Mawalla Advocates yaijibu Jamii Forums

Mimi namjua Nyaga vizuri kutoka wakati wa Ilboru na si fisadi. Ni kweli kwamba ni mtu ambaye si wa bei nafuu na kama akifanya kitu ata toa bill kubwa kwa kazi yake lakini kazi yake ni nzuri na haina usirisiri hata kidogo. Ni business lawyer mzuri na nilivyoongea na wafnaya biashara na mikataba ya biashara ni mtu wa uwazi. Nyaga ni mfano mzuri kwa vijana wa Kitanzania ni jinsi gani unaweza kufanya kazi kwa maadili mema.

Kama unamjua ni vizuri sana na inaelekea unamjua toka shule pia ujue kwamba unavyomjua mtu kwa nje ni tofauti kabisa na alivyo na anachofikiri, Kimsingi mimi simkubali huyu jamaa kwa haya yafuatayo:

Kutumiwa na Singita Grumeti Reserve: Jamaa huyu amekuwa akitumiwa na Singita Grumeti Reserve ili achukue maeneo kule Serengeti ili wao waweze kuongeza Camps zao na pia kufanya watu wengine wasianzishe Camps kule. Ameleta mzozo mkubwa sana kule kwenye vijiji vya Motukeri na nata kwa kuwahonga wenyeviti wa vijiji na madiwani pesa ambazo wao wanaona ni nyingi ili wampe shamba kubwa kama hekari 1000 ili afugie mifugo yake akiwa na kampuni yake ya kisanii yenye jina mbele then inaishia na Holdings. Hii imesababisha watu kuvurugana na kugombana kutokana na Ngawira anazopewa na Grumeti kuwahadaa wanakijiji kujiongezea maeneo

Gomba Estate na Burka. Kwa nini jamaa huyu anaonekana kwenye mikataba ya mashamba makubwa kama haya akiwa kama consultants? Nachokijua ni kwamba mashamba haya yakiisha muda wake huwa mali ya serikali na muwekezaji huyarudisha kwa Serikali. Yeye anakuwa nani hapo katikati in between Serikali na muwekezaji? na mbona baada ya ugawaji yeye hubaki na plot nyingi sana ambazo huwagawia rafiki zake including pilosi ambao humsaidia kwenye mambo yake?

Mawala Private Road:Huyu jamaa ana barabara yake ambayo kila anayepita hulipia except watu wanaokaaa jirani. makampuni kama Sokwe, Thomson, African environments hutozwa zaidi ya $1000 kwa mwaka kwa ajili ya kutumia barabara hiyo. Na kuna ushahidi mkubwa sana kuwa eneo hilo lote wamegawana na nywele nyeupe utadhani wao tu ndo wanastahili kupata hayo maeneno

In short huyu jamaa ni mbinafsi na pia anatuona sisi Watanzania ni wajinga sana kiasi cha kutumiwa kama Carl Peters kutufanyia mikataba ya kilaghai
 
Jamani hebu mwangalieni huyo jamaa aliyekaa hapo pembeni ya msemaji mkuu. Ni kama vile anaujua ukweli wenyewe na anatafakari ama auweke ukweli hadharani au aendelee kutumiwa kudanganya. Kwa ujumla haonekani kuridhishwa na kinachozungumzwa
 
Mawala Advocates
Rex Attorneys
Mkono Advocates
Malegesi

and so on, ni agents wa serikali (CCM) kuiibia nchi
 
Kweli paa linateleza!

Hivi hii nchi kuna jambo litafanywa kwa usahihi bila kutumbukizwa kwenye ufisadi? Kuna idara yoyote ya serikali inaweza kusema kwamba yenyewe haijihusishi na ufisadi? Kuna wafanya biashara wanaofanya biashara na serikali bila ufisadi?

sliding roof, asante and now let the house slide

Hivi watu mnadhani civil servants woote ni mafisadi? kuna watu wanafanya kazi za umma ili nyinyi muishi vizuri, wanazoa vinyesi, wansafisha vidonda, na kutibu ndugu zenu nyinyi stupid thinkers ambao kazi matusi kila leo hivyo wakiweka tools chini itakuaje? acheni hizo kauli zenu za kejeli jamani zinakatisha tamaa!! ofcourse kama kawaida yenu mtaanza matusi na kusema crap and what have you. ila mjue kuna maandishi yanakera mno! why cant you be specific mnatukana idara ipi ya serikali! mki generalize mnakatisha tamaa watu wengine ambao ni muhimu!! hivi mkidundwa marungu huko nani asafishe na kutibu vidonda vyenu?
 
Asanteni Saaana watanzania wenzangu....Nafurahi kwani inaonyesha hawa jamaa wanajitihada kubwa za kutafna nchi yetu,

Ndo watu wetu hao kila mtu anataka kula,

Mh....
 
Hivi watu mnadhani civil servants woote ni mafisadi? kuna watu wanafanya kazi za umma ili nyinyi muishi vizuri, wanazoa vinyesi, wansafisha vidonda, na kutibu ndugu zenu nyinyi stupid thinkers ambao kazi matusi kila leo hivyo wakiweka tools chini itakuaje? acheni hizo kauli zenu za kejeli jamani zinakatisha tamaa!! ofcourse kama kawaida yenu mtaanza matusi na kusema crap and what have you. ila mjue kuna maandishi yanakera mno! why cant you be specific mnatukana idara ipi ya serikali! mki generalize mnakatisha tamaa watu wengine ambao ni muhimu!! hivi mkidundwa marungu huko nani asafishe na kutibu vidonda vyenu?

Wewe mbona unaropoka? Sema hadharani hapa-NI IDARA GANI YA SERIKALI ISIYO NA UFISADI? Kuwa specific, otherwise itakuwa crp!
 
Hivi watu mnadhani civil servants woote ni mafisadi? kuna watu wanafanya kazi za umma ili nyinyi muishi vizuri, wanazoa vinyesi, wansafisha vidonda, na kutibu ndugu zenu nyinyi stupid thinkers ambao kazi matusi kila leo hivyo wakiweka tools chini itakuaje? acheni hizo kauli zenu za kejeli jamani zinakatisha tamaa!! ofcourse kama kawaida yenu mtaanza matusi na kusema crap and what have you. ila mjue kuna maandishi yanakera mno! why cant you be specific mnatukana idara ipi ya serikali! mki generalize mnakatisha tamaa watu wengine ambao ni muhimu!! hivi mkidundwa marungu huko nani asafishe na kutibu vidonda vyenu?
huo ufisadi un afanywa na wakubwa zao wakishirikiana na watu wa chini wachache.
 
Mnavyosema sofware kwa 1 billion inategemea sofware inafanya nini!!!. Kuna sofware za $10,000 na kuna sofware za $1 Billion!! hivyo ni vigumu kusema bei bila kujua sofware zina uwezo gani.
 
Just imagine,arusha amepima viwanja na akawauzia halmashauri.....ardhi ni ya serikali,bado anaiuza kwa srikari,na hapa alijiita land use and planning consultant!huu si wizi kweli....

Hii kali ya mwaka
 
Chalii amenunua ndege aina ya MT-7(MAULE), , NA KWA SASA anawachungulia wabaya wake kwa chini wakipita kama nyenyere!
BSOsph3ajyyJAAAAAElFTkSuQmCC
.......with a price tag of $240,000. Du!!!
View Photos of a 2010 Maule Mt-7-235 for sale in WESLACO, Texas - AeroTrader.com
 
Sasa hii nchi kila mtu ni msemaji.. Sijui hili litaisha lini...

Brella wakaguliwe na mkaguzi mkuu wa serikali.. Halafu taarifa itolewe kwa umma..
 
Mkur%252520Nyaga%252520Mawalla%252520akiongea%252520na%252520wanahabari%2528kulia%2529%252520shoto%252520Bertholomeo%255B1%255D.JPG


Wakili kutoka Kampuni ya Mawalla Advocates kutoka Arusha Nyaga Mawalla (kulia) akionyesha kielelezo na kivuli cha gazeti moja kilichoandika habari kuhusu Kampuni ya Mawala kufanya biashara ya kununua software kwa thamani ya shlingi bilioni moja. Kampuni hiyo imekanusha mbele ya waandishi wa habari jana jijini Dar es salaam kwamba haijawahi kufanya biashara hiyo. Pichani (shoto) ni wakili Lemmy Bartholomew wa Kampuni ya Mawalla Advocates. Picha na Mwanakombo Jumaa-MAELEZO.


