Matajiri wa Moshi miaka ya 90 hadi 2000's

Matajiri wa Moshi miaka ya 90 hadi 2000's

Na wanasema konda akichukua nauli siku hiyo anajua mzee.
Sijui alifunga cctv???😀😀😀
Kunakipindi konda aliingiwa na tamaa akachukua nauli, wamerudi ofisini Jamaa akamwambia akazitumbukize chooni mwenyewe.MZEE saivi mambo sio mazuri kivile japo anapambana kimtindo Ila saivi ni mwanamziki kazindua album juzi kati
 
Ibra alikuwa hataki gari zake (coaster) zikae foleni ya kilo kipindi hiyo. Basi kwa ubabe zikawa zikija tuu zinaingia mbele kabisa ndio zipakiwe.

Na ubabe huo akawa nao hadi mizani ya himo. Basi zake zikikuta foleni zinaenda piga pini gari ya mbele na kuunga moja kwa moja mizani. Hakuna kupanga foleni.

Jamaa wa gari za machame wakawa wanamlalamikia Mengi. Akawaambia siku imetokea tukio kama hilo tena basi wamvutie waya na wasisogeze gari ilipo.


Mwisho wa siku hamadi kibindoni machame ndio inatakiwa iingie mizan gari ya ibra na ibra mwenyewe akiwemo hawa hapa wana force wawahi.

Mengi akavutiwa waya akaja fasta.
Ibra akatoa mashine jamaa aliposhuka kwenye gari yake. Mengi kachomoka na silaha ya kivita.

Ibra akanywea. Akatukanwa kinyama hadi hizi mambo za ndumba kwenye familia yao. Mengi akamwambia kwanza gari zenyewe haziko kwa jina lake. Kama zikko kwa jina yake amletee kadi ya gari atampa coaster mpya.
Ibra alinywea sana.
Adabu akaishika
Hapa umetuingiza chaka.. Mizani ya Himo mpaka Moshi mjini pana km zaid ya 20.. sasa mtu atoke mjini mpaka afiki mizani bado gari zipo mizani...mmmmh
 
Story ya kwamba biashara yake ina ubia au uhusiano na Rizmoko, ilivyoanza, ni kwamba Dr Slaa enzi zile aliibua hiyo issue kuwa kuna vichwa vya Scania(sikumbuki vilikuwa vingapi), ila nadhani mia kadhaa. Dr Slaa alisema kuwa vichwa vile vya Scania ni vya Rizmoko. Sasa wakati watu wanasubiria Riz aende bandarini, badala yake vikatolewa pale na Ngiloi ambaye ndo mwenye hiyo Panone. The rest is history... Kwahiyo watu wakajumlishia kuwa kuibuka kwake kwa ile kasi ni matokeo hayo ya Rizmoko.

Ndo nilivyosikia.
Mwisho wa siku utagundua mali na za Panone mwenyewe coz Lake Oil and gas watu wansema pia ni za rizmoko
 
Kunakipindi konda aliingiwa na tamaa akachukua nauli, wamerudi ofisini Jamaa akamwambia akazitumbukize chooni mwenyewe.MZEE saivi mambo sio mazuri kivile japo anapambana kimtindo Ila saivi ni mwanamziki kazindua album juzi kati
Masihara hayo.
Mziki kabisa??
Anaimba kwa kipare au??
 
Siku hizi nyumba zimejaa vumbi kutani na batini,vijana wanaoza kwa gongo iliyochanganywa na maji.watoto was moshi huwaita MVIMBO.nani aliwafundisha wachaga kuacha utajiri was mila na kukimbilia wa kichawi.Vijana wanateketea.
Inahuzunisha sana
 
Inahuzunisha sana
yaani vijana wanatia huruma hata wale tulioamini wangekuwa mapadri au mashehe wameharibika,mkuu kuna mbabe mmoja pale mto rau alikuwa na miguu kama stendi ya baiskeli aliitwa hamadi vimiguu alikuwa mbabe haswaa nilipomkuta anapigwa makofi na vitoto nikasema kweli gongo sio kitu kizuri.vijana wamekwisha wameoza.
 
Kauchunguzi kangu kadogo nilicho fanya inaonekana members wengi humu ndani ni wachaga, uzi umewekwa Jana ila umefakamiwa na wachaga
Kwa iyo 70% ya members humu ni wachaga???
 
Kumbuka mamaeliza muuza gongo maarufu,baadae akaitwa mama" Eliza msukule."alikuja fufuliwa na mganga was kuitwa yahaya mbwana.
Hahaha umenikumbusha
Mama Eliza punguza uchawi unatumaliza
Watu walijaa makaburi ya njoro kwenda kushuhudia kaburi la Eliza msukule
 
Moshi inahitaji tamthiliya yake mkuu ndefu kama isidingo.
Na kweli kama isidingo
Ila nani wa kuiact?kila mtu anaogopa
Si unaona wana Jf kibao wamekimbia uzi
Wanasoma comments tu
Imagine hadi watoto zao na vitukuu wamo humu
 
Kunakipindi konda aliingiwa na tamaa akachukua nauli, wamerudi ofisini Jamaa akamwambia akazitumbukize chooni mwenyewe.MZEE saivi mambo sio mazuri kivile japo anapambana kimtindo Ila saivi ni mwanamziki kazindua album juzi kati
Hahahah kazindua albam?
Ningekuwa moshi ningefika nimuunge mkono
 
yaani vijana wanatia huruma hata wale tulioamini wangekuwa mapadri au mashehe wameharibika,mkuu kuna mbabe mmoja pale mto rau alikuwa na miguu kama stendi ya baiskeli aliitwa hamadi vimiguu alikuwa mbabe haswaa nilipomkuta anapigwa makofi na vitoto nikasema kweli gongo sio kitu kizuri.vijana wamekwisha wameoza.
Gongo imewamaliza vijana
Sema kuna watu wamejenga kupitia gongo
Kuna wamama nawajua walikuwa wauza gongo,wakatoboa saivi wameokoka
Hahahah
 
Back
Top Bottom