Meko Junior
Senior Member
- Mar 23, 2018
- 159
- 362
Kisa cha pili
Mauaji Mbezi Siku ya uzinduzi wa nyumba
Jamaa mmoia mwenyeji wa Moshi kwa akina Mamndenyi mtani wangu na Asprin babu kijana.. Huyu mwana alipiga dili ndefu na wenzake ila kwenye mgao akawazima wenzake akasepa na mzigo wote akapotea mazima..
Akaibukia Mbezi akanunua kiwanja akajenga nyumba nzuri kubwa ya kisasa kwa ile pesa ya dili aliyodhulumu wenzake! Akaandaa na sherehe ya kuizindua siku ya Jumapili.. Akamualika mama yake mzazi toka Moshi na ndugu na jamaa na marafiki wengine
Siku ya uzinduzi asubuhi ile ya Jumapili watu wengine wakiws wameenda kanisani, wengine waliobaki nyumbani wakiandaa vyakula nk.. Mama mzazi akawa yuko sebuleni anaangalia TV jamaa kalala ndani
Walifika watu watatu rika la mwanae wakaingia mpaka sebuleni na kumsalimia mama kwa heshima zote kisha wakamuulizia jamaa
Mama mzazi akidhani ni wageni waalikwa akamuita mwanae! Jamaa akatoka ndani akiwa na uchovu mwingi.. Ghafla uso kwa uso anakutana na wale jamaa zake aliowapiga
Jamaa bila kupoteza muda wakamwambia mama yake kwamba kilichowaleta pale ni roho ya mtoto wake! Jamaa akajaribu kuwaomba wasimdhuru atawapatia chao, lakini wakamwambia siku hiyo hawakuhitaji hela tena bali roho yake tuu..
Akala risasi tatu akafa palepale jamaa wakasepa bila kuchukua hata sindano..! Walioenda kanisani na wageni waalikwa wengine walikuta msiba badala ya sherehe za uzinduzi wa nyumba
Soma Mw.4:8 - 13.Lost books from Bible,
Google hiyo, utaona na kujua mengi kuhusu Adam .
Waliamua kuyaficha
[emoji22]Mauaji ya visasi (kulipa kisasi) ni dhambi ya tatu kuzaliwa duniani
Dhambi ya kwanza ngono na usaliti pale Eden, lakini hii ina mazonge mengi kwakuwa uongo na kutotii maagizo vyote vinaingia hapo! Ni dhambi yenye vipengele A, B C na D
Dhambi ya tatu ni mauaji, ambayo asili yake ni choyo na wivu, pale Kaini alipofanya uchoyo wa kutoa sadaka iliyonona na matokeo yake ikakataliwa.. Ya mdogo wake Abel ilipokelewa na ndipo roho ya chuki ilipomuingia Kaini na kuamua kumuua mdogo wake kwa mama. Adam hakuwa babayake wa damu.
Tangu hapo mkeka wa mauaji ya visasi uliasisiwa ulimwenguni.. Tangia hapo maelfu kwa maelfu wameuawa kwa mauaji ya visasi. Nimekisoma kisa cha kijana wa Songwe aliyeuwawa mbele ya mkewe na mwanae na wauaji wakaondoka bila kuchukua chochote! Visa hivi ni vingi mno na nitasimulia baadhi kadiri ya kumbukumbu zangu, nakukaribisha nawe uungane nami kama kuna chako unakikumbuka!
Maisha haya hutukutanisha na wengi lakini pia na mengi, kuna watu kwa sababu zozote zile wanajiona ya kwamba wao ndio wao na wengine si kitu.
Wao ndio wanastahili kupata
Wao ndio wanastahili maisha mazuri
Wao ndio wanaijua pesa kuliko wengine
Wao ndio wanastahili maisha na vitu vizuri kuliko wengine
Visa hivi vya mauaji ya visasi vina asili moja! Wauaji hawachukui chochote! Visa hivi vyanzo vyake ni
Usaliti wa kibiashara/dili
Usaliti kwenye mapenzi/mahusiano
Harakati za kisiasa na madaraka
Wivu wa maendeleo/kupata kwa wengine
Dhuluma
Utemi
Ubabe nk nk
Kwenye hili kuna wauaji wa kukodi ama baadhi hutekeleza mauaji wenyewe tena kwa taarifa kabla ya kutekeleza mauaji.
Sometimes kwenye haya mambo ukishindwa kusamehe lipa kisasi! Haikuongezei kitu lakini inakupunguzia maumivu! Ila usiijaribu hii njia imejaa mabaya!
Mnamkumbuka yule traffic aliyeuliwa kwa risasi pale sayansi ? Jamaa alikuja na boda akamuuliza Afande unanikumbuka? Jamaa akajibu ndio.
Jibu hilo lilitosha kummininia risasi zilizoondoka na uhai wake
Nitakuja na visa vingine.
Mkuu, inapendeza pale ambapo hujaelewa jambo UULIZE usikae kimya halafu ukajiridhisha kwamba ni magumashi. Nakushauri nenda Chapel na uwaulize maswali hao utakaokuwa unawasikiliza. Chukua muda wako japo dk chache sio masaa pitapita kwenye maandiko.😳😳😳😳.. me ndio maana nimeacha kwenda Chapel... Mambo ya magumashi ni mengi mno.
Nyoka aligegeda mtuKuchapiwa ni siri ya ndani na ilianzia pale Eden.. Wewe unadhani baada ya Eva kuongopewa na ibilisi(nyoka) na kula 'tunda' la mti wa kati alitoka salama? Adam alikula makombo tuuu...
Kaini ni uzao wa ibilisi na ndio maana hakuona umuhimu wa kutoa sadaka nzuri..
Dhambi ya tatu ni mauaji, ambayo asili yake ni choyo na wivu, pale Kaini alipofanya uchoyo wa kutoa sadaka iliyonona na matokeo yake ikakataliwa.. Ya mdogo wake Abel ilipokelewa na ndipo roho ya chuki ilipomuingia Kaini na kuamua kumuua mdogo wake kwa mama. Adam hakuwa babayake wa damu.
zitto junior pitia hapa.Kaini siyo mtoto wa Adam ?
kaka ambiere, unashaurije kuhusu kulipa kisasi?je tumuachie MUNGU kama bible inavyosema kwetu wakristo?au tumalizaane na wabaya wetu tu wenyewe!maaana unafanyiwa mambo yenye kuumiza sana mpaka unakua na uchungu mwingi kiasi kwamba unatamani kulipiza ili uchungu uondoke!ila dini ndo zinatuzuia tuu!yaani aiseee
19Vitaje..[emoji38]
Mmmmhh rudi kwenye uganga wa kienyeji sasa. Huku utatuia kwenye dhambi bure.Kuchapiwa ni siri ya ndani na ilianzia pale Eden.. Wewe unadhani baada ya Eva kuongopewa na ibilisi(nyoka) na kula 'tunda' la mti wa kati alitoka salama? Adam alikula makombo tuuu...
Kaini ni uzao wa ibilisi na ndio maana hakuona umuhimu wa kutoa sadaka nzuri..
Dah mbaya sana hii poleni sana mkuuNdio kwanza natoka msibani...na bila shaka nitausindikiza msiba mpaka kaskazin... yes visas...na kisa kipo hivi...
Ilikuwa siku ya jumapili usiku nipo pub flan napiga kilaji huku nasubiria vitasa vya mandonga...akatokea dogolas yupo na rafiki yake...wakanipa hi thn wakajongea kwenye meza yao na nikamuita muhudum nikamwambia wasikilize wale...basi akawasikiliza nikawaanzishia vinywaji vya kama 25,000 hivi...na mim nikawa na jamaa yangu tunazipasua bia na k vant..
Ilipofika mida ya saa tano usiku...nikawa nimechoka so nikaenda zangu lala...Asubuh ya jumatatu nasikia taarifa za msiba dada mmoja kauwawa na kubakwa..kudadis kumbe ni mke wa mdogo wangu sio wa damu lakin nimempita umri...
Jana nikaenda msiban na nikakutana na dogo na akaanza nisimulia kisa kilivyo tokea...
Nikamuuliza ilikuwaje..akaniambia pale ulinipo niacha..tulihama bar na kuhamia bar nyingine...ambayo hyo bar ipo karibu na kwao..sasa kuna jamaa alitokea na ni jiran yao na wamekua wote...akamwambia mwana amnunulie bia kwel dogo akamnunulia bia 2...mchiz akanywa akasepa kumbe mchiz ana jamaa yake hapo washapanga kuwa kwa kuwa dogo yupo hapa basi mkewe atakuwa nyumban peke yake so lazima akampige machine kwan anamtamanig muda mrefu...
