Maswali yalioninyima usingizi nilipokua mtoto

Maswali yalioninyima usingizi nilipokua mtoto

Nachokumbuka mimi ni baba alimleta fundi rangi home sasa katika stori nikamuuliza fundi rangi ni nani aliyepiga rangi kule juu angani? Daaa fundi akadai ni yeye! Nikamuuliza alipandaje? Kwani alinijibu akaomba nitolewe pale alipokuwa.
(!)mvua ikinyesha huwa ni mito ya mungu imejaa?

Hehehehhe kaona utamchanganya hehehe
 
Nilichukua ndizi nikaenda kuifukia ili iote tupate ndizi nyingi...nilikuwa naamini ukichimba sana chini unatokea nchi nyingine...
 
nilipokuwa mdogo nilimwambia mom akaniokotee mdogo wangu baharini akawa ananizungusha tu(mi wa mwisho)
2 mbinguni kupoje je kuna nyumba na watu wanaoishi huko
3 nilimwambia mom kwanini asimbadili kaka angu mmoja kuwa dada nina kaka sita afu sina dada kakaangu nilieombwa abadilishwe kuwa dada alinipigaje tena ndo alikuwa anabalehe kipindi hicho mimi nilikuwa la kwanza lol

Namba tatu imenichekesha sana.Like.
 
Nilikuwa sijui kama baba na mama wanasex nilikuja kujua darasa la 5..tena nimewasikia wanafunzi wenzangu wakiongea...niliwaza sana
.nilivorudi nilikuwa nawatizama sana baba na mama...nawashangaaa...dah...nimechelewa sana kujua .nimekuja kujua mwanamke nae anako..joa kwenye sex nikiwa darasa la 7.siku izi chekechea anayajua mambo...tv mbaya sana
 
Mi naishi mkoani wakati mdogo nikisikia MTU anataja Dar-es-salaam picha niliyokuwa naitengeneza kichwani ni kuwa hakuna vumbi wala mchanga ni cement na maghorofa mwanzo mwisho.Ss likizo moja tukapata kachance ka kwenda dar Nilipofika kakaangu ananiambia tushafika aisee ckumuelewa nililia namwambia nataka kwenda dar hapa mbona kuna michanga?
 
Nyoya la tausi nililiweka katikati kitabu na kulilisha mabaki ya penseli ili liwe tausi....tukicheza kombolela tukiwa tumejificha ikitokea demu anakojoa kule mafichoni kwenye kombolela mimi na washkaji zangu tulikuwa tunaamini ukichukua nyoya la kuku ukilipaka katika ule mkojo wa demu..lazma yule demu aombe mfanye matusi

wewe kweli muuza sura!
 
Nilikuwa nikijiuliza mbona Mungu hatokei/haji kuchukua sadaka zake alizotolewa wakati wa ibada?

Hapo sasa mkuu, hili lilinichanganya sana mimi pia wakati wa utoto, mwalimu wetu wa Sunday school alikuwa mama yangu mzazi alikuwa anatuambia hizi Sadaka ni za Mungu nikajua zinaachwa pale then Mungu anakuja kuzichukua pale sisi tukienda nyumbani, sasa nikashangaa siku hiyohiyo jioni kukuta kile chombo cha sadaka nyumbani kwetu nikamwuliza mama Mungu hajachukua sadaka leo? Akasema hapana atachukua kesho lakini kesho yake akapeleka kanisani zile sadaka nikagundua kuwa sadaka ni za wanadamu wala siyo za Mungu(mpaka sasa naamini sadaka za kanisani ni za wachungaji wala siyo za Mungu)
 
Nini haswa kilikua kinachofanya mtu awe amemuoa mwanamke...nilikua naamini kuweka mkono kwenye kwapa ya mwanamke...nikiamini kuoa ni kuweka mkono wako kwapani kwa mwanamke....
 
Nilikua naamini kwenda hospitali ni kuchomwa sindano tu...

Hii umenikumbusha yangu..nikiumwa nikipelekwa hospital nalia sana ila naambiwa nitanunuliwa soda
..then najikazaaa...nikitoka hapo tu nadai soda na keki..nawaringishia wenzangu...DUH KAZI KWELI KWELI SODA MPAKA UUMWE heheheheh

Siku hizi mwanangu kila tukitoka hospital anadai toy mpya sio soda hataki hata kusikia anazinywa kila siku...yeye anadai toy jipya..anamatoy box linajaa..kwa kuwa nataka achome sindano namridhisha...kazi kweli kweli kuwa uyaone
 
Kutakuwa na kufanana kwa imani hizi za utotoni kutoka sehemu moja hadi nyingine, nikiwa mdogo nilikuwa naamini watoto wananunuliwa dukani na pia niliambiwa Shetani anaishi mtoni kwenye migomba flani ambayo haitoi ndizi na kwenye magimbi basi nikawa naogopa kupita maeneo hayo kwa kumwogopa Shetani, nilikuwa naambiwa kwamba MVUA ikiwa inanyesha na RADI inapiga huku JUA likiwaka basi hapo Shetani anampiga mke wake mateke nikaamini hivyo mpaka darasa la tatu, nikawa naona watu wengi wakipiga wake zao mara kwa mara huku nikishuhudia kwa nadra hili suala la Mvua, Radi na Jua nikawa najiuliza, mbona Shetani anapiga mke wake mara moja moja lakini majirani zetu wanapiga wake zao karibia kila siku? Na huku naambiwa Shetani ni mbaya? Tena nilikuwa naamini Shetani ni jitu jeusi halafu Mungu ni mzungu kumbe ni utoto na mafundisho potofu kutoka kwa jamii inayonizunguka, lakini leo siangalii hata hizi filamu zinazoitwa za Yesu maana ni fiksi tu na brainwash
 
Nakumbuka siku niliyoota vuzi nikafikiri nina cancer! sababu bibi alininunulia suruali ya mtumba nilivovaa sikuvua hadi usiku. Nilikua naambiwa vua hio suruali tufue nagoma, kufika usiku nakuta kanywele kameota! Dah! Nikajua ni madhara ya ile nguo ya mtumba!
 
Kuna siku shule nikiwa darasa la pili niliambiwa wanyonya damu wanakuja leo...nilitetemeka mpaka haja ndogo ikaachia kwa woga...hehehehe
 
Kuna baadhi ya mambo yalinifanya niumize akili enzi za uto to
1- mtu akivaa overall (kanyela mumo) anakunyaje?
2-mama akienda kujifungua, je mototo hupitia wapi kutoka tumboni?
3-baba na mama, walizalia pamoja?
4-mwalimu ndie mtu mwenye akili kuliko watu wote?
5-rais ndie mwenye nchi?

Ongezea maswali yalio kutatiza utoton

Nilikuwa najiuliza kwa nini umeme ukikatika gari zinawaka taa.
 
Niliambiwa ukila chakula bila kunawa shetani anakula chakula chako..niliaminiiii sana nilihakikisha nanawa...na usiku wakati wa kulala kama sijaosha miguu shetani analala na mimi ..nilihakikisha nanawa sisahau..KUMBE JANJA YA WAZAZI hehehehe
 
hii threads z the best....yan unajua utoton tunakuwaga na maswali kbao yanabaki kutuumiza kichwa tu.
......nakumbuka sijaanza chekechea basi naachwa nyumban na mdogo wangu mimuangalie, mama angu na dada na kaka walienda shamba.....sasa ikapita ndege inapima sijui madini au inafanya maping na kakifaa fulan kananing'ia chini...jaman nilikimbia kama kichaaa kwan nilijua ule ndo mwisho wa dunia...nikawa najiuliza hii ndege hapa kijijin imetokea wapi? afu kwa nn inaenda hadi milima ya kule inarudi hadi upande mwingne....nikajua hii inanitafta mm inazuga tu.aliniokoa baba wa jiran huko njian akanishikilia had wazazi walivorudi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom