Matapeli wa Madini Mwenge, kuweni makini

Status
Not open for further replies.

suzie _barbie

JF-Expert Member
May 2, 2017
1,523
3,073
Habari zenu wapendwa,

Jamani kilichonikuta jana, nilikua naelekea bank ndo kukutana na jamaa kachoka anajidai yeye mchimbaji mdgo mdgo kutoka Tanga anataka kubadilisha iwe Fedha nikamwambia simwelewi maana alikua anaongea haraka, ghafla akatokea mwanamke na jamaa akamsimasha na kuomba msaada uleule ndo yule mmama kusema dada umeshindwa kumsaidia nikwamwambia simwelew lakini yule jamaa akawa kaniganda eti mimi dada yake kisa kanisimamisha wa kwanza.

Sasa yule mama ndo kujifanya anaongea na padri ambaye huwa ananunua madini na kuwauzia Wachina. Sasa nikawambia si msaidiane but yule jamaa akawa kaniganda eti mimi dada yake na hamjui mtu mjini. Ghafla huyo padri kafika na dereva na kupima huyo mzigo kama uko sawa akaona ndiyo wakasema inabd tufungue account kwa jina langu kwasababu waliniuliza nilikua naenda bank kufanya nini nikawambia kufungua account ndo kujifanya tusaidie kufungua account tuwekee hzo mil.40 lkn inabidi tuwe na mil 2 ili kukamilisha.

Hapo jamaa akawa kashasema atanipa 3 million.Sasa hapo sielew chochote mara wakaomba simu zote na hela ili jamaa tusimtapeli.. (imagine) basi hela ikawa haijakamilika ndo kutoa jiwe moja sawasawa na mil.moja na nusu. Wakaniambia nishuke nitoe copy ya kitambulisho lakini nikawambia bank mbona photocopy machine ipo wakasema tunataka tukiingia bank tuharakishe zoezi.

Kutoka stationery sikuwaona wamechukua hela yangu na simu zangu mbili zote smartphone ndo kuulizia watu hapo Mwenge wakasema dada umeliwa. I was confused nikaenda Sonara kuwaonesa jiwe wakasema ni fake hiyo na huyo mdada kunisimulia story kama hizo nyingi tu kwasababu watu kila siku wanatapeliwa.

Wapendwa, kuweni makini sana mtu akikusimamisha na kukuongelesha sana na humwelewi usimjibu wanatumia dawa au muitie mwizi. And you kama unajijua ndo zako, may Fire Strike you.

Sasa hiyo namba yake niliisave kwenye line na line yangu ni BACKUP that means nikirenew naweza ipate. Je nikiipata nifanyaje?
 
Nimemkumbuka baba mmoja alitapeliwa 3Million kisa red mercury hapo Serena hotel

Dah unawakabidhi vipi watu usiowajua Mali kisha unaondoka na kuwaacha

Pole natumai watu wameshajifunza kupitia thread hii
 
Huna utaalamu wa madini unamsaidiaje mtaalamu wa madini???.
Pole ila ni ujingawako wakutokuwa na utaratibu wa kufikiri kwa kasi.
Haijakufikia that's why nilikataa mwanzoni Mpaka yule mdada alivyokuja ..yaani akili zimerud badae
 
Pole sana Dada yangu.
Hivi inatokeaje unamkabidhi mtu vitu vyako vya Muhimu kama simu na vitu vingine?

Usiwe unapagawa ukitajiwa fedha nyingi za Bure. Wewe pita zako tu.

Acha ' wamnyooshe ' Mkuu kwani kuna Watu wengine wanadhani Dar es Salaam ni kama huko Vijijini Kwao ' Mbwinde '.
 
Haijakufikia that's why nilikataa mwanzoni Mpaka yule mdada alivyokuja ..yaani akili zimerud badae
Inaonyesha unataka kusingizia uchawi, badala ya kuweka Alama ili yasikutokee tena.
Ninarudia pole ila ni ujinga wako, yakinitokea napiga kimya inakua fundisho kumkichwa. Unakua kama washabiki wa ccm wanadanganywa na kanga na kofia kwa mateso ya miaka mitano, huku wakiimba kwafuraha eti mbele kwa mbele??
 
Mambo mengine ni ya kujitakia, wala hakuna cha dawa wala nini. Kama ni dawa sijui uchawi tuambie unafanyaje kazi mpaka kweli ufanyiwe hivyo. Wale wezi wanatumia psychology kutokana na muonekano wa mtu, na jinsi anavyotembea, na kushangaa shangaa kila kitu anachokiona, na kutazama vitu vya kawaida kwa muda mrefu.

Askofu Dr Gwajima alishatoa ushauri wa kupiga selfie kwanza na kutuma instagram kabla ya kuendelea na shughuli nyingine.

Ushauri wangu, watu mnapokuwa na fedha nyingi na kuwepo barabarani mjitaidi kuwa wawili, halafu hakuna kuongea na mtu wala kupoteza muda wa kusimama simama.
 
huo wizi umeshamiri pia ubungo bus terminal, hasa kwa wale abiria wanaoingia na bus za usiku,..na wanapenda kumuokota mtu na kumpeleka ubungo plaza
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom