Mawaziri wenye PhD Feki hawa hapa!

Mawaziri wenye PhD Feki hawa hapa!

Ana MBA tena ile strong ya miaka ileeeeee..enzi za mwalimu. Siyo hizi ambazo kila mtu anasoma siku hizi evening classes.

Mama Nagu ametumia muda mwingi maishani mwake kusoma - kuanzia kilakala hadi UDSM. Ametumia muda mwingi pia kupata vidiploma kibao tu ili kujiendeleza. Ni aibu kuwa PhD yake inaweza kufuta yote hayo aliyofanya kujiendeleza kielimu.
 
si waje open university tumwangukie Prof Mbwete Open University wapate vyeti vya ukweli.
 
Mama Nagu ametumia muda mwingi maishani mwake kusoma - kuanzia kilakala hadi UDSM. Ametumia muda mwingi pia kupata vidiploma kibao tu ili kujiendeleza. Ni aibu kuwa PhD yake inaweza kufuta yote hayo aliyofanya kujiendeleza kielimu.

You can say that again!
Kama ni kichwa kimekaa vizuri mno... sidhani hata yeye ana wasiwasi ... maana hata kama ni kufanya formalities arasimishe hicho kisomo cha kupata PhD haitakuwa tatizo kwake hata kidogo tatizo kwake labda ni muda tu.Tabu ni kwa hao wenye vichwa ngumu visivyojiweza. Kaaazi kweli kweli!
 
Simpo....kama PhD haitambuliki...acha kutumia u-dokta. Kama wahusika waliwasilisha nyaraka feki, kamata hiyo mutu na fukuza kazi. Kama vetting process ni porous...timua hao vihiyo wanaofanya vetting....hivyo ufumbuzi ni simpo...TIMUA, TIMUA ndo heshima itarudi.
 
katika hili sakata....nini msimamo wa serikali maana kwangu mimi ni kama hakuna any official statement kuonyesha serikali inalichukulia vipi hili swala. Kelele zimepigwa sana toka mwaka jana but nothing has happened.
 
Hivi inaongeza nini PhD kwa mwanasiasa? mimi sioni kama wananchi wanachagua wanasiasa kwasababu ya vyeti?? hawa jamaa ni kwamba wamezoea uwizi sasa wameenda kuiba hata kitu ambacho hakina sababu..
 
Watanzania kinachotuharibia nchi yetu ni kupenda sana njia za mkato...shortcuts kwenye kila kitu.
 
Kuna huyu jamaa mwingine Dr Nangale naye alinunua PhD yake?
 
Nijuavyo mimi ni kwamba forgery ya documents kama vyeti vya masomo ni kosa la jinai. Tungoje tuone kama Afande Mwema atakuwa na ubavu wa kutuma vijana wake wakiwa na pingu wakawakamate wahusika. All are equal under the law.
 
sasa si wajiudhuru kwa kufoji kwao, maana wanawafundisha nini wananchi wanaowaongozi, kama vp warudi tena darasani wakatafute zilizohalali, wanataka makubwa na heshima ndio maana wanafanya hivi, lakini akiwa mlalahoi kafanya hivi mbona fasta tu utasikia kapelekwa mahakamani, lakaini hwa toplayer tunawaona tu wanaendelea na kazi zao tena hakuna bughudha hata kidogo
 
kwa kuwa sisi ccm kauli mbiu yetu ni kulindana....tutawalinda hawa wote na hawatafikishwa popote..........au mmesahau mambo ya watoto wa vigogo BOT? Sisi ccm ni balaa nchi ni mali yetu tutaongoza tunavyotaka msitubugudhi.....wacha tule maisha.....
 
WC, Hii nchi ngumu sana...

