Matatizo ya Figo kuongezeka chanzo ni nini?

bulabo

JF-Expert Member
Aug 20, 2015
620
759
Heri ya mwaka mpya
Hii issue ya matatizo ya figo naiona kama imeongezeka sana mtaani baada ya ndugu yetu mmoja kuwa na hili tatizo...tulivyoaanza kwenda clinic ya kutoa maji imenistua kuona wagonjwa wengine vijana kabisa. Mawazo yenu wadau na watalaam chanzo nini hasa maana vijana wengi wanapiga mazoezi sana. Kuna daktari mmoja alinieleza tubadili mfumo wa kula kwa maana kama unakula wanga akadai tule mwisho saa saba mchana na usiku wa saa moja kamili tule vyakula vyepesi.
Tunashukuru Mungu mkapa hospital-dodoma wametusaidia. Tunaishukuru serikali kwa kuiweka hii hospital na kuwawezesha hawa madaktari bingwa maana hela ya kumpeleka india kubadili ilikuwa mtihani lakini Dodoma wanaweza na wamefanya kumbadilishia.

Naomba kuwakilisha
 
Samahani mkuu, spea mmeipata wapi? hongereni na tunamtakia mgonjwa afya imara zaidi.
 
Pia punguzeni kutumia madawa ya asili msiyoyaelewa elewa.

Mtu unakunywa madawa ya kuharisha ili upungue mwili,unaharisha siku 2 mfululizo non-stop(mpk maji yanaisha mwilini) na unadhani ni sifa?tena unakunywa hizo dawa kila baada ya miezi 3.

My friend in long run jiandae kwa figo yako kupata matatizo tu.

Alisikika mlevi mmoja akiongea wkt akitoka kilabuni.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Maji ndio chanzo kikubwa,
Yakiwa machache una zi overload nephron kufanya reabsorption as much as possible ili usipoteze hayo machache uliyonayo.

Yakiwa mengi pia, Zinazidiwa na maji hali inayofanya ishindwe kufanya reabsorption ya nutrients nyingine za muhimu..

Matokeo yake ni kutoa
Too concentrated/Too diruted Urine.
 
Ambacho sielewi ni

1. kwa nini mtu anakufa kwa kidney failure wakati wengine wanatoa mpaka figo moja na kubaki na moja. Ina maana wenye matatizo ni kwamba yamefeli yote mawili?

2. Kuna kupandikizwa figo. Watu maarufu na wenye hela kama marehemu Ruge alikosa wa kumuuzia au kumchangia figo ?

3. pia ipo njia ya kudili na ugonjwa kwa kutumia dialysis. Si tiba ya kidumu, na si rahisi kwenye gharama na haileti ahueni sana, lakini inarefusha maisha angalau. Again, samahani kutumia mfano wa mgonjwa maarufu na mpendwa wetu marehemu Ruge ambae ungedhani alikuwa na ways and means za kukabiliana na janga hili, kwa nini, kwa mfano, hakufanyiwa dialysis?
 
Maji ndio chanzo kikubwa,
Yakiwa machache una zi overload nephron kufanya reabsorption as much as possible ili usipoteze hayo machache uliyonayo.

Yakiwa mengi pia, Zinazidiwa na maji hali inayofanya ishindwe kufanya reabsorption ya nutrients nyingine za muhimu..

Matokeo yake ni kutoa
Too concentrated/Too diruted Urine.
Sasa tunywe maji kiasi gani tusinywe kiasi gani?

Fafanueni jamani!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
images-39.jpg
images-37.jpg
images-38.jpg
 
Link yako inasema tatizo ni nguruwe, kwa kiasi kikubwa.

Kwa hiyo Wamasai wako njema na ng'ombe na mbuzi zao. Tatizo Wachagga na nguruwe!
Red meat ni tatizo alichosema ni kuwa Marekani ulaji wao mkubwa ni nguruwe.
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom