Maswali yalioninyima usingizi nilipokua mtoto

Maswali yalioninyima usingizi nilipokua mtoto

1. Mimi nilijua watu wakubwa hawanyi hadi nilipomchulia chooni dadangu ambaye alikuwa mjamzito nikamuona anajikamua yaani nilishangaa hadi leo naikumbuka siku hiyo
2. Mtu akifa (mwanamke) hapa atafufuka ulaya akiwa mzung mwanamme anakuwa na maisha mengine
3. Wakubwa hawajambi
4. Mama hana jina
5. Nilikuwa sijui muda (time) kigoma cha taarifa ya habari kikilia kila mtu anaotea hata kama jua kali namna gani mtu anakurupuka (saa moja)
:A S 109:
 
1-Nilikua nikisikia kwene redio kabla ya taarifa ya habari wanasema"ufatao ni muhtasari wake" mi nikawa najua wanasema ufatao ni "MUSA NA ASKARI WAKE".....nimekuja kugundua nilipofika darasa la tatu. 2-Nilikua najua nasoma shule ilikuwafurahisha wazazi,sio wa faida yangu..nimekuja kugundua ni kwa faida yangu baada ya kuanza a level.
 
Mimi nilijuaga mtoto analetwa na meli kubwa, siku ikija basi wazazi wanaenda kuchagua mtoto
 
Hata ili la mvua ya mawe lilikuwa linanichanganya sana, nilijua ni mawe kweli
 
Nakumbuka wakati huo wa utoto tunadanganyana kuwa ukimsema vibaya Nyerere hata ukiwa chumbani yeye anakusikia kwake Msasani, nikawa naamini Nyerere ni mchawi kuliko wachawi wote Tz.

Hahahah! hata sisi 2liamini nyerere ni noma sana dah! kumbe ni binadamu kama sisi 2
 
Mimi kuna vitu vingi. 1. nilikua nikijiuliza hivi nitapataje uhakika kuwa mtu au watu flani wanaendelea kuwepo vile vile kama walivyo wakati siwaangalii. Nilihisi nikiona mtu halafu nigeuke anaweza akawa kabadilika na hayuko vile tena, sasa nitaprove vipi kuwa mama ana baki kuwa mama hata mda ambao simwoni!

Nilikua sipendi kula na nikawa nalazimishwa sana, nikatengeneza idea kua hawa watu labda wanataka ninenenpe ili wanile, maana sikuona faida kwao ni nini ya hadi kunichpa nile eti!

Hahaha ulikuwa mtoto wa ajabu..hadi mama yako ulikuwa humuamini atakukula.siku hizi unaamini watu?
 
Utoto shida et zamani ukiweka sindano au wembe kwenye njia ya treni, tren inaanguka..ila baadaye ikawekewa sumaku ya kuvuta sindano na nyembe!!

Dah aisee hata mimi nimekuwa nikiamini hicho kitu. Lakini cha ajabu mpaka leo kuna kitu bado sina hakika kama ni kweli ama la, eti ukiwa unavuka reli na gari wakati treni inakuja gari itazima katikati. Baada ya comment yako hilo swali limenirudia ghafla.
 
Nilikuwa nikijiuliza mbona Mungu hatokei/haji kuchukua sadaka zake alizotolewa wakati wa ibada?
 
Mimi nilikuwa naamini ukiongea kwa sauti kubwa usiku sana sauti yako inasikiwa na wachawi na kesho yake unakuwa marehemu
 
  1. mimi nilikuwa nikiwaskia big boys wakizungumzia kumkojole msichana, nilikuwa nadhani mkojo huu huu wa kawaida! sasa nikawa najiuliza msichana akishakojolewa, tena kwa wingi wa mkojo, huwa unaenda wapi? matakoni ama tumboni!
  2. mimi nilikuwa naamini, tukisafiri ile miti nayo inasafiri kwa kurudi nyuma!

Hahahahaha! Mie nilkuwa nikisikia shahawa zimemwagika kitandani basi nikadhani hizo shahawa huwa nituunga unga, nilvokuja kujua nilijiona bonge la kiazi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom