PM Majaliwa: CHADEMA, ACT Wazalendo, NCCR, CUF, CCM na DP vimepokea jumla ya Tsh 17.5 bilioni ikiwa ni Ruzuku

johnthebaptist

JF-Expert Member
May 27, 2014
83,728
141,592
Waziri mkuu mh Majaliwa amesema Vyama 6 vya Siasa vyenye Sifa ya kupata Ruzuku ya Serikali vimepokea Jumla ya tsh 17.5 bilioni

Vyama hivyo sita ni Chadema, ACT wazalendo, NCCR mageuzi, CUF, CCM na DP

Chanzo: Swahili Times

Nawatakia Juma Takatifu Lenye Baraka tele!

---
Katika bajeti ya 2022/23, Serikali imetoa ruzuku ya Sh17 bilioni kwa vyama sita vya siasa vyenye sifa za kupewa ruzuku.

Vyama hivyo ni CCM, Chadema, NCCR- Mageuzi, ACT Wazalendo DP na CUF na kwamba itaendelea kufanya hivyo ikiwa ni takwa la kisheria.

Kauli hiyo imetolewa bungeni leo Jumatano Aprili 5, 2023 na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa wakati akisoma hotuba ya Makadilio ya Mapato na matumizi kwa Ofisi na Wizara zilizo chini yake

Kwa kauli hiyo, ni dhahiri kuwa imehitimisha minong'ono ya Chadema kuwa hawajachukua ruzuku kutoka Serikali.

Kwa muda sasa kumekuwa na mjadala kwenye mitandao ya kijamii kuhusu Chadema ambao walishakaririwa mara kadhaa wakisema hawachukui ruzuku ingawa siku za hivi karibuni wamekuwa kimya kuhusu jambo hili.

Waziri Mkuu hakusema vyama hivyo kila kimoja kimechukua kiasi gani cha fedha kwa wakati huu.

Waziri Mkuu amesema demokrasia imeendelea kuimarika nchini ikiwemo uhuru wa vyama vya siasa na nyombo vya habari katika kujenga nchi yao.


MWANANCHI
 
Waziri mkuu mh Majaliwa amesema Vyama 6 vya Siasa vyenye Sifa ya kupata Ruzuku ya Serikali vimepokea Jumla ya tsh 17.5 bilioni

Vyama hivyo sita ni Chadema, ACT wazalendo, NCCR mageuzi, CUF, CCM na DP

Source: Swahili Times

Nawatakia Juma Takatifu Lenye Baraka tele!
Isijekuwa zimeingizwa kwenye akaunti tu kama alivyofanya fei toto kuweka pesa kwenye akaunti ya yanga
 
Waziri mkuu mh Majaliwa amesema Vyama 6 vya Siasa vyenye Sifa ya kupata Ruzuku ya Serikali vimepokea Jumla ya tsh 17.5 bilioni

Vyama hivyo sita ni Chadema, ACT wazalendo, NCCR mageuzi, CUF, CCM na DP

Source: Swahili Times

Nawatakia Juma Takatifu Lenye Baraka tele!
Ruzuku ni haki yao ipo kikatiba kabisa shida ni hiyo ruzuku kuwafunga midomo wakati ni haki yao

USSR
 
Dodoma. Katika bajeti ya 2022/23, Serikali imetoa ruzuku ya Sh17 bilioni kwa vyama sita vya siasa vyenye sifa za kupewa ruzuku.

Vyama hivyo ni CCM, Chadema, NCCR- Mageuzi, ACT Wazalendo DP na CUF na kwamba itaendelea kufanya hivyo ikiwa ni takwa la kisheria.

Kauli hiyo imetolewa bungeni leo Jumatano Aprili 5, 2023 na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa wakati akisoma hotuba ya Makadilio ya Mapato na matumizi kwa Ofisi na Wizara zilizo chini yake

Kwa kauli hiyo, ni dhahiri kuwa imehitimisha minong'ono ya Chadema kuwa hawajachukua ruzuku kutoka Serikali.

Kwa muda sasa kumekuwa na mjadala kwenye mitandao ya kijamii kuhusu Chadema ambao walishakaririwa mara kadhaa wakisema hawachukui ruzuku ingawa siku za hivi karibuni wamekuwa kimya kuhusu jambo hili.

Waziri Mkuu hakusema vyama hivyo kila kimoja kimechukua kiasi gani cha fedha kwa wakati huu.

Waziri Mkuu amesema demokrasia imeendelea kuimarika nchini ikiwemo uhuru wa vyama vya siasa na nyombo vya habari katika kujenga nchi yao.

MWANANCHI
 
Serikali ya Rais Samia Suluhu imetoa ruzuku jumla ya Tsh Bilioni 17.5 kwa vyama vya siasa sita vyenye sifa ya kupata ruzuku.

Vyama vinavyonufaika na Ruzuku hiyo ni NCCR-Mageuzi, CCM, CHADEMA, DP, CUF na ACT- Wazalendo.

Chadema walikataa kupokea ruzuku wakidai kuwa hawakuukubali uchaguzi wa 2020 lakini baada ya kupokea ruzuku hii wanathibitisha uchaguzii haukua batili

Hongera sana Rais Samia Suluhu kwa kuimarisha democrasia nchini pamoja na kufanikisha siasa za kistaarabu lakini pia umefanikisha umoja wa kitaifa hakika Mama unaupiga mwingi kila sekta

Fs8sKPtWwAEcoUG
 
Serikali ya Rais Samia Suluhu imetoa ruzuku jumla ya Tsh Bilioni 17.5 kwa vyama vya siasa sita vyenye sifa ya kupata ruzuku.

Vyama vinavyonufaika na Ruzuku hiyo ni NCCR-Mageuzi, CCM, CHADEMA, DP, CUF na ACT- Wazalendo.

Chadema walikataa kupokea ruzuku wakidai kuwa hawakuukubali uchaguzi wa 2020 lakini baada ya kupokea ruzuku hii wanathibitisha uchaguzii haukua batili

Hongera sana Rais Samia Suluhu kwa kuimarisha democrasia nchini pamoja na kufanikisha siasa za kistaarabu lakini pia umefanikisha umoja wa kitaifa hakika Mama unaupiga mwingi kila sekta

Fs8sKPtWwAEcoUG
Mama Yuko vzuri anapiga chenga hatari hata ukiwa na makengeza unalambwa tu chenga
 
Mama Yuko vzuri anapiga chenga hatari hata ukiwa na makengeza unalambwa tu chenga
Mama haachi gepu yani Ukilinganisha upinzani wa sasa na miaka 5 iliyopita aisee utagundua Mama amefanya kazi kubwa sana ya kuondoa uhasama wa kisiasa kupitia maridhiano
 
Wabunge 19 haramu.

Ruzuku inayotokana na wabunge 19 halali wanaitafuna.

Waoza meno asili yao ni ujambazi.
 
Unajua maana ya maridhiano wewe??
Imekuwa SHIELD ya kupokea ruzuku😂

Kwani baada jembe kufariki, ulifanyika uchaguzi mwingine? Maana tunaambiwa ulikuwa batili na wale 19 seats batili lakini ruzuku tunachukua
 
Katika issue ya maridhiano ni nipe nikupe ikiwa na maana ukitaka reconciliation na mtesi wako lazima uwe tayari kuachana na perception uliyokuwa nayo ili naye akupatie kile ukitakacho.Shida ninayoijua kwa maconservative walio kwenye jukwaa hili si ruzuku ambayo CHADEMA wameanza kuichukua ila ni kiu yao ya siasa za uhasama kama zile za enzi za mzilankende zilizowafanya chadema waishi kama digidigi mbele ya chui wenye njaa.Na siasa zile za kibabe zilisecure vyeo vyao wakati wa uchaguzi tofauti na Mh Samia anayetaka kila mtu ashinde kwa ushawishi wake na si nguvu ya vyombo vya dola wakiwemo polisi wetu
 
Back
Top Bottom