Matapeli wa Madini Mwenge, kuweni makini

Matapeli wa Madini Mwenge, kuweni makini

Status
Not open for further replies.
Pole sana Dada yangu.
Hivi inatokeaje unamkabidhi mtu vitu vyako vya Muhimu kama simu na vitu vingine?

Usiwe unapagawa ukitajiwa fedha nyingi za Bure. Wewe pita zako tu.
Wana dawa wale.
 
usiamini mtu haraka

hamna hela ya haraka haraka maisha haya
Kuwa macho Siku zote ukisikia mtu anasema ana Madini ujue ni Chain ya Matapeli. Ikiwezekana piga kelele ya mwizi wakamatwe utakuwa umesaidia wengi. Awe mzee, kijana, mchafu ni WEZI wanakuja na staili ya kuleta Wazee ili wasishtukiwe haraka. Shutka Ukisikia neno MADINI AU STAMICO AU MCHIMBAJI. Pole dada wenzako tulishalizwa siku hizi mtu akinisimamisha nisyemjua najiandaa kutapeliwa.
 
Kwa sasa sitapeliwi kizembe hivyo. Niliwahi kutapeliwa baiskeli ya shule mwaka 2001 nikiwa darasa la sita nikiwa Bukoba. Nilitapeliwa mazingira kama yako. Mwizi wangu nilikuja kukutana nae mubashara wilaya ya Karagwe mwaka huo huo, nilikuwa na bi mkubwa so nikamkaushia maana nilidanganya baiskeli iliibwa nikiwa shule basi nikachapwa za kutosha.
 
Matapeli wengi wa kupiga pesa ndefu huwa wanatumia mizizi. Ukijibu tu hata salamu(kuongea nao), umejiharibia mana kizizi kimeshanasa. Fahamu zitarudi umelizwa.
Ndio.nakumbuka wakati nauza hard ware.alikuja jamaa,na bodaboda ndo kamleta ilikuwa asubuhi.jamaa akatoa oda ya vitu vya laki sita.lakini wakati naongea nae nikachange ghafla.nikawa sielewi naongeleshwa nini,naitikia tu.giza giza.
Sasa jamaa kumbe target yake alikuwa anataka aibe boda boda.akasema pale hela hana wapi kuna tigo pesa.bodaboda akamjibu twende bunju.
Unaambiwa boda boda walikwenda kumuokotea mlimani city.kalala.hela hana.
Pikipiki imeibiwaa,
Kasoro hajaliwa tigo.na nguo kaachiwa.
 
utapeli wa zamani sana huo lakini bado kunawatu mnatapeliwa,mara nyingi unapokuwa town usipende mazoea na watu hovyohovyo ukiwa makini town unaona kila kitu wezi walivyo jiposition wachafuzi wa miji n.k
 
Sijui kwanini watu wengne wanakuwa na jazba.Anyway kwa wale ambao haijawatokea please kuweni makini.
Kuna siku nilikutana na matapeli wa aina hiyo Iringa nikiwa nimebeba zangu Ada ya Shule,mwanzoni nilikataa kama wewe lakini baada ya muda akatokea jamaa mmoja kavaa kinadhifu sana,baada ya kuongea mawili matatu,nikakubaliana naye kumsaidia huyo aliyejiita muuzaji wa madini kwa kumpeleka Bank,Bahati nzuri baada ya kutembea mita kama 30 hivi kuelekea Bank kuna hisia za hatari zikanijia,pale pale nika-make U-turn ya ajabu!Hawakuamini.


Hivi huwa wanamtambua vipu mtu mwenye pesa?
 
Kuwa macho Siku zote ukisikia mtu anasema ana Madini ujue ni Chain ya Matapeli. Ikiwezekana piga kelele ya mwizi wakamatwe utakuwa umesaidia wengi. Awe mzee, kijana, mchafu ni WEZI wanakuja na staili ya kuleta Wazee ili wasishtukiwe haraka. Shutka Ukisikia neno MADINI AU STAMICO AU MCHIMBAJI. Pole dada wenzako tulishalizwa siku hizi mtu akinisimamisha nisyemjua najiandaa kutapeliwa.



watanitapalije sasa madini nayajua kama sala in and out.
 