Tumeshaona wasomi feki
Bidhaa kibao feki
mikataba feki
kesi feki
dhamana feki
Raia feki
ahadi feki
Mitihani feki

Sasa subiri utasikia
Mashtaka feki
makaripio feki [kutoka kwa mkuu]
ahadi feki


sijui tumebakiza nini tena feki

Kenya ni nchi ya kitu kidogo... Tanzania iwe nchi ya mafeki tu!

uchaguzi feki
rais feki
serikali feki
maendeleo feki
 
Muhimu kupata viambatanisho alivyotumia jamaa kufikia conclusion kwamba jamaa wana vyeti fake.
Sitta azungumzia digrii za vigogo zenye mushkeli




Na Muhibu Said



21st October 2009







Sitta2(6).jpg

Spika wa Bunge, Samuel Sitta.



Spika wa Bunge, Samuel Sitta (pichani), amesema tuhuma dhidi ya mawaziri sita na wabunge wanne waliotajwa kuwamo katika orodha ya watuhumiwa 19 wenye vyeti vya elimu vyenye mushkeli, zinafanyiwa kazi.
Tuhuma hizo zinadaiwa kuwasilishwa kwa Spika wa Bunge na Mwanaharakati, Kainerugaba Msemakweli, kwa njia ya barua na viambatanisho, Septemba 15 na 16, mwaka huu.
Akizungumza na Nipashe kwa njia ya simu jana, Spika Sitta alisema kwa sasa yuko nje ya nchi na kusema kwamba: "Nadhani wataalamu watakuwa wanazifanyia kazi."
Awali, Katibu wa Bunge, Dk. Thomas Kashililah, jana alisema kuwa juzi aliwauliza vijana wake kama barua ya Msemakweli imewasilishwa katika Ofisi za Bunge na kusema kwamba: "Wakaangalia kwenye kitabu cha register (usajili), wakasema hawajaiona."
Hata hivyo, akizungumza na Nipashe jana, Msemakweli ambaye kitaaluma ni Mwanasheria, alisema barua aliipeleka Septemba 15, mwaka huu na kuikabidhi kwa kiongozi wa Masijala ya Ofisi za Bunge kama utaratibu unavyotaka na kugongwa muhuri wa Ofisi ya Bunge.
Alisema siku iliyofuatia (Septemba 16, mwaka huu), alipeleka viambatanisho vyake, pia wakamgongea muhuri wa Ofisi ya Bunge.
Nipashe inayo nakala ya barua na viambatanisho hivyo, ambavyo vyote vinaonyesha kugongwa muhuri wa Ofisi ya Bunge.
Mawaziri na wabunge hao walihusishwa na kashfa hiyo kufuatia utafiti huru uliofanywa na Msemakweli kwa msaada wa Tume ya Vyuo Vikuu nchini (TCU), katika kipindi cha mwaka mmoja na kubaini kwamba wanasiasa hao walitumia vyeti vyenye mushkeli na kuviwasilisha katika ofisi za umma kwamba wana elimu hiyo, kitu ambacho si kweli.
Kwa mujibu wa Msemakweli, utafiti huo ulianza kufanyika Juni 25, mwaka jana hadi Oktoba 9, mwaka huu katika nchi za Marekani, India na Uingereza, ambako vigogo hao wanadaiwa kuwa walisoma na kupata shahada hizo.
Baada ya kubainika kwamba, hawana sifa za elimu wanazodai kwenye wasifu wa elimu zao, Msemakweli alisema ripoti hiyo ilikabidhiwa kwa Ofisi ya Spika wa Bunge.
Alisema kitendo cha kuwasilisha nyaraka zenye mushkeli katika ofisi ya umma ni kinyume cha Ibara ya 68 na 56 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Pia, ni kuvunja sheria ya Vyuo Vikuu ya mwaka 2005 (5 na sheria ya makosa ya jinai sura ya 16 (333).
Msemakweli alisema hayo alipozungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Jumapili iliyopita na kusema kwamba, alilazimika kufanya utafiti huo baada ya kuingiwa na wasiwasi kuhusu elimu ya vigogo hao.
Alidai vigogo hao wanajiwasilisha kuwa wana shahada za masuala ya kimataifa na diplomasia, biashara na utawala, wengine shahada za uzamili, udaktari wa falsafa, na wengine shahada za ualimu nakadhalika, wakati si kweli.
Msemakweli alisema katika taarifa aliyowasilisha kwa Ofisi ya Spika wa Bunge, aliomba iwawajibishe vigogo hao kwa kashfa hiyo na kwamba, anaendelea na utafiti kwa vigogo wengine tisa na kwamba, atauarifu umma mara tu atakapokamilisha.
Msemakweli alidai ana ushahidi wa kutosha juu ya madai anayoyatoa dhidi ya vigogo hao kwani amefanya utafiti wa uhakika na kwamba, kigogo yeyote atakayehisi kuwa ameonewa aende kwenye vyombo vya sheria na yuko tayari kwenda kuthibitisha madai yake.
 
