Maswali yalioninyima usingizi nilipokua mtoto

Maswali yalioninyima usingizi nilipokua mtoto

Mimi niliteseka na kujua kazini wanafanya kazi gani???!!!
Kama ni hesabu zoezi la ngapi??!!!!
Kama ni sayansi mada gani???!!
Madaftari wanapewa na nani???!!

Wasahishiwa kama sisi shuleni???!!!
Mbona hawavai yunifomu???!!

Yaaani nilidhani kazi ni kusoma, kuandika na kusahishiwa tu maana wanabeba mafaili na mikoba na kila nikichungulia wa mzee naona makabrasha kibao!!!!
 
Mimi sikuwahi kuwa na maswali yasiyo na jibu. Nikijiuliza swali natengeneza na jibu hapo hapo. Nilikuwa najua for sure mimba inapatikana baharini, chini ya mnazi. Mwanamke anasimama anaegemea mnazi, halafu mume anamshika tumbo anamuambia uwe na mimba ya mtoto wa kike. Afu wanarudi nyumbani (sikujua kama kuna kufanya 'matusi')

tetettee zamani hili ndio lilikuwa neno "matusi"
huwa nikitaka kumtania mume wangu namwambia ..............................
ngoja niishie hapo

ila watoto wa siku hizi wanasema mapenzi kwa nini jamani na wanayatamani TV hizi
 
ya kwangu yalikuwa haya:
1. je mtu akifa anapandia wapi kwenda mbinguni?
2.je raisi anakunya?


Haaaaaaah umenchekesha sana aisee mi nilikuwa nadhani Raisi anachukua vitu bure madukani yaani hanunui
 
Mimi niliteseka na kujua kazini wanafanya kazi gani???!!!
Kama ni hesabu zoezi la ngapi??!!!!
Kama ni sayansi mada gani???!!
Madaftari wanapewa na nani???!!

Wasahishiwa kama sisi shuleni???!!!
Mbona hawavai yunifomu???!!

Yaaani nilidhani kazi ni kusoma, kuandika na kusahishiwa tu maana wanabeba mafaili na mikoba na kila nikichungulia wa mzee naona makabrasha kibao!!!!

mm nilikuwa najua manesi na madaktari huwa hawaumwi.
 
Mimi nilijua pembeni ya reli wanaruhusiwa kupita wafanyakaz wa reli tuu na wakikukamata mtu mwingine wanakupa kisago
 
Kumbe wewe ni wa juzi tu wakati wa kizazi cha TV. Mimi niliamini kuwa ndani ya redio wako watu ingawa wana umbile dogo lakini wana uwezo wa kuzungumza. Siku moja kuna mtu alinidanganya kuwa baba yake alifungua redio na ndani walikuwako watu wawili.

hahahaaa et ndani ya redio alikuta watu wawili?? Wat ; wat;
 
Mi nimewahi kumwuliza maza mbele ya masista na mabraza eti mjamzito yupoje! Wote wakabaki midomo wazi. Pale pale nikajua hapa nitakuwa nimetereza tu nikatoka spidi kali sana kwa sababu ilikuwa ukiongea pumba unafinywa balaa.
Siku ya pili nikatengeneza mtu wa udongo mwenye katoto ndani nikaenda kwa sista nikapasua tumbo nikauliza huyu ni mja mzito au ana mimba? We nilipata kichapo.
 
Kuna watu mnacheksha sana duh

..je raisi anaku..nya? Aisee we fikra zako ni kiboko
 
Kwanini mwaka haubadiliki?
Huu mwaka ulikuwa unaniogopesha sana 1998,yaani kila siku tunaandika huo huo mwaka
nikajijibu,lbd utakuwa mwisho wa dunia
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom