Matumizi ya simu katika Mahusiano

Matumizi ya simu katika Mahusiano

simu ya mkononi ni private,yeye yake mimi yangu,hata kama nikimpa asome si kigezo cha kuwa mwaminifu...so she dont touch my phone hata akitaka kumpigia mtu lazima aniombe..uaminifu aupimwi kwa sms..
 
ukiona mtu hataki cm yake iguswe na yake huyo, kama unajua haina sms mbaya kwa nini uikatalie. cm inapigwa utafikiri wewe ndo costumer care wa mitandao yote. afu eti cm yangu usiguse na mie yako sigusi, jiamin baba kuna lilojificha nyuma ya pazia ndo maana unakuwa mkali kwenye cm.
 
Wadau naleta kwenu,mada hii :ni Lipi jema katika mahusiano kati uhuru wa kutogusa simu ya mwenza wako (msg ) na hata ikiita na kuwa mnaweza kusomeana au kuchulia msg??maana naona mahusiano mengi yanavunjika sababu ya simu za mkononi!!nawakilisha

Mkuu kwa upande wangu naona uhuru wa kugusa simu au kutogusa simu ya mpenzi wako ni ngumu kujibu moja kwa moja maana inategemea sana na uelewa na makubaliano ya wapenzi husika.

Ktk hali ya kawaida, kwa watu wanaopendana na kuaminiana sioni tatizo kabisa mpenzi wangu akichukua simu na kusoma meseji, nimkataze kweni atakuta nini cha ajabu kama ni mtu ninayejiamini, kujiheshimu na kumheshimu yeye (Hapa nazungumzia mahusiano ya wawili)?

Kwa upande wa pili si jambo jema sana kama wote au mmoja wenu ni mtu wa utani na kutumiana meseji za utani hususani wa kimapenzi na rafiki zako wa zamani, kazini au majirani halafu mkaendekeza tabia ya kusomeana meseji. Hii inaweza kuleta hali ya kutokuelewa maana inaweza kusababisha ionekane kuwa una mpenzi mwingine au unacheat au ni muhuni. Na pia kuna sakata la kutumiwa meseji za kifamilia zaidi kutoka kwenu ambazo si nzuri mpenzi wako kuyafahamu matatizo ya ndani kabisa ya ukoo wenu mapema.

Kwa kuhitimisha, ni vizuri wahusika wenyewe (wapenzi) kukubaliana kama watakuwa wanasomeana meseji au laa lakini pia si vizuri ku-keep history ya meseji zilizopita ambazo unajuwa zinaweza kumkera mwenza wako akizisoma ili kuondoa mtafaruku unaoweza kuepukika kirahisi. Na zaidi ya hapo, kama unajijua umeamua kuwa na mpenzi wa kudumu au mke ni vyema ukajiheshimu na kupunguza utani na mawasiliano ambayo baadaye yanaweza kuja kukuvunjia mustakabali wa maisha yako ya ndoa hapo baadaye. Kama itatokea umetumiwa meseji ya aina hiyo, delete haraka na umuombe aliyetuma aache kukutumia aina hiyo ya meseji kama kweli wewe ni mtu uliyedhamiria kuyatunza mahusiano yako.

Thanks,
HP
 
ukiona mtu hataki cm yake iguswe na yake huyo, kama unajua haina sms mbaya kwa nini uikatalie. cm inapigwa utafikiri wewe ndo costumer care wa mitandao yote. afu eti cm yangu usiguse na mie yako sigusi, jiamin baba kuna lilojificha nyuma ya pazia ndo maana unakuwa mkali kwenye cm.

