Matapeli wa miaka ya 90's walikuwa balaa sana

Matapeli wa miaka ya 90's walikuwa balaa sana

2006 kuna machinga alipita mtaani kwetu anauza Radio na urembo urembo, pale mtaani kwetu Kuna kichochoro flan kimekaa kama mlango wa kuingia kwenye nyumba ya mtu.

Sasa muhuni mmoja kwenye mlango wa kile kichochoro akaweka pazia moja limechoka kiasi alaf akasimama kwa upande wa nje yule muuza radio alivyofika muhuni akamsimamisha akaelewana nae bei alaf akamwambia ngoja niingie ndan nikufatie hela akasogeza pazia akachoma ndichi.

Sasa machinga anashangaa masaa yanaenda mtu harudi alivyo choka akaamua kufununua lile pazia kuchungulia anashangaa anaona njia inatokea upande wa pili, kilicho tokea hapo ni kilio tu.
 
Hiyo nilikutana nayo karikoo hapo fourway 2006,jamaa kanibembeleza nikakubali bila kuuliza bei,baada ya kumaliza kubrashi nauliza bei naambiwa elfu nne na miasita,he,nikasema kulikoni ,eti kahesabu alivyokuwa anachovya hiyo kiwi,nililipa,Tangia siku hiyo nikajua hapo kariako wamejaa matapeli sio wabrashi viatu.siku hizi nikipita pale nikiwa na viatu vimechafuka Huwa wakiniita Huwa nawasonya tu napita zangu.
Mi alibrash kimoja,akanitajia Bei,nijamwambia sikupi,akasema nimrudishie dawa yake,nikamwambia afute kiwe Kama mwanzo au abrash na lingine,akabrash,nikampa Mia mbili
 
Dah umenikumbusha mbali sana miaka ya ,86 nipo darasa la nne enzi hizo alikuja jamaa mmoja hivi sijui ni kabila gani yule mwamba ila ndio hivyo alifanikisha

Ukampa?
 
Saiv wandugu utapeli umehamia kwenye makanisa uko kuna utapeli wakutisha na wanaotapeliwa uko kila uchao wanageuka kua mazuzu na hta ukimpa wazo la kujitoa uko anakuona ww ndyo shetani mwenyewe!
 
2006 kuna machinga alipita mtaani kwetu anauza Radio na urembo urembo, pale mtaani kwetu Kuna kichochoro flan kimekaa kama mlango wa kuingia kwenye nyumba ya mtu.

Sasa muhuni mmoja kwenye mlango wa kile kichochoro akaweka pazia moja limechoka kiasi alaf akasimama kwa upande wa nje yule muuza radio alivyofika muhuni akamsimamisha akaelewana nae bei alaf akamwambia ngoja niingie ndan nikufatie hela akasogeza pazia akachoma ndichi.

Sasa machinga anashangaa masaa yanaenda mtu harudi alivyo choka akaamua kufununua lile pazia kuchungulia anashangaa anaona njia inatokea upande wa pili, kilicho tokea hapo ni kilio tu.
Hivi niliwahi kushuhudia Muuza kuku.Mhuni kachagua majogoo makubwa 3, akamwambia amsubiri nje ya nyumba akachukue pesa, kumbe nyumba wala sio yake yule Msela, akaingia ndani akapitia mlango wa nyuma
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Bro wangu alitumwa mafuta ya taa akiwa na dumu la lita 5 na elfu 5 mkononi akakutana na mshkaji aliyemuambia jana Benki Kuu imeibiwa hivyo anapita mtaani kukagua noti.

Bro akakabidhi noti

[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
niko kwenye basi mbele yangu amekaa jamaa ana wasiwasi sana..

kufika njiani wakapanda jamaa wa3 wamebeba kamba ya kufungia mbuzi.

mojamoja kwa moja siti alipokaa yule jamaa na kuanza kumbeba bila kumpa hata muda wa kujitetea!!

jamaa mmoja kati ya wale wa3 kazi yake ni kuwatuliza abiria waliotaka kujua kitu gani kinaendelea!

jamaa alichokuwa anasema ni kwamba yule anaebebwa pale malaria imempanda kichwani na kutoroka hospitali..

kumbe jamaa alikuwa n pesa walienda kumkwangua zote kisha kumuacha.
 
Back
Top Bottom