kwa kuwa sisi ccm kauli mbiu yetu ni kulindana....tutawalinda hawa wote na hawatafikishwa popote..........au mmesahau mambo ya watoto wa vigogo BOT? Sisi ccm ni balaa nchi ni mali yetu tutaongoza tunavyotaka msitubugudhi.....wacha tule maisha.....

Nadhani ndugu hujafahamu nini maana ya uongozi na nini ubeberu. Kauli yako ni ya kijeuri na dharau na kumbuka walioweka CCM madarakani ni wananchi tangu zama za ASP na TANU, hivyo basi wananchi watakapochoka hawatashindwa kuitoa CCM madarakani hata kama wawe na silaha gani. Iogope nguvu ya umma. Kama huamini tizama Senegal kilitokea nini na Rwanda kimetokea nini!!! mara nyingi dola ikiwa ya mabavu na wananchi wakiona hamna haki basi linalofatia ni lawlessness country na hapo hakuna atakayekuwa na amani si tajiri wala maskini. Nakushauri badilisha kauli yako.

Na swala vyeti ni kwamba hawajamaa wametudanganya na sio kutudanganya tu wamewadanganya wananchi. Uongozi ni dhamana sasa ukiwa unadanganya elimu yako tu je utaaminika kwa uongozi. maana dhamana inataka uaminifu sasa unadhani mie nitampa jamaa kura akija kugombea jimbo langu hata siku moja. Hivyo kimsingi ni tofauti ishu hii na watoto wa BOT. hawa jamaa ni wabunge wakivurunda basi hapati mtu kura. BOT ni serikali ambayo imejaa mafisadi wakivurunda hakuna mtu wa kuwauliza maana vigogo wapo nyuma.
 
....pia wapinzani kama CUF au Chadema walitakiwa wafungue kesi mara tu baada ya uchaguzi kupinga matokeo yao kwa kuwa waliwahadaa wapiga kura kuwa wao ni wasomi weledi hivyo wawaamini kuwawakilisha bungeni.wangetumia kesi ya KIHIYO lakini vyama vitu vya upinzani kazi kusema tu vitendo hakuna.muda huu wangetumia kupita kwenye majimbo ya hawa wabunge wenye elimu feki kuwambia wananchi kuwa hawa ni matapeli.kiasi kipindi cha uchaguzi kikifika hawa jamaa wamechafuka.ndio maana wengi wao wamepata uwaziri kwa vile rais aliamini anachagua watu wasomi.tumezungumza sana sasa vitendo tunataka toka CUF na Chadema.

Chitalilo alifunguliwa kesi na wapiga kura wa jimboni mwake kwa kugushi vyeti. Ingawa alipatikana na hatia lakini Spika wa Bunge akasema hiyo kesi haihusiani na mambo ya Bungeni. Wanalindana. Mpaka leo bado ni mbunge. Kuwepeleka mahakamani ni kupoteza muda, Dawa ni kuwa na wabunge wa upinzani wengi tu bungeni.


.
 