Akamuacha jamaa yake pale amlie rada dogo yy akaenda nyumban kwa dogo akavunja mlango...akamkuta mke wa dogo na mtt kama wa miaka 7 wa kike...akamtia ngum mke wa dogo kumtoa wenge...akaanza kumkaba na kumvua ngoa sasa yule mke wa dogo ikasemekana akakosa pumzi ...jamaa akala mzigo mid kama ya saa tisa usiku
Kaka yake na dogo akawa anarudi gafla anakutana na mtu anatoka mbio...na anajigonga ukutan sasa yy akajua ni mwiz akaanza mkimbiza bila kujua mchiz kafanya unyama gan ndan...akamkimbiza sana lakin hakufanikiwa kumkamata lakin alimihis kama ni mtu fulan...hivyo akarud home akakuta umeme umekatika...sasa anaita shemej wala haitiki...akakutana na mtoto wa dogo...akamwambia mama kavamiwa na kaka fulan akawa anampiga...kwenda chumban anamkuta shemeji yake kama kazimia na damu nyingi kitandan...sasa nyumba yao ipo karibu na kituo cha polisi na hata hospital ya rufaaa ipo karibu na kwao...
Kaka mtu akambeba mtoto kwenda nae polis kutoa taarifa...huku nyuma dogo anarud nyumban...yupo na jamaa yake anakuta mazingira ambayo hayaelewi...anaingia chumban anakutana na mke wake hajielewi...anamtafuta mtt hamuon...ikabid ambebe mkewe kumpeleka hospital...mke anachukuliwa vipimo taarifa inatoka amefariki...jamaa anawaza kama wamemuua mke basi na mtt atakuwa wanemuua kupoteza ushahid...sasa daktar wakamwambia aende polis kureport tukio...anaenda polis anakutana na kaka yake pamoja na mtoto wake
Dogo anafika kituon anamwambia kaka yake wameniulia mke...kaka yake anamwambia hyo mtu nimekutana nae na nimemkimbiza...dogo akauliza amevaaje..akamwambia amevaa mabuti na kofia...dogo akavuta hisia na kumwambia kaka yake au ni muddy?? Kaka mtu akamwambia atakuwa ni yy caz alihis hicho kitu lakin hakuwa na uhakika
Wakatoka na defender pale mpaka eneo la tukio...polis wakachukua picha na mlangon kuna alama ya viatu alivyo kuwa anauvunja...
Wakaenda mpaka kwa kina muddy ni nyumba ya pili tu ni jiran sana..
Wakagonga na kuna mtu akafungua polis wakahoji muddy yupo jamaa akawa mbishi akapigwa rungu moja tuu...akasema muddy anakaa chumba cha tatu...polis dogo na kaka yake...wakagonga sana mlango bila mafanikio...ikabid wauvunje..muddy anaamka anajifanya ametoka usingizin na hajui lolote...
Polis wakamuhoji viatu vyako vipo wap...akawaonesha lakin baada ya upekuz zaid wakakuta ameficha lile buti...kwel ni yy..wakamwambia umechukua nn nyumba ya hapo jiran akatoa simu na suti...dogo anajua paswed ya mkew..kuiweka ikafunguka..pemben kulikuwa na shoka dogo akachukua akataka kumkata kata muddy na polis walimdhibit asifanye ivo..
Wakamchukua muddy kwa mahojiano zaidi...dogo analia tu muda wote...jana walimuhoji taarifa ya habari...kumuuliza kama walikuwa na bifu na muddy akanijibu hapana lakin kuna rafik yake muddy aliiba mtaani na dogo alimuona so alienda kureport polis na wakamueka ndan week mbili..na alivyotoka akamwambia dogo nitakuonesha...sasa ndio wakaungana na muddy kufanya malipiz...
Hahahah..shida sasa unatumia vitabu gani sijui. Bible tulio zoea ni tofauti na ya kwako.Nimestaafu hulk natarajia kuwa nabii
Uko sahihi watu hawajui biblia umeandikwa kwa mafumboKuchapiwa ni siri ya ndani na ilianzia pale Eden.. Wewe unadhani baada ya Eva kuongopewa na ibilisi(nyoka) na kula 'tunda' la mti wa kati alitoka salama? Adam alikula makombo tuuu...
Kaini ni uzao wa ibilisi na ndio maana hakuona umuhimu wa kutoa sadaka nzuri..