Sir robby
JF-Expert Member
- Jun 22, 2022
- 2,400
- 4,074
Hakika hii Tanzania sasa imekuwa balaa. Serikali imekosa ubunifu kabisa wa vyanzo vya mapato. Haiwezekani kitu kimoja kilipiwe kodi au tozo mbili.
Hivi karibuni Serikali imekuja na tozo ambayo mweka fedha benki anakatwa kila anapotoa fedha ktk akaunti yake na benki nayo wakati huo huo inakata hakika huu ni wizi wa mchana.
Sababu kubwa ya haya matozo na kodi lukuki ni kutokana na matumizi makubwa yanayofanywa na Serikali. Matumizi hayo ni pamoja na:
1. Ununuzi wa magari ya kifahari kwa viongozi kuanzia ngazi ya wilaya wa chama na Serikali
2. Misafara mikubwa ya viongozi
3. Mishahara na posho kubwa ya wabunge halali na wale 19 wasio halali
4. Wizi mkubwa wa fedha za miradi za Serikali unaofanywa na watendaji na wakandarasi na wazabuni mbalimbali.
Ushauri kwa serikali
Ni vema serikali ikapunguza matumizi yake ili kuwapunguzia wananchi masikini zigo la kulipa kodi
Na tozo lukuki zilizowekwa na serikali.
Pia serikali iwachukulie hatua kali watu wote wanaoiba fedha zake ikibidi ifirisi mali zao ili kufidia wizi walioufanya. Pia serikali iangalie ukubwa wa mishahara ya wabunge kwani ni mikubwa sana na ukizingatia hawalipi kodi na pia kuwalipa mishahara wabunge fake 19 ni uhujumu uchumi wa fedha za umma.
Hivi karibuni Serikali imekuja na tozo ambayo mweka fedha benki anakatwa kila anapotoa fedha ktk akaunti yake na benki nayo wakati huo huo inakata hakika huu ni wizi wa mchana.
Sababu kubwa ya haya matozo na kodi lukuki ni kutokana na matumizi makubwa yanayofanywa na Serikali. Matumizi hayo ni pamoja na:
1. Ununuzi wa magari ya kifahari kwa viongozi kuanzia ngazi ya wilaya wa chama na Serikali
2. Misafara mikubwa ya viongozi
3. Mishahara na posho kubwa ya wabunge halali na wale 19 wasio halali
4. Wizi mkubwa wa fedha za miradi za Serikali unaofanywa na watendaji na wakandarasi na wazabuni mbalimbali.
Ushauri kwa serikali
Ni vema serikali ikapunguza matumizi yake ili kuwapunguzia wananchi masikini zigo la kulipa kodi
Na tozo lukuki zilizowekwa na serikali.
Pia serikali iwachukulie hatua kali watu wote wanaoiba fedha zake ikibidi ifirisi mali zao ili kufidia wizi walioufanya. Pia serikali iangalie ukubwa wa mishahara ya wabunge kwani ni mikubwa sana na ukizingatia hawalipi kodi na pia kuwalipa mishahara wabunge fake 19 ni uhujumu uchumi wa fedha za umma.