Maxence Melo atinga ofisi za IMF Washington DC

Maxence Melo atinga ofisi za IMF Washington DC

Sasa badala ya kukutana na JPM anakwenda kumwambia Director wa IMF?Max ulitakiwa ukamwambie Magufuli bwana,au unamwogopa ? Huyu Kristina hatosaidia lolote. Mwenye rungu la kuboresha mazingira ya wafanya biashara hapa Tanzania ni JPM.
Mawazo yako
 
Mkuu Maxence Melo rudi haraka uje na mpango wa kuanzisha JF SACCOS na mie niwe mtunza hazina na nnakuhakikishia kuwa "Kibubu" chetu kitakuwa salama wala manoti hayawezi "kuyeyuka" kama kule Arachugga maana mie ni mmoja kati ya wanafunzi bora kabisa wa Mshana Jr
 
Magufuli hafurahishwi na taarifa Kama hizi, anafurahia kuona watu wakishindwa na kuanguka na kuaibika
Ni shetani pekee apendaye anguko la wengine na usimfananishe na Laisi wetu mpendwa.
 
Aiseee; amefikaje huko? Ni JF au kuna chombo kingine?

Heko na Hongera nyingi. Natumaini ombi litafanikiwa.

Lakini ngoja nikutupie dongo laini.
Hiyo picha ya kwanza umejinyenyekesha sana mkuu! Au ni kabla ya kuwasilisha mahitaji kwa mkubwa?

Heri unyenyekevu kuliko kujimwambafai
 
Jiwe akijua kuwa yuko huko kwa mabeberu atampima mkojo kwani kitu hicho jiwe hapendi, labda kama atamsifia jiwe kuhusu ununuzi wa ndege, na ujenzi wa madaraja.
 
Sasa badala ya kukutana na JPM anakwenda kumwambia Director wa IMF?Max ulitakiwa ukamwambie Magufuli bwana,au unamwogopa ? Huyu Kristina hatosaidia lolote. Mwenye rungu la kuboresha mazingira ya wafanya biashara hapa Tanzania ni JPM.
Magufuli kabla ya kumsaidia atamuomba atoe siri za watu wenye id hapa JF. Au msukuma mwenzako unamuonaje?
 
Back
Top Bottom