Siku hizi simu ni zaidi ya 'mawasiliano'...mbona zamani kulikuwa na simu za landline, ambazo kila mwanafamilia (achialia mbali wapenzi) walikuwa wako huru kuzijibu na hazikuleta matatizo yote haya tuyaonayo sasa? Kwani mtu huwezi tumia simu yako ya mkononi kama landline? Inawezekana...ila tumeshapita enzi zile, tuko kwenye era ambayo simu ni zaidi ya mawasiliano tu...simu ni diary, ofisi, safe yako ya kutunza siri/information zako za siri etc. Kubali kataa, hata kwa wanandoa, kuna mambo/vitu/siri zako ambazo hutaki mkeo/mumeo ajue..na si lazima siri hizo ni kuhusu usaliti wa kimapenzi. na siri hizo zinaweza zikafumuka kupitia kuchungulia chungulia simu za mwenzio na zikaharibu 'uhusiano wa kimapenzi'! Sasa juu ya nini kila mtu hasiwe na privacy yake...
 
Kama ni mke au mume ni haki yake kuwa huru kwa simu yako ila kama uko mwaminifu.
Kama hujiamini kwa maswala mbalimbali ndiyo utakuwa mchungu mwenzio kushika simu yako.
 
David ana mpenzi ambaye anampenzi ambao wana wapenzi je unaujua mtandao wako tulizanaaa
 
Kwangu mimi haiko shida....sina la kuficha, ukimpa uhuru mpenzi wako kusoma msg kama hakuna jambo la utata mwenyewe ataacha.

Yakishaanza mambo ya password and deleting messages hapo ndo unatafuta matatizo
 
Tatizo watanzania tunapenda saana siasa..
Jambo hata ambalo liko wazi tunaanza siasa..
Hapa kinachokosekana ni UAMINIFU tu..kama mnajiamini sioni kwa nini mnyimane na mzikumbatie simu zenu kwapani..
Baadhi wameweka hadi password..wengine hata bafuni waenda nazo..
UKWELI hutuweka HURU!..
 
uwiiii.....jana kuna mtu kachezea kichapo kutoka kwa mke wa mtu.....kisa simu....ilikuwaje.....
will be back shortly.....
 
Kama ni mke au mume ni haki yake kuwa huru kwa simu yako ila kama uko mwaminifu.
Kama hujiamini kwa maswala mbalimbali ndiyo utakuwa mchungu mwenzio kushika simu yako.

A certain level of privacy is a human right!! Haki hiyo hutolewa na mwenye nayo na si ya kuchukuliwa na mtu mwingine kwa sababu ya uhusiano wa aina hii au ile. Ndio maana utaona tofauti kati ya kumpa simu mtu mwingine na mke/mme au bf/gf!! Unaweza kuwa una uaminifu kwa mwenzi wako lakini bado kuna mambo kadhaa yako katika simu ambayo hutaki yajulikane kwa upande mwingine: Here are some challenges:

a) Je waweza kumpa mwenzi wako email accounts za watu WOTE unaowasiliana nao??
b) Je unaweza kumpa password yako mwenzi wako ya ATM card yako?
c) Unaweza kumpa passwords za accounts zako za online CV, facebook, twitter, emails (official and private).

Tuache utani, hayo mambo wengi hawafanyi si kwa sababu ya kukosa uaminifu. Ni kwa sababu ya KUJIKINGA na tusiyoyajua kutoka kwa hao wanatuzunguka.
 
Ukitaka uhusiano wako uingie matatani gusa simu ya mwenzio
Mkuu weka password utakuwa huru hata ukienda bafuni kuliko kubeba simu unapo enda chooni.
 
Siku hizi simu ni zaidi ya 'mawasiliano'...mbona zamani kulikuwa na simu za landline, ambazo kila mwanafamilia (achialia mbali wapenzi) walikuwa wako huru kuzijibu na hazikuleta matatizo yote haya tuyaonayo sasa? Kwani mtu huwezi tumia simu yako ya mkononi kama landline? Inawezekana...ila tumeshapita enzi zile, tuko kwenye era ambayo simu ni zaidi ya mawasiliano tu...simu ni diary, ofisi, safe yako ya kutunza siri/information zako za siri etc. Kubali kataa, hata kwa wanandoa, kuna mambo/vitu/siri zako ambazo hutaki mkeo/mumeo ajue..na si lazima siri hizo ni kuhusu usaliti wa kimapenzi. na siri hizo zinaweza zikafumuka kupitia kuchungulia chungulia simu za mwenzio na zikaharibu 'uhusiano wa kimapenzi'! Sasa juu ya nini kila mtu hasiwe na privacy yake...

You nailed it, mkuu!!!
Kama isivyo rahisi kwa sisi ku-share information zinazohusu online CV, facebook, twitter, ATM, emails (official & private) accounts, ndivyo inavopaswa kuwa vigumu kushare telephone number, names, sms zilizo kwenye simu!! Kama uaminifu unapimwa kwa mm kutoshare personal information, basi ni bora nisiitwe mwaminifu.

Nijuacho mimi ni kuwa information destroys/builds, kwa sababu ya kutojua gharama ya mm kushare any info - ndio maana ninachagua kutofanya "sharing".

Hebu tujipime katika mzani huu, ni wangapi kati yetu tunataka ku-share simu lakini hatutaki ku-share bank accounts, email and other accounts passwords? Kama ni swala la uaminifu na upendo, kuna vingi muhimu kuliko simu - mbona hatuvifanyi??
 
Mimi nimeona na kusikia sehemu nyingi sana wanaogombana wote sababu kubwa ni simu tu na kusomeana msg!ndio najiuliza kila siku ipi bora kati kutosomeana kabisa au kuwa wazi kwa simu ya mwenzako??(Wenye mahusiano au mke na mume)

Ivi siri na aibu kubwa ya binadamu si utupu/uchi? Lakini kwa nini unakuwa huru kuvua nguo zako mbele ya mkeo/mumeo? Mi nadhani huyo ni mtu ambaye unaweza kushare nae siri yako kubwa, so kwenye simu kuna siri gani ambayo hutaki mwenza wako aijue?
 
dr. mume na mke siri za nini?
kwa nini kuwe na siri kati yenu?




Siku hizi simu ni zaidi ya 'mawasiliano'...mbona zamani kulikuwa na simu za landline, ambazo kila mwanafamilia (achialia mbali wapenzi) walikuwa wako huru kuzijibu na hazikuleta matatizo yote haya tuyaonayo sasa? Kwani mtu huwezi tumia simu yako ya mkononi kama landline? Inawezekana...ila tumeshapita enzi zile, tuko kwenye era ambayo simu ni zaidi ya mawasiliano tu...simu ni diary, ofisi, safe yako ya kutunza siri/information zako za siri etc. Kubali kataa, hata kwa wanandoa, kuna mambo/vitu/siri zako ambazo hutaki mkeo/mumeo ajue..na si lazima siri hizo ni kuhusu usaliti wa kimapenzi. na siri hizo zinaweza zikafumuka kupitia kuchungulia chungulia simu za mwenzio na zikaharibu 'uhusiano wa kimapenzi'! Sasa juu ya nini kila mtu hasiwe na privacy yake...
 
hata mie nashangaa hizi siri za kutotaka mke/mume azijue...
kama anaona "sehemu zako za siri"
password ya atm, mpesa, tigo pesa, mnashare, hakuna ambacho mnafichana..... then simu inakuwa na siri...mmmmmmmh nashangaaa mie



Ivi siri na aibu kubwa ya binadamu si utupu/uchi? Lakini kwa nini unakuwa huru kuvua nguo zako mbele ya mkeo/mumeo? Mi nadhani huyo ni mtu ambaye unaweza kushare nae siri yako kubwa, so kwenye simu kuna siri gani ambayo hutaki mwenza wako aijue?
 
Ivi siri na aibu kubwa ya binadamu si utupu/uchi? Lakini kwa nini unakuwa huru kuvua nguo zako mbele ya mkeo/mumeo? Mi nadhani huyo ni mtu ambaye unaweza kushare nae siri yako kubwa, so kwenye simu kuna siri gani ambayo hutaki mwenza wako aijue?



ww acha kumdanganya mwenzio! ww mbona hufanyi hivyo?
 
Back
Top Bottom