Matumizi ya elfu kumi yangu leo

Matumizi ya elfu kumi yangu leo

Nimeamka asubuhi nina elfu kumi mfukoni , sasa hesabu yake sasa :-
Chai kwa mama niwekee. 1,500/=
Nikatoka kwenda mjini nauli. 1,000/=
Nikala mchana huko mjini. 2,500/=
Nikanunua vocha 1,000/=
Nikanunua maji 600/=
Nimerudi nikanunua bando (MB) 1,000/=
Sasa nina chenchi 2,400/=
Nawaza kula cha jioni na maji pia ya kunywa.

Nitatoboa kweli???
Matumizi yako hayaendani na kipato chako.

1. Kwa nini upande basi kwenda mjini ? acha Anasa, tembea.
2. Kwa nini unywe maji ya chupa wakati ya bomba yapo bwerere? Anasa hizo
3. Kwa unywe chai asubuhi - acha Anasa
4. Kwa nini ule mchana? Anasa hizo.

Acha Anasa kijana, maana ungeokokoa Tshs. 5600, kwa hiyo ukijulisha na Tshs 2400 ungebakiwa na 7,000. Maisha mnayafanya yawe magumu ninyi wenyewe!! Poor Budgeting
 
Kama ni maji ya Moshi au Arusha sawa utakunywa ya bombani hata yakikaa mwezi mzima...

lakini haya ya Dsm utabeba Amoeba na typhoid tupu plus kemikali.
Hata Arusha maji sio mazuri, maji mazuri ya bomba ni Moshi.
 
Matumizi yako hayaendani na kipato chako.

1. Kwa nini upande basi kwenda mjini ? acha Anasa, tembea.
2. Kwa nini unywe maji ya chupa wakati ya bomba yapo bwerere? Anasa hizo
3. Kwa unywe chai asubuhi - acha Anasa
4. Kwa nini ule mchana? Anasa hizo.

Acha Anasa kijana, maana ungeokokoa Tshs. 5600, kwa hiyo ukijulisha na Tshs 2400 ungebakiwa na 7,000. Maisha mnayafanya yawe magumu ninyi wenyewe!! Poor Budgeting
Sawa mkuu, lakini kutoka Mbagala mpaka kariakoo kweli nitembee ? Ingekuwa Ubungo sawa, au kama kinondoni, au magomeni au buguruni sawa. Mbagala kweli mkuu, ?
 
Hata Arusha maji sio mazuri, maji mazuri ya bomba ni Moshi.
Unazungumzia Arusha chini labda.

Ila Arusha upande wote wa juu ya barabara kuu maji ni masafi. Yaani sekei, sanawari, mianzini, philips na ukanda wote wa juu ambapo source ya maji ni mlimani.
 
Sawa mkuu, lakini kutoka Mbagala mpaka kariakoo kweli nitembee ? Ingekuwa Ubungo sawa, au kama kinondoni, au magomeni au buguruni sawa. Mbagala kweli mkuu, ?
kaka kuna shida gani ukiamka saa 9 alfajiri, utafika town mapema tu hata ofisi yako haijafunguliwa - pia jioni fanya mazoezi - saa 11 ukitoka hadi saa moja moja jioni ushafika boda unaoga, unapiga ugali maharage unalala.
 
chai 100; andazi 100 ×2 = 200 jumla 300.

vocha : 1000

Lunch 1500 ( pilau) wali 1200; ugali nyama 1000;
maji unakunywa hapo hapo.

nauli 800.

dinner 1500; maji hapo hapo.

total 4800 ;

elfu 10 ni kwa siku mbili.
 
kaka kuna shida gani ukiamka saa 9 alfajiri, utafika town mapema tu hata ofisi yako haijafunguliwa - pia jioni fanya mazoezi - saa 11 ukitoka hadi saa moja moja jioni ushafika boda unaoga, unapiga ugali maharage unalala.
Hili zoezi ni zuri japo gumu. Zoezi zuri.
 
Ushauri wa bure,uwe unalala kutwa nzima ili kusave pesa,uwe unakula mlo wa usiku tu ambao ni 2,000 kwa hiyo utakuwa umesave 8,000/= kwa kila siku,huna haja ya bundle au maji pindi uwapo umelala.
Mjini mipango!!
Utumbo utajinyonga mkuu!utajikuta unatumia mamilion ya fedha kujitibu

Ova
 
Haha...hahaha

Chai ulitakiwa unywe 1000.
Nauli 1000
Mchana 2000
Maji bombani
Bando jiunge la chuo 1500 kwa wiki
Jumla 5500 unabaki na 4500 ukijumlisha na 1500 za bando za week nzima utakuwa na zaidi ya 5000 ukiwa bado haujala usiku.
bando la 1500 kwa wiki nahisi halimtoshi. ila ushauri mzuri
 
Nimeamka asubuhi nina elfu kumi mfukoni , sasa hesabu yake sasa :-
Chai kwa mama niwekee. 1,500/=
Nikatoka kwenda mjini nauli. 1,000/=
Nikala mchana huko mjini. 2,500/=
Nikanunua vocha 1,000/=
Nikanunua maji 600/=
Nimerudi nikanunua bando (MB) 1,000/=
Sasa nina chenchi 2,400/=
Nawaza kula cha jioni na maji pia ya kunywa.

Nitatoboa kweli???
Matumizi yako 50% sio ya msingi, ulitakiwa uchague chai au mlo wa mchana, pia bando nunue 1500 ya week ( university offer) hapo utaokoa 5500/-kwa wiki kwenye airtime&bundle.
 
Unazungumzia Arusha chini labda.

Ila Arusha upande wote wa juu ya barabara kuu maji ni masafi. Yaani sekei, sanawari, mianzini, philips na ukanda wote wa juu ambapo source ya maji ni mlimani.
Inawezekana, chini ya barabara kuu ni kimbembe, maji sio masafi kabisa. Ila Moshi ni kama ulaya, unakunywa maji ya bomba. Ndio maana katika miji yote Tanzania, Moshi is my favourite.
 
chai 100; andazi 100 ×2 = 200 jumla 300.

vocha : 1000

Lunch 1500 ( pilau) wali 1200; ugali nyama 1000;
maji unakunywa hapo hapo.

nauli 800.

dinner 1500; maji hapo hapo.

total 4800 ;

elfu 10 ni kwa siku mbili.
Muongo mkubwa wee!hata wee ukipewa hyo 10000 haikutoshi....
Alafu uzi huu umeonesha ni jinsi gani swala la mlo lilivyokuwa tatizo Kwa asilimia kubwa ya watz,mshahara wote unaishiaaa tumboni
Kweli ccm mtatuuaaa

Ova
 
Back
Top Bottom