Maxence Melo: Watanzania wana haki ya kutokuamini taarifa iliyotolewa na Waziri Mkuu kuhusu alipokuwa Makamu wa Rais

Waziri Nape anapenda sana kukurupuka bila kushirikisha ubongo vizuri, anatumiaga sana mihemko kuliko kufikiri.

Kwani wewe Nape Nnauye ukikaa kimya juu ya hili utaonekana mjinga ama?! Haujui Watanzania wanakutazama na kukuona usivyotumia akili.
 
Simchukii ila tabia yake ni haaminiki kwa yeyote mwenye akili Timamu.
Hivi unajihesabu una akili timamu?
JamiiForums-565905357.jpg
 
sasa nimeamini kabisa kwamba Mpango (PhD) ndiye raisi ajaye Tanzania 2025 or sooner ukiona mpaka ceo wa JF anachangia ujue mama yao karibia anakabidhi kiti, ujue kwamba hawa wote ni sehemu ya mapinduzi sasa Mpango hatabiriki hawaelewi uraisi wake utakuwaje ndio maana wanatapa tapa huku na kule, all I kniw Mpango is christian so angalau atawasha umeme, umeme ukiwepo mengine tutajipanga hatuhitaji serikali ilo itupe miundo mbinu baasi.

what goes around comes around …
 
Naona hata Nape alikuwa hajui alipo na alifikiri ya mitandaoni ni kweli,
Kwanini hakusema watashughulikiwa waliosambaza habari mda ule na kasubiri mpaka kaonekana?
Kuna wakati mwingine tunawaza mengi mjue na tunajiuliza wenyewe
 
Tumwanini vipi PM na alishawahi kutudanganya kuhusu marehemu Magufuli?! Mazingira yanafanana na yaliyotokea juu ya VP.

..uko sahihi kabisa.

..Na kuongezea, hata kama PM Majaliwa angekuwa hajawahi kudanganya kuhusu Jpm bado unayo haki ya kutokumuamini kuhusu VP Mpango.

..VP kusafiri bila wananchi kupewa taarifa ni makosa. Na mimi sijawahi kusikia VP wa nchi yeyote ametumwa " kazi maalum. " Majukumu ya namna hiyo hufanywa na agents wasiojulikana, na sio VP ambaye dunia nzima inamjua.
 
Aya ya mwisho ndio imebeba ujumbe mkubwa.

Uongo uliasisiwa awamu ile na kutukuzwa sana , tulipokemea tukaitwa sio wazalendo.

Imagine watu walikua wanastage matukio ya mashirika ya umma kutoa gawio unakuta kina ATCL , TTCL na mengineyo yaliyokuwa yanatoa magawio bandia huku uhalisia yakiwa hoi taabani.
 
View attachment 2840103

Akizungumza East Africa Radio asubuhi hii, Disemba 12, 2023, Mkurugenzi Mtendaji wa JamiiForums, Maxence Melo amesema Haki za wananchi zinazopatikana nje ya mtandao zinapaswa kutolewa pia ndani ya mtandao kwa kuwa ni haki za msingi zinazogusa maisha ya watu.

Kuhusu kutokutolewa kwa taarifa za alipokuwa Makamu wa Rais Dkt. Mpango, Melo amesema Makamu wa Rais ni kiongozi wa umma, analipwa kwa pesa za umma. Hata kama alienda kwa kazi maalum ni lazima wananchi waambiwe kwa kuwa analipwa kwa kodi zao. Hata kama hawatasema kaenda kufanya kazi gani lakini wananchi wanapaswa kujua kaenda wapi, kwa siku ngapi.

