Matumizi ya elfu kumi yangu leo

Matumizi ya elfu kumi yangu leo

Nataka nijue kipato chako kwa mwezi ndipo tufanye mahesabu. Kama ni biashara ukiuza 50000 kwa siku labda faida ni 15000 hakikisha usile zaidi ya nusu ya faida hapo utatoboa

Sent using Jamii Forums mobile app
Laki tano kwa mwezi, kuna kodi ya nyumba, kuna watoto wanasoma, kuna matumizi mengine km sabuni, mafuta,mavazi nk.
 
Nimeamka asubuhi nina elfu kumi mfukoni , sasa hesabu yake sasa :-
Chai kwa mama niwekee. 1,500/=
Nikatoka kwenda mjini nauli. 1,000/=
Nikala mchana huko mjini. 2,500/=
Nikanunua vocha 1,000/=
Nikanunua maji 600/=
Nimerudi nikanunua bando (MB) 1,000/=
Sasa nina chenchi 2,400/=
Nawaza kula cha jioni na maji pia ya kunywa.

Nitatoboa kweli???
Utatoboa ikiwa utaacha matumizi kwa vitu visivyo vya lazima kama chai badala yake kula chakula cha mchana mapema. Vocha sio lazima na badala yake mwenye shida na wewe atakutafuta yeye. Nauli sio matumizi ya lazima na badala yake utembee kwa miguu
 
Nimeamka asubuhi nina elfu kumi mfukoni , sasa hesabu yake sasa :-
Chai kwa mama niwekee. 1,500/=
Nikatoka kwenda mjini nauli. 1,000/=
Nikala mchana huko mjini. 2,500/=
Nikanunua vocha 1,000/=
Nikanunua maji 600/=
Nimerudi nikanunua bando (MB) 1,000/=
Sasa nina chenchi 2,400/=
Nawaza kula cha jioni na maji pia ya kunywa.

Nitatoboa kweli???
Sasa hapo unawaza nini? Piga wali ndondo 1000/- maji ya kandoro 1000/- hapo umebaki na nauli ya kwenda kwenye mishemishe.
 
Kama ni maji ya Moshi au Arusha sawa utakunywa ya bombani hata yakikaa mwezi mzima...

lakini haya ya Dsm utabeba Amoeba na typhoid tupu plus kemikali.
Mkuu kuna watu wanakunywa maji ya bombani Dar hii wengi sana!
 
Laki tano kwa mwezi, kuna kodi ya nyumba, kuna watoto wanasoma, kuna matumizi mengine km sabuni, mafuta,mavazi nk.
Kumbe unafamilia? Kunywa chai nyumbani. Beba kiporo kama lunch. Maji beba kutoka nyumbani kwenye chupa ya kilimanjaro. Dinner unakula nyumbani. Hapo matumizi yako ni nauli tu.
 
Mkuu kuna watu wanakunywa maji ya bombani Dar hii wengi sana!
Labda kwa sehemu chache, kuna mshkaji wangu hakuwahi kuishi huku juzi tu alikuja akakaa wiki 2, alikuwa hachemshi maji ya kunywa sasahv tayari ana Typhoid.
 
Back
Top Bottom