Mkuu Mkandara,
Umenena kweli. Tatizo letu ni ulimbukeni wa elimu. Mtu hasomi ili aelimike, na kutumia elimu hiyo kwa manufaa yake na jamii, bali ili watu wamjue kwamba amesoma. Forgery Tz ni nyingi mno. Halafu, cha kuchekesha ni wakati Raisi alipotangaza majina ya mwawaziri: Nakumbuka alitulia kidogo, akatabasamu, akasema ilikuwa kazi kweli kweli kuwateua mawaziri, maana kumejaa Madokta, na Maprofessor! Halafu bado akaishia kujipinga mwenyewe kwa kusema " Lakini uwaziri hausomewi". Sasa kulikuwa na haja gani ya kupapalikia hizo PHD na Proffesor wakati anajua fika kwamba uwaziri hausomewi? Mie hapa naona jambo moja tu : wanamtandao walijipanga in advance namna watakavyogawana madaraka, hivyo kuandaa digrii feki, (ambazo nahisi hata Mh. alijua hivyo). Kwa hiyo aliwateua akijua hivyo. Ila kinachotokea sasa ni kujipanga kwa ajili ya uchaguzi 2010. Nahisi Muungwana anataka kuwatema , maana ndo hao hao wanaomhujumu kinamna. Kwa kuwa jamaa wana pesa, njia pekee ya kuwashinda ni kutumia busara hii ambayo hawawezi kuponyoka, wanatakiwa waachie ngazi kwa udanganyifu. Swala hapa tusijadiri kama digrii zinatambulika au la, swala ni je wamesomea? Hata kama ni kutumia open University, bado unaweza kutrack kama mtu amesomea au la. Ukweli ni huu: Muungwana anajua fika kuwa jamaa wana vyeti feki, ila kwa kuwa wanamhujumu kinamna , basi amewatosa na safari hii hawaponi, maana ndio waliokuwa wanamsulubu Spika Sitta, sasa naye zamu yake kuwatwanga....Patamu hapo!
 
Mkuu Mkandara,
Umenena kweli. Tatizo letu ni ulimbukeni wa elimu. Mtu hasomi ili aelimike, na kutumia elimu hiyo kwa manufaa yake na jamii, bali ili watu wamjue kwamba amesoma. Forgery Tz ni nyingi mno. Halafu, cha kuchekesha ni wakati Raisi alipotangaza majina ya mwawaziri: Nakumbuka alitulia kidogo, akatabasamu, akasema ilikuwa kazi kweli kweli kuwateua mawaziri, maana kumejaa Madokta, na Maprofessor! Halafu bado akaishia kujipinga mwenyewe kwa kusema " Lakini uwaziri hausomewi". Sasa kulikuwa na haja gani ya kupapalikia hizo PHD na Proffesor wakati anajua fika kwamba uwaziri hausomewi? Mie hapa naona jambo moja tu : wanamtandao walijipanga in advance namna watakavyogawana madaraka, hivyo kuandaa digrii feki, (ambazo nahisi hata Mh. alijua hivyo). Kwa hiyo aliwateua akijua hivyo. Ila kinachotokea sasa ni kujipanga kwa ajili ya uchaguzi 2010. Nahisi Muungwana anataka kuwatema , maana ndo hao hao wanaomhujumu kinamna. Kwa kuwa jamaa wana pesa, njia pekee ya kuwashinda ni kutumia busara hii ambayo hawawezi kuponyoka, wanatakiwa waachie ngazi kwa udanganyifu. Swala hapa tusijadiri kama digrii zinatambulika au la, swala ni je wamesomea? Hata kama ni kutumia open University, bado unaweza kutrack kama mtu amesomea au la. Ukweli ni huu: Muungwana anajua fika kuwa jamaa wana vyeti feki, ila kwa kuwa wanamhujumu kinamna , basi amewatosa na safari hii hawaponi, maana ndio waliokuwa wanamsulubu Spika Sitta, sasa naye zamu yake kuwatwanga....Patamu hapo![/QUOTE]
Kwa hiyo Makongoro Mahanga ndio aliyelikoroga?alijua ana Phd Feki akaanza kumsakama Sitta na kundi lake.inabidi yafanyike maandamano kushinikiza hawa watu waachie ngazi.tusimuachie Msemakweli peke yake. wameturubuni Watanzania wote.
 
Back
Top Bottom