Pole sana.
Ila nimependa namna ulivyo muwazi na mkweli
kwenye swala la kutapeliwa maana tungekuwa kina sie
wa mjini tungesema " Kuna kisa nimesimuliwa na mwanamme wa dar...
Soma hapa uone mwanaume wa dar alivyo bwege".
 
Pole sana lkn ndiyo changamoto hizo, mimi wife aliibia 1ml na point something kwa stahili kama hiyo yako, tena yy alinipigia mm simu nikamuwekea hiyo pesa kwa account yake. Inaamana niliibiwa mimi. Hawa jamaa wanapenda kuibia wadada sana ni Mara chache kumkurupikia jinsia tofauti.
Pole sana but next time uwe makini.

Cc: Sakayo
 
Habari zenu wapendwa,

Jamani kilichonikuta jana, nilikua naelekea bank ndo kukutana na jamaa kachoka anajidai yeye mchimbaji mdgo mdgo kutoka Tanga anataka kubadilisha iwe Fedha nikamwambia simwelewi maana alikua anaongea haraka, ghafla akatokea mwanamke na jamaa akamsimasha na kuomba msaada uleule ndo yule mmama kusema dada umeshindwa kumsaidia nikwamwambia simwelew lakini yule jamaa akawa kaniganda eti mimi dada yake kisa kanisimamisha wa kwanza.

Sasa yule mama ndo kujifanya anaongea na padri ambaye huwa ananunua madini na kuwauzia Wachina. Sasa nikawambia si msaidiane but yule jamaa akawa kaniganda eti mimi dada yake na hamjui mtu mjini. Ghafla huyo padri kafika na dereva na kupima huyo mzigo kama uko sawa akaona ndiyo wakasema inabd tufungue account kwa jina langu kwasababu waliniuliza nilikua naenda bank kufanya nini nikawambia kufungua account ndo kujifanya tusaidie kufungua account tuwekee hzo mil.40 lkn inabidi tuwe na mil 2 ili kukamilisha.

Hapo jamaa akawa kashasema atanipa 3 million.Sasa hapo sielew chochote mara wakaomba simu zote na hela ili jamaa tusimtapeli.. (imagine) basi hela ikawa haijakamilika ndo kutoa jiwe moja sawasawa na mil.moja na nusu. Wakaniambia nishuke nitoe copy ya kitambulisho lakini nikawambia bank mbona photocopy machine ipo wakasema tunataka tukiingia bank tuharakishe zoezi.

Kutoka stationery sikuwaona wamechukua hela yangu na simu zangu mbili zote smartphone ndo kuulizia watu hapo Mwenge wakasema dada umeliwa. I was confused nikaenda Sonara kuwaonesa jiwe wakasema ni fake hiyo na huyo mdada kunisimulia story kama hizo nyingi tu kwasababu watu kila siku wanatapeliwa.

Wapendwa, kuweni makini sana mtu akikusimamisha na kukuongelesha sana na humwelewi usimjibu wanatumia dawa au muitie mwizi. And you kama unajijua ndo zako, may Fire Strike you.

Sasa hiyo namba yake niliisave kwenye line na line yangu ni BACKUP that means nikirenew naweza ipate. Je nikiipata nifanyaje?
Pole sana dada..
Ila haya mambo ya kitambo sana sema labda ulijisahau au huku wahi kupata hizi taarifa.
Nakupa pole tena
 
Matapeli wengi wa kupiga pesa ndefu huwa wanatumia mizizi. Ukijibu tu hata salamu(kuongea nao), umejiharibia mana kizizi kimeshanasa. Fahamu zitarudi umelizwa.
Kuna uwezekano unachosema ila sidhani.
Hawa jamaa kinacho wafanya wa wapate watu ni gear tu.
Gear atakayo ingia nayo usipostuka mapema basi umeenda. Au utapata usumbufu
 
Wewe unayajua wengine tunayaona kwenye TV. Nawaasa wasioyajua wasiwachekee wala kuwasikiliza hao wachimbaji na wauza madini Feki. Piga kelele mwizi ukisikia neno Madini kwa Stranger ni WEZI.




kweli kabsaa mara nyingi tamaa nda inawafanya wanatapeliwa. ni kuwa makini.

kama mtu hajui madini simshauri ajiingize kabsaa ataishia kulia.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom