Uchaguzi 2020 Mawakala wa CHADEMA, ACT-Wazalendo, CUF na NCCR-Mageuzi wakamatwa baada kuzuia wapiga kura kuingia kituoni kwa madai ya wao kutopewa barua

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,501
9,280
TANGA: Mawakala wa CHADEMA, ACT-Wazalendo, CUF na NCCR-Mageuzi wakamatwa baada kuzuia wapiga kura kuingia kituoni kwa madai ya wao kutopewa barua

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Blasius Chatanda amesema baadhi ya mawakala wa vyama tofauti vya siasa wamekamatwa kwa madai ya kuzuia wananchi kupiga kura kwa kufunga milango.

Amesema walizuia wananchi kupiga kura kwa madai ya wao kutopewa barua za kuwatambulisha ili waruhusiwe kuingia kwenye vituo vya kupigia kura.

Kamanda Chatanda amesema mawakala hao ambao baadhi walizungumza na Mwananchi Digital kabla ya kukamatwa,walikuwa katika vituo vya Tongoni na Ofisi ya Mtendaji ya Kata ya Ngamiani Kusini .

"Ni kweli baadhi ya wafuasi wa vyama vya siasa tunawashikilia kwa mahoajino kwa sababu kulikuwa na kutoelewana kwenye vituo walivyokuwepo jambo ambalo lingeweza kuleta vurugu kama tungewaacha waendelee kuwepo kwenye maeneo hayo," amesema.

Hata hivyo amesema wapo ambao waliwaelewesha na kuwaachilia kutokana na kuonekana walikosa elimu na hivyo kushindwa kufuata utaratibu

Chanzo: Mwananchi
 
Mambo mengine ni ya ajabu sana sasa Wakala unaendaje Kituoni bila barua ivi kweli inaingia akilini? barua ndiyo inayokutambulisha kwa Msimamizi wa Kituo sasa kuzuia wananchi wasipige kura kisa eti huna barua its insanity Kituoni shughuli ni moja ya kupiga kura tu.
 
Siipendi CCM mimi mtu akiwa anaishabikia huwa namuona IQ yake ndogo sana na wala sina muda wa kujibishana nae. Nikifikiria tu nakatwa NSSF na mwajiri wangu ananiongezea halafu kuja kuipata pesa yangu napewa kidogo kidogo wakati tayari nimeshakatwa zaidi kodi kwenye mshahara wangu zaidi ya laki 1. Yaani kodi ni kubwa kuliko mafao yangu. Shame on you wewe hapo unayeshabikia upumbavu unaoitwa CCM
 
Napendekeza kama mgombea hana
wakala kura zake ziende kwa Jina la mgombea
wa kwanza kutokea katika karatasi l
a kupigia kura. Hatuwezi kuendekeza wagombea wazembe.
 
Siipendi ccm mimi mtu akiwa anaishabikia huwa namuona IQ yake ndogo sana na wala sina muda wa kujibishana nae. Nikifikiria tu nakatwa nssf na mwajiri wangu ananiongezea halafu kuja kuipata pesa yangu napewa kidogo kidogo wakati tayari nimeshakatwa zaidi kodi kwenye mshahara wangu zaidi ya laki 1. Yaani kodi ni kubwa kuliko mafao yangu. Shame on you wewe hapo unayeshabikia upumbavu unaoitwa ccm
Ni kweli, wengi wanaoipenda CCM hawana akili kabisa, ni midoli tu.
 
Mambo mengine ni ya ajabu sana sasa Wakala unaendaje Kituoni bila barua ivi kweli inaingia akilini? barua ndiyo inayokutambulisha kwa Msimamizi wa Kituo sasa kuzuia wananchi wasipige kura kisa eti huna barua its insanity Kituoni shughuli ni moja ya kupiga kura tu.
Wakati wa Udictator wa Idd Amini Dadaa kule Uganda waliokuwepo lakini wewe umevunja record.
 
Ni kweli, wengi wanaoipenda CCM hawana akili kabisa, ni midoli tu.
Yaan wapo kama misukule. Wiki iliyopita nilikua naumwa nimeenda hospital huwezi amini naambiwa hizi dawa zimetolewa kwenye bima unatakiwa ununue cash. Niliishiwa nguvu hadi machozi yalikua yananilenga wakati hapo nyuma hizo dawa nilikua napata. Halafu mtu anakwambia chagua ccm...ccm my foot
 
TANGA: Mawakala wa CHADEMA, ACT-Wazalendo, CUF na NCCR-Mageuzi wakamatwa baada kuzuia wapiga kura kuingia kituoni kwa madai ya wao kutopewa barua

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Blasius Chatanda amesema baadhi ya mawakala wa vyama tofauti vya siasa wamekamatwa kwa madai ya kuzuia wananchi kupiga kura kwa kufunga milango.

Amesema walizuia wananchi kupiga kura kwa madai ya wao kutopewa barua za kuwatambulisha ili waruhusiwe kuingia kwenye vituo vya kupigia kura.

Kamanda Chatanda amesema mawakala hao ambao baadhi walizungumza na Mwananchi Digital kabla ya kukamatwa,walikuwa katika vituo vya Tongoni na Ofisi ya Mtendaji ya Kata ya Ngamiani Kusini .

"Ni kweli baadhi ya wafuasi wa vyama vya siasa tunawashikilia kwa mahoajino kwa sababu kulikuwa na kutoelewana kwenye vituo walivyokuwepo jambo ambalo lingeweza kuleta vurugu kama tungewaacha waendelee kuwepo kwenye maeneo hayo," amesema.

Hata hivyo amesema wapo ambao waliwaelewesha na kuwaachilia kutokana na kuonekana walikosa elimu na hivyo kushindwa kufuata utaratibu

Chanzo: Mwananchi
Hali Kama hii ilikuwa it ok kule Moshi mjini,ila hekima na busara za RPC Kilimanjaro zilimuokoa DED Moshi mjini kutokupigwa na mawakala
 
Ni kweli, wengi wanaoipenda CCM hawana akili kabisa, ni midoli tu.
Lakini mtu ukiongea tu hivi atabisha.. kuna mtu kanambia mpigie CCM kura urahisi nikamwambia nipe sababu tatu kashindwa kunipa..huwezi ukanambia eti madaraja barabara na ndege hivo vitu vilitakiwa viwepo since hata hajafikiriwa kua rais na hata kama asingeleta yeye hata mwengine huko angeleta ... ndio wajibu.... nimemuulza unajua kwenye kodi za biashara kwamba kuna kitu kinaitwa service levy bonge la kodi ambalo ni jipya na halina explanation yakueleweka unajua ni wafanya biashara wangap wamelalamika

watu wanaongea ongea coz wapo wapo tu wana judge kwa cover .. dig deep ingia kwenye wakandamizwaji ndio utaona
 
Back
Top Bottom