Mazao ya mpunga na mahindi kuuzwa kwa utaratibu wa stakabadhi ghalani kama korosho na pamba

X-bar

JF-Expert Member
Mar 20, 2019
1,002
1,146
Salaam;

Nimepata habari kuwa Naibu Waziri wa Kilimo Mh. Bashe ametoa maelekezo kwa vyama vya ushirika nchini kusimamia uzwaji wa mpunga na mahindi upitie kwenye vyama hivyo kwa utaratibu wa stakabadhi ghalani kama ilivyo kwa kwa mazao ya korosho na pamba.

Amesema utaratibu huo utasaidia kuongeza thamani ya mazao hayo na kuwanufaisha wakulima na kuwaepusha na unyonyaji wa wafanyabiashara wa mazao hayo.

Kwa maoni yangu naona utaratibu huu unaweza kuleta usumbufu katika upatikanaji wa chakula hasa tukizingatia kuwa mazao hayo ndo muhimu zaidi kwa nchi yetu (staple food).

Lakini nahofia utaratibu huu unaweza kuleta matatizo kwa wakulima wenyewe kama ilivyotokea katika uuzwaji wa korosho, kahawa na pamba.

Kiufupi sioni manufaa ya kutumia utaratibu huu kwa mpunga na mahindi kwa vile haya ni mazao ya chakula na si ya biashara hata kama yanauzwa.
 
Bashe naye bhana, kwa hio drama za pamba na korosho anataka kuzileta kwenye mpunga na mahindi? Pamba malipo yao ni shida, korosho hata magunia ni kwa mgao kama umeme wa Tanesco. Vitu vingine havihitaji siasa ndugu Bashe.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
utaratibu huo waweza kuleta matatizo kwa wale wanaotegemea nafaka hizo kama staple food kula kwa binadamu ni wakati wote hivyo mahitaji ya binadamu hayatasubili kupimiwa
 
Salaam;
Nimepata habari kuwa Naibu Waziri wa Kilimo Mh. Bashe ametoa maelekezo kwa vyama vya ushirika nchini kusimamia uzwaji wa mpunga na mahindi upitie kwenye vyama hivyo kwa utaratibu wa stakabadhi ghalani kama ilivyo kwa kwa mazao ya korosho na pamba. Amesema utaratibu huo utasaidia kuongeza thamani ya mazao hayo na kuwanufaisha wakulima na kuwaepusha na unyonyaji wa wafanyabiashara wa mazao hayo.

Kwa maoni yangu naona utaratibu huu unaweza kuleta usumbufu katika upatikanaji wa chakula hasa tukizingatia kuwa mazao hayo ndo muhimu zaidi kwa nchi yetu (staple food). Lakini nahofia utaratibu huu unaweza kuletamatatizo kwa wakulima wenyewe kama ilivyotokea katika uuzwaji wa korosho, kahawa na pamba.

Kiufupi sioni manufaa ya kutumia utaratibu huu kwa mpunga na mahindi kwavile haya ni mazao ya chakula na si ya biashara hata kama yanauzwa.

Bashe unakosea sana kwenye haya mazao mpunga ma mahindi. Stop this nonsense.
 
Salaam;
Nimepata habari kuwa Naibu Waziri wa Kilimo Mh. Bashe ametoa maelekezo kwa vyama vya ushirika nchini kusimamia uzwaji wa mpunga na mahindi upitie kwenye vyama hivyo kwa utaratibu wa stakabadhi ghalani kama ilivyo kwa kwa mazao ya korosho na pamba. Amesema utaratibu huo utasaidia kuongeza thamani ya mazao hayo na kuwanufaisha wakulima na kuwaepusha na unyonyaji wa wafanyabiashara wa mazao hayo.

Kwa maoni yangu naona utaratibu huu unaweza kuleta usumbufu katika upatikanaji wa chakula hasa tukizingatia kuwa mazao hayo ndo muhimu zaidi kwa nchi yetu (staple food). Lakini nahofia utaratibu huu unaweza kuletamatatizo kwa wakulima wenyewe kama ilivyotokea katika uuzwaji wa korosho, kahawa na pamba.

Kiufupi sioni manufaa ya kutumia utaratibu huu kwa mpunga na mahindi kwavile haya ni mazao ya chakula na si ya biashara hata kama yanauzwa.

Unajua unalima unataka pesa chap chap, sio uende kwenye ushirika and other nonsense.

Hivi mshahara wako tungeufanya upitie ushirika na ujinga mwingine ungejisikiaje Mr Bashe?
 