Akitoa maoni yake kuhusu hatua ya Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Nape Nnauye kuwashughulikia waliotoa Taarifa za uzushi kuhusu kifo cha Makamu wa Rais, Melo amesema "Nimesikia Waziri atachukua hatua, ni sawa. Lakini wewe pia ukiguswa sheria hii ichukue mkondo wake, isionekane ipo kwa ajili ya kulinda viongozi pekee. Kuna ushahidi wa matukio mengi yametokea kwa wananchi na hakuna hatua yoyote iliyochukuliwa"

Ameongeza "Sheria ya Makosa ya Mtandao (Kifungu cha 16) inasema anayetoa taarifa za uongo kwa makusudi atashughulikiwa. Kazi ipo kwenye kuprove kama mtu alifanya kwa kusudi, lakini sheria hizi hazitumiki zikivunjwa kwa wananchi wa kawaida lakini zikivunjwa kwa viongozi ndio zinafanya kazi. Kuna "impunity"

Katika hatua nyingine, amebainisha kuwa kwenye matukio muhimu yanayohusisha viongozi wa kitaifa taarifa sahihi zinapaswa kutolewa. Kama kuna uzushi taarifa sahihi zitolewe kuondoa uzushi huo maana kukaa kimya huendeleza kusambaa kwa uzushi.

Melo aliulizwa pia ni kwa nini habari za uzushi kuhusu afya ya Makamu wa Rais ziliendelea kusambaa hata baada ya Waziri Mkuu kutoa taarifa. Alisema watanzania wana haki ya kutokumwamini Waziri Mkuu, yaliwahi kutokea enzi za Uongozi wa Hayati Magufuli, mazingira ya wakati huo na sasa kwa kiasi fulani yalikuwa yanafanana.
Good.
 
Max anasema "wananchi wana haki ya kutokuamini" taarifa ya serikali, huo ni uamuzi wao kuamini au kutoamini, na ndio haki yao inayozungumziwa.

Lakini siku zote hakuna haki ya upande mmoja, hili tukubaliane, hata serikali nayo iliyotoa taarifa ambayo wengine wamegoma kuiamini, ilikuwa ni haki yake, hili nalo lieleweke.

Naona wengi wanasema wana haki ya kutoiamini taarifa ya serikali kwasababu ilitolewa na PM, yule ambaye aliwahi kutudanganya kuhusu hali ya Magufuli.

Sasa kiuhalisia inatakiwa hivi, anayeipinga taarifa ya PM anatakiwa aje na uthibitisho wa kutuambia wapi Dr. Mpango alilazwa, na ugonjwa aliokuwa anaumwa, lakini kutuambia tu PM haaminiki kwasababu ya uongo wake wa mwanzo, hili kwangu halitoshi kunishawishi 100%

Naamini huwezi kutumia past kuhukumu present, kila hukumu lazima iambatane na ushahidi wa pande mbili, kisha mahakama ipime uzito ndio iamue without any doubt.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
 
..uko sahihi kabisa.

..Na kuongezea, hata kama PM Majaliwa angekuwa hajawahi kudanganya kuhusu Jpm bado unayo haki ya kutokumuamini kuhusu VP Mpango.

..VP kusafiri bila wananchi kupewa taarifa ni makosa. Na mimi sijawahi kusikia VP wa nchi yeyote ametumwa " kazi maalum. " Majukumu ya namna hiyo kufanywa na agents wasiojulikana, na sio VP ambaye dunia nzima inamjua.
Mkuu uko sawa kabisa achilia mbali kiongozi kukaa nje siku 40 eti kwa kazi maalum.

Kwa kumbukumbu zangu kuna kiongozi aliwahi kukaa India sana , alipouliziwa Magufuli akasema "nilimtuma kwa matibabu nje" sasa uongo kama huu ulikuja kumkuta Magufuli mwenyewe yuko hoi halafu nje huku wanaambiwa yuko fit ofisi ila yuko na mafile mengi.

Hadi miaka 2 imepita tena leo yanajirudia yale yale, hapo ilitakiwa kitengo cha habari ofisi ya VP , Waziri wa habari yule mwanamipasho , msemaji mkuu wa serikali na huyo baba wa uongo kutoka Ruangwa walitakiwa kuwekwa pembeni ila kwa kua ni banana republic sheria zinafanya kazi kwa wezi wa kuku tu.
 
Back
Top Bottom