Kama mnakumbuka yapata mwezi mmoja nilianzisha thread hapa kwenye Siasa lakini ilihamishiwa Business. Ila ilikuwa ni critical not only kwa BRELA kama institution na public body bali ili question not only utendaji wa mkuregenzi wa BRELA bwana MAHINGILA, ile thread ili question mpaka uwezo wa kishule na uwezo mdogo wa kujieleza aliouonyesha kwenye website ya BRELA.

thread yenyewe hii hapa:

https://www.jamiiforums.com/busines...597-mahingila-of-brela-another-dodgy-ceo.html

Apparently a local newspaper (sijui gazeti gani) bila ku-quote au kuipa JF credit kwa kugundua uozo ule wa BRELA na CEO wake kutumia 1 billion kuiuzia BRELA software ambayo haikufanya kazi.

Sasa kwa kuonyesha kuwa ile thread ilikuwa muhimu na imewagusa watu MAWALLA ADVOCATES wameitisha press conference na kukanusha kuwa hawaijauzia BRELA fake software.

Cha ajabu ni kuwa kule BRELA kwenyewe hawajataka kujibu hizi tuhuma za ubadhirifu wa pesa za umma infact wamekaa kimya as if hii issue sio muhimu kwao.

Sasa mnasema ngoma ilale au?

Lemmy Kushoto na mwona Paulo Nyaga Mawalla duuuuuh

Hao wanunue software gani ya mabilioni hao ni wajanja wa kucheza na viwanja vya watu mkiwachunguza mawalla wamejilimbikizia viwanja karibia nchi nzima na kuuzia wananchi kwa bei ya juuuu me sijaona Mawalla Advocate imetendea jamii kitu cha maana zaidi ya kupola viwanja tuuuu basi.

huku kwetu maswa wamejibebea maheka ya viwanja na huko msoma wao ndio walisababisha yule mtoto wa mkulima akafungwa wakati yuko darasa la saba kisa alienda kuchunga ng'ombe kwenya eneo la wawekezaji kwa jina Gurumet Reserve. sasa hawa ni mawakili kweli kama walishindwa mtetea yule mtoto wa bunda mpaka akawekwa magereza na serikali ikaingilia kati

 
Sasa hii nchi kila mtu ni msemaji.. Sijui hili litaisha lini...

Brella wakaguliwe na mkaguzi mkuu wa serikali.. Halafu taarifa itolewe kwa umma..


Brella huko kuna kitu(Demu) wa Paul Nyaga Mawalla pale hata mfanyeje

 
Hypothetically,

Je Mawalla Advocates wanaweza kuwapiga JF injunction?

If so hii itaangukia kwa nani Jamii Media au?

Just curious

sababu? well that's an option being discussed among others na huyo aliyenunua ndege hapo juu
 
Mimi si mtetei Nyaga lakini naeleza ukweli tu ninavyojua mimi

1. Software: Si kitu cha kirahisi tu ni lazima ujue ni software gani na inafanya nini mafano software ya MPESA inathamani gani? hivyo ni vigumu kujua na kama si sofware nzuri basi wasinunue. Kitu kimoja tu ambacho sijakipenda ni kwamba kwa kampuni kununua sofware ni lazima wajue support kama ipo maana sofware zinahitaji development na zinaweza kuwa na hitilafu.
2. Pili mimi siko bongo hivyo hata sijui Brela ni nini lakini najua unaweza kuuza sofware kwa zaidi ya $1 million. Nimesoma kwa juu juu kwamba ni regulatory agency na sioni kitu kibaya kwa regulatory agency software kutengenezwa na business lawyer!
3. Navyomjua Nyaga ni Business lawyer hivyo anafanya mikataba ya wekezaji na kusaidia wawekezaji ku sign mikataba hivyo hao wazungu unaosema ni watega wake na anafnya kazi kama lawyer mwingine yeyote. Ni vigumu kupigina chenga na utapeli unapotaka kufanya biashara bongo hata mimi binafsi namtafuta Nyaga anisaidie kwenye biashara zangu mpya nataka kufanya bongo. Mimi kwenda bongo kufanya shuhuli kama ya kufungua kampuni itanichukua wiki tatu hadi nne wakati nikitumia lawyer ni siku kumi tu. Hivyo tuache maneno ya kwamba kama mtu ukifanya biashara wa wawekezaji basi wewe ni fisadi!.
Biashara si ufisadi na kama umefanya kiwazi basi tuangalie je sofware inafanya nini kwbla ya ushabiki
 
Mimi si mtetei Nyaga lakini naeleza ukweli tu ninavyojua mimi

1. Software: Si kitu cha kirahisi tu ni lazima ujue ni software gani na inafanya nini mafano software ya MPESA inathamani gani? hivyo ni vigumu kujua na kama si sofware nzuri basi wasinunue. Kitu kimoja tu ambacho sijakipenda ni kwamba kwa kampuni kununua sofware ni lazima wajue support kama ipo maana sofware zinahitaji development na zinaweza kuwa na hitilafu.
2. Pili mimi siko bongo hivyo hata sijui Brela ni nini lakini najua unaweza kuuza sofware kwa zaidi ya $1 million. Nimesoma kwa juu juu kwamba ni regulatory agency na sioni kitu kibaya kwa regulatory agency software kutengenezwa na business lawyer!
3. Navyomjua Nyaga ni Business lawyer hivyo anafanya mikataba ya wekezaji na kusaidia wawekezaji ku sign mikataba hivyo hao wazungu unaosema ni watega wake na anafnya kazi kama lawyer mwingine yeyote. Ni vigumu kupigina chenga na utapeli unapotaka kufanya biashara bongo hata mimi binafsi namtafuta Nyaga anisaidie kwenye biashara zangu mpya nataka kufanya bongo. Mimi kwenda bongo kufanya shuhuli kama ya kufungua kampuni itanichukua wiki tatu hadi nne wakati nikitumia lawyer ni siku kumi tu. Hivyo tuache maneno ya kwamba kama mtu ukifanya biashara wa wawekezaji basi wewe ni fisadi!.
Biashara si ufisadi na kama umefanya kiwazi basi tuangalie je sofware inafanya nini kwbla ya ushabiki
unamtetea, acha kufanya watu wajinga
 
tuWanabodi hata mimi namfahamu vizuri huyu kijana Nyaga Mawalla.

Kitu ambacho nataka mfahamu jamaa ni Genius!. Ni genuine genius katika fani ya sheria.

Nilimtangulia madarasa kibao Ilboru alikuwa ni kichwa cha ukweli kama sikosei jamaa atakuwa ametoka na poiti 7 O-Level na point 3 A-Level.

Alijiunga UD kuchukua sheria nilimuona akichangia kile kipindi cha 'Kiti Moto' alishuka na nondo za kufa mtu nikazidi kuthibitisha ni kichwa mbaya!.

Mimi nilisoma kitu kingine kabla sijatua UD kufanya sheria. Japo kusoma sheria chuo chochote humu nchini unapata digrii yako yako ya sheria yenye hadhi sawa, lakini wanaosomea UD wanateseka zaidi, kwanza wanaipiga kwa miaka 4 wakati wenzao ni miaka mitatu tuu. Cha pili UD hakuna kupata Ist class wakati vyuo vingine ni Ist class za kumwaga.

Moja ya matatizo makubwa kabisa ya kusoma sheria ni kukremu makesi zaidi ya 500 na kuwa na kumbukumbu rasmi ya majina na maudhui ya kesi hizo wenyewe wakiita sightation.

Sasa huyu Nyaga na mwanafunzi mwenzake mwingine akiitwa Baimu, walizukusanya kesi zote muhimu za kusomwa na wanafunzi wa sheria wa UD na kuzicompile pamoja katika bonge la mkitabu wakaliita 'BAIMU & MAWALLA'. Ukishalipata hilo buku, wewe sio lazima kwenda maktaba unless ni kwa information quest.

Ndipo kuna lecture mmoja akaniibia kuwa baada ya first class ya Prof. Asha Rose Migiro, Prof. Palamagamba Kabudi na Prof. Hamoud Majamba, Ist class nyingine ilikuwa iwe ni ya Nyaga Mawalla ili walimbania tuu na mpaka leo UD wabaendelea kubania hizo Ist Class!,

Sasa ninaposikia mambo anayofanya na hiyo fani yake ya sheria nazidi kumkubali.

Watanzania tuna tatizo na kukubali mafanikio ya wenzetu. Kwani Billy Gate alianzaje?. Hamuamini kuwa Nyaga ndio Billy Gate wa Tanzania?. Kama Billy Gate original amekuwa bilionea wa dunia kwa kugundua microsoft, kuna tatizo gani Nyaga kugundua hiyo program ya Brella?. Tena ikifanikiwa TRA watamtumia kuwatengenezea ile ya kuhakikisha kila mtu analipa kodi. Ile Asycuda++ haisaidii kitu?.
 
Back
Top Bottom