Salaam;
Nimepata habari kuwa Naibu Waziri wa Kilimo Mh. Bashe ametoa maelekezo kwa vyama vya ushirika nchini kusimamia uzwaji wa mpunga na mahindi upitie kwenye vyama hivyo kwa utaratibu wa stakabadhi ghalani kama ilivyo kwa kwa mazao ya korosho na pamba. Amesema utaratibu huo utasaidia kuongeza thamani ya mazao hayo na kuwanufaisha wakulima na kuwaepusha na unyonyaji wa wafanyabiashara wa mazao hayo.

Kwa maoni yangu naona utaratibu huu unaweza kuleta usumbufu katika upatikanaji wa chakula hasa tukizingatia kuwa mazao hayo ndo muhimu zaidi kwa nchi yetu (staple food). Lakini nahofia utaratibu huu unaweza kuletamatatizo kwa wakulima wenyewe kama ilivyotokea katika uuzwaji wa korosho, kahawa na pamba.

Kiufupi sioni manufaa ya kutumia utaratibu huu kwa mpunga na mahindi kwavile haya ni mazao ya chakula na si ya biashara hata kama yanauzwa.
Mazao yote ni ya biashara (mwaka huu yalikua declared hivyo)..... Kwasababu yotr yanatumiwa na wakulima kuingiza kipato. Ndio maana wameanzisha BODI YA MAZAO MCHANGANYIKO badala ya bodi ya mazao ya chakula....

Sent using Jamii Forums mobile app
 
kwani ni lazima ama hiayi ya anayejisikia?
Ambapo ni soko la ziada kwa anayependa..

Naomba nijifunze inakuwaje tatizo?
Salaam;
Nimepata habari kuwa Naibu Waziri wa Kilimo Mh. Bashe ametoa maelekezo kwa vyama vya ushirika nchini kusimamia uzwaji wa mpunga na mahindi upitie kwenye vyama hivyo kwa utaratibu wa stakabadhi ghalani kama ilivyo kwa kwa mazao ya korosho na pamba. Amesema utaratibu huo utasaidia kuongeza thamani ya mazao hayo na kuwanufaisha wakulima na kuwaepusha na unyonyaji wa wafanyabiashara wa mazao hayo.

Kwa maoni yangu naona utaratibu huu unaweza kuleta usumbufu katika upatikanaji wa chakula hasa tukizingatia kuwa mazao hayo ndo muhimu zaidi kwa nchi yetu (staple food). Lakini nahofia utaratibu huu unaweza kuletamatatizo kwa wakulima wenyewe kama ilivyotokea katika uuzwaji wa korosho, kahawa na pamba.

Kiufupi sioni manufaa ya kutumia utaratibu huu kwa mpunga na mahindi kwavile haya ni mazao ya chakula na si ya biashara hata kama yanauzwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mi walianza kunifurahisha pale walipokuwa wanakimbizana kutoa matamko ya kushangilia bei ya unga kupanda

Kwamba walaji tuache kulalamika unga kupanda ili wakulima nao wafaidike kwani wamenyonywa siku nyingi

Nikawa najiuliza, hivi hawa wanaamini kabisa kwamba kuna mkulima mdogo hadi leo bado anamahidi stoo!?

Wakulima wetu hawa wanalima kwa jembe la mkono, wakilima ekari nyingi ni tatu hadi tano! Kuapata mbolea na vibarua wanakopa! Mavuno hayo hayo ndo chakula, mahitaji ya msingi ya binadamu, matibabu nakadhalika!

Kwamba leo bado wanamahindi ya kusaga wauze unga kilo moja kwa 1500 had 1800/-

Sasa hivi asilimia kubwa ya hao wanaowaita wakulima wanyonge hakuna mwenye mahindi ya kuuza! Wajanja wanayo ya matumizi ya chakula na wale wenzangu na mimi huenda tunalalamika nao bei kupanda maana walishayauza yote kipindi cha mavuno na sasa wananunua kwa waliowauzia

Bashe bado anakazi kubwa sana ya kukaa chini na kuandaa mkakati bora wa kunyanyua wakulima.

Hili la stakabadhi gharani linaweza kufanya kazi ila linahitaji maboresho hasa kwa kuondoa udhaifu uliokwisha jitokeza kwenye korosho, pamba nk

Asifanye haraka sana kutafuta majibu, anatakiwa atulize akili, ajifunze, atafute ushauri kwa wataalamu, ajipe muda wa kujiridhisha ili akitoka awe ametoka kweli kweli! Likifanikiwa tutafurahi, likifeli atajua kabisa sababu gani limefeli na itakuwa rahisi kutafuta plan B

Mara nyingi maamuzi ya kukurupuka huwa yakifeli hata hujui sababu za kufeli


Sent using Jamii Forums mobile app
 
anaipinga kauli ya mkuu 'mkulima aachwe auze popote ndani au nje si kalima kwa jasho lake iweje wakati wa kuvuna mumpangie pa kuuza'

Vyama vya ushirika vinamlazimisha mkulima awauzie wao na kwa bei wanazopanga wao

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom