Maswali yalioninyima usingizi nilipokua mtoto

Maswali yalioninyima usingizi nilipokua mtoto

😀 😀 hahahaa kuna watu wanachekesha sana huku..Daah!! utoto raha
 
Mimi niliambiwa hii..eti zeruzeru hawafi wanapaa mbinguni..nikaamini

hili la zeruzeru hata me enzi zangu niliwahi kusikia eti hawafi wanapotea tu! kumbe matatizo na hawa watu yalianza zamani sana!
 
Hivi umasikini huu wa Tanzania mpaka lini?
Shule za tech zinapokuwa za mwisho, hivi kuna mpango wa kuwekeza kwenye sayansi nchi hii?

tunazungumzia ulipokuwa mtoto sasa wewe unaleta sayansi? kama vip muulize mulugo atakujibu!
 
Mimi nlijiuliza ukipanda,mbegu ya mhindi wa kuchoma/kuchesha utaota mhindi wa kuchoma, niule bila kuuchoma?? Nlishajaribu kila nkila mhibdi naacha baadhi naenda kufukia uote
 
mi nilijua lugha ya kiswahili inafundishwa kila nchi duniani kuanzia shule ya msingi kama sisi tunavyojifunza lugha yao
 
Mimi nlijiuliza ukipanda,mbegu ya mhindi wa kuchoma/kuchesha utaota mhindi wa kuchoma, niule bila kuuchoma?? Nlishajaribu kila nkila mhibdi naacha baadhi naenda kufukia uote
hahaha unanikumbusha wakati wa kula chungwa ukila vipeke vyake nilijua vinaweza ota tumboni
 
Nachokumbuka mimi ni baba alimleta fundi rangi home sasa katika stori nikamuuliza fundi rangi ni nani aliyepiga rangi kule juu angani? Daaa fundi akadai ni yeye! Nikamuuliza alipandaje? Kwani alinijibu akaomba nitolewe pale alipokuwa.
(!)mvua ikinyesha huwa ni mito ya mungu imejaa?
 
mi nilikuwa naogopa gari hata kama limepaki nikiona zile taa najua macho pia nlijua gari linaweza kwenda hata bila dereva!
pia nkimwona padri mzungu ndiye mungu!
 
mi.nilikua sielew kwa nini gar liwe na radio na taa wakat hamna nguzo na nyaya za umeme wa tanesco zinazoleta umeme kwenye gar
 
Mimi nlijiuliza ukipanda,mbegu ya mhindi wa kuchoma/kuchesha utaota mhindi wa kuchoma, niule bila kuuchoma?? Nlishajaribu kila nkila mhibdi naacha baadhi naenda kufukia uote

Mie nilisumbuka upande wa samaki niliamini ukifukia mifupa ya samaki ni kama mbegu basi atachepua mmea wa samaki hahahahaha! Watoto huwa wanafikiri sana.
 
mi nilikuwa naogopa gari hata kama limepaki nikiona zile taa najua macho pia nlijua gari linaweza kwenda hata bila dereva!
pia nkimwona padri mzungu ndiye mungu!

Hahahahahaha! Kumbe akili za kitoto zinafanana yaani nakumbuka kwa jirani kulikuwa na isuzu kibunua mchanga dah yaani likiwashwa kama nipo karibu nilikuwa naogopa hakuna mfano make nilzani huwa linajiendesha labda linaweza likaamua kunikimbiza te te te te te!
 
Kumkuta mzee nyumba ya jirani katoa meno ya bandia kaweka kwenye kisahani anakula ugali, mbio mpaka home natweta kusimulia wakubwa kuwa mzee fulani anakula ugali na meno!!!! Walinicheka saaanaaaaaa, pamoja na maelezo yao huo ulikuwa mwisho wa kumzoea yule dingi, akitokea tu mi mbio!!!!
 
Mie nilikuwa nashindwa kutofautisha kati ya kusali na kuomba, unajua kipindi cha nyuma mtoto mwenzio ukimuomba kitu mfano pipi anakuambia kaombe kanisani basi mie nilkuwa natimba kweli mpaka walimu wa sundayschool walinizoea.
 
Nyoya la tausi nililiweka katikati kitabu na kulilisha mabaki ya penseli ili liwe tausi....tukicheza kombolela tukiwa tumejificha ikitokea demu anakojoa kule mafichoni kwenye kombolela mimi na washkaji zangu tulikuwa tunaamini ukichukua nyoya la kuku ukilipaka katika ule mkojo wa demu..lazma yule demu aombe mfanye matusi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom