katika mahusiano yote niliyopitia nilikuwa nikiponzwa na Upole na Ile Hali ya kumuamini mtu kupita Uwezo. Kipindi nipo CBE niliingia katika Mahusiano na Binti mmoja ambaye nilikuwa nikimpenda na Kumthamini kuliko Hata Mama Yangu Mzazi..
Kila alichokuwa Akinieleza nilikuwa nikikubali na kuamini.. Nilimuonyesha kila aina Ya mapenzi, nilimuonyesha ni Jinsi gani Mwanamke Anatakiwa kupendwa... Alikuwa Huru kushika na Kuangalia Chochote.. Iwe Simu; lap top na Vingine vingine kibao. Na hata Yeye alinipa Uhuru Huo kitu Ambacho kiliongeza Upendo Wangu kwake.
Kumbe nilikuwa nikifanywa Mjinga, Mpumbavu na Limbukeni.. Kumbe wakati nikiamini nipo mimi kama mimi kumbe mwenzangu Alikuwa na Mtu wa Pembeni. Na ili mimi nisigundue Akanunua Simu ambayo Ilikuwa Akiificha na kuchati na watu wake akiwa kwao ama mbali na Wewe.
MUNGU hakutaka kumficha mnafiki, Mungu hakutaka niendelee kudanganywa. Ilikuwa Siku ambayo nilikuwa katika Maandalizi Ya Semister nikiwa Nimejiinamia Simu Yangu Ikaingia Sms Upande Wa WhatsAp... Sijui ni kitu gani kilinipata lakini Nilijikuta nikiogopa kuifungua Ile Sms.. Wakati Nikiendelea kujifikiria zikaanza kuingia sms Mfululizo nikaona Bora Nizisome....
Nikaifungua Sms Ya kwanza Ambayo Ilionekana kutumwa na Namba Ngeni.... Hapo nikakutana na Picha Ya mwanamke niliyempenda Akiwa Uchi tena Huku Amekumbatiwa kwa nyuma.. Sijawahi kuumia, kulia kama Nilivyoumia Siku Hiyo..
Bahati Mbaya Nikaharibu Masomo Yangu.. Ibrah Nikadisco na Hata niliporudia mwaka bado nikaangukia pua.. Ingawa ni Mtu Mwenye jina kwasasa Lakini Namchukia mpaka naingia kaburini