Huwo mchezo nilichezewa, pale maeneo ya Tandale, kipindi kile Tandale ya Lumbesa.
Sikua na pesa, ila jamaa alifanikiwa kuondoka na kiredio changu, Ki philpis Dukani kilikua kinauzwa 700.
Ila na mimi sikua siku iendelee iwe mbaya kwangu, nikaenda pale karibu na ulipo msikiti, kutoka tandale sokoni kama unakuja Argentina, Zamani walikua wanashusha miwa pale.
Nikamtafuta mwenye njaa pale, nikamwelekeza akakubali kucheza. Yeye ndiye nilifanya ndiye, mdondosha burungutu, mimi mwokotaji. ili iwe rahisi kuelewesha kama nilivyo fanyiwa, mpaka mtu aingie.
Mtu wa kwanza kumwangushia, alikua mkulima alieleta mazao pale, kumbe jamaa mzigo bado ulikua kwa dalali haujauzwa, hivyo alikua mtupu nikaachana nae.
Wa pili mmachinga na nguo zake mkoni huyu alilia Tsh.3,000 pale uwanja wa fisi.