabara ingine kuu ya kuingia Mbagala kupitia Tandika Buzza. hii ingesaidia sana kupunguza msongamano wa magari na kuboresha usafiri wa mabasi uliopo sasa. Eneo lililopo kwa ajili ya kujenga mwendokasi njia ya Kilwa road ndio ningelitumia kujenga TRENI YA CHINI KWA CHINI. Na hii ndio ningeiita mwendokasi mana hakuna trafik light za kupunguza kasi kama ilivyo kwa huu mkurupuko wa sasa. Mtanisamehe natumia jina mkurupuko mana naona ni kama vile uchunguzi yakinifu haukufanyika na kuona TATIZO KAMA HILI LINALOJITOKEZA SASA.
Njia karibu zote zinazoingia mjini kwa sasa zimejengewa njia mbadala. mfano kwa mtu wa Kimara Mbezi ya kule badala ya kutegemea Morogoro road anaweza zunguka Madale au Segerea, Gongolamboto badala ya njia ya airport anaweza zungukia Tabata. Sasa ni muhimu njia ya Kilwa road ipatiwe mbadala wa kuzungukia Tandika Buza. Itasaidia sana sana kuliko huu mkurupuko wa mwendokasi mnaotaka kuuweka. Na nyie wakazi wa Mbagala mmezidi ukimya hamuoni mkurupuko huu unaenda kuwadodesha.
Kilwa road imetulia wahusika msiiharibu na mkurupuko wenu wa mwendokasi. Sawazisheni pale Bandarini kuingia mjini iwe njia nne. Baada ya hapo fuateni mawazo yangu msiitibue Kilwa road please!!!
Ningekuwa mimi kwenye kiti cha maamuzi NINGESIMAMISHA KWANZA HUU MRADI NA KUTAFAKARI NJIA NZURI ZAIDI YA USAFIRI WA MWENDOKASI ambao sio mwingine zaidi ya underground train( treni ya chini kwa chini kwa route ya Mbagala). Hata kama itachukua miaka kumi kukamilisha ni kheri kuliko mkurupuko huu.
Network ya mwendokasi jijini haifai hususani Mbagala kwa sababu: inasababisha uharibifu wa miundombinu ya barabara iliopo kwa kuchimba mashimo yalioinuka (matuta) kwenye barabara iliopo. hii inaongeza kwa uchakavu wa magari na ucheleweshaaji wa magari mengine yanayotumia njia hiyo mfano gari/roli litalazimika kusimama kila kituo watu wavuke. sasa kuna magari makubwa yanaitegemea Kilwa road kupeleka na kutoa bidhaa katika viwanda vilivyopo Mbagala na njia ya Kilwa road kwa ujumla.. Shughuli za viwandani zitacheleweshwa na mashimo haya mafundi watakubariana na mimi, kuwa gari lazima litaenda service mapema kulinganisha na yale yanayopita njia isiyokuwa na mashimo. Haya Ndio maandalizi ya kuelekea 2025 ya viwanda!
Ningekuwa mimi kwenye kiti cha maamuzi, fungu la kujenga mwendokasi Mbagala ningelitumia kutengeneza njia au barabara ingine kuu ya kuingia Mbagala kupitia Tandika Buzza. hii ingesaidia sana kupunguza msongamano wa magari na kuboresha usafiri wa mabasi uliopo sasa. Eneo lililopo kwa ajili ya kujenga mwendokasi njia ya Kilwa road ndio ningelitumia kujenga TRENI YA CHINI KWA CHINI. Na hii ndio ningeiita mwendokasi mana hakuna trafik light za kupunguza kasi kama ilivyo kwa huu mkurupuko wa sasa. Mtanisamehe natumia jina mkurupuko mana naona ni kama vile uchunguzi yakinifu haukufanyika na kuona TATIZO KAMA HILI LINALOJITOKEZA SASA.
Njia karibu zote zinazoingia mjini kwa sasa zimejengewa njia mbadala. mfano kwa mtu wa Kimara Mbezi ya kule badala ya kutegemea Morogoro road anaweza zunguka Madale au Segerea, Gongolamboto badala ya njia ya airport anaweza zungukia Tabata. Sasa ni muhimu njia ya Kilwa road ipatiwe mbadala wa kuzungukia Tandika Buza. Itasaidia sana sana kuliko huu mkurupuko wa mwendokasi mnaotaka kuuweka. Na nyie wakazi wa Mbagala mmezidi ukimya hamuoni mkurupuko huu unaenda kuwadodesha.
Kilwa road imetulia wahusika msiiharibu na mkurupuko wenu wa mwendokasi. Sawazisheni pale Bandarini kuingia mjini iwe njia nne. Baada ya hapo fuateni mawazo yangu msiitibue Kilwa road please!!!