Maswali yalioninyima usingizi nilipokua mtoto

Maswali yalioninyima usingizi nilipokua mtoto

Mi nlikua najiuliza mtu akituma hela mpesa inamfikia je mtu mwingine aliye mbali ile hela inapita wapi yani we acha tu.
 
hii threads z the best....yan unajua utoton tunakuwaga na maswali kbao yanabaki kutuumiza kichwa tu.
......nakumbuka sijaanza chekechea basi naachwa nyumban na mdogo wangu mimuangalie, mama angu na dada na kaka walienda shamba.....sasa ikapita ndege inapima sijui madini au inafanya maping na kakifaa fulan kananing'ia chini...jaman nilikimbia kama kichaaa kwan nilijua ule ndo mwisho wa dunia...nikawa najiuliza hii ndege hapa kijijin imetokea wapi? afu kwa nn inaenda hadi milima ya kule inarudi hadi upande mwingne....nikajua hii inanitafta mm inazuga tu.aliniokoa baba wa jiran huko njian akanishikilia had wazazi walivorudi.

Ha ha ha ha ha hahhahahaahhahahahhahahahahaahahahhahahaha..iliwahi nitokea hii mwanzoni miaka ya 2000 ile midege ya jeshi..dahh
 
Kuna baadhi ya mambo yalinifanya niumize akili enzi za uto to
1- mtu akivaa overall (kanyela mumo) anakunyaje?
2-mama akienda kujifungua, je mototo hupitia wapi kutoka tumboni?
3-baba na mama, walizalia pamoja?
4-mwalimu ndie mtu mwenye akili kuliko watu wote?
5-rais ndie mwenye nchi?

Ongezea maswali yalio kutatiza utoton

Hahahahah kweli utoto raha sana
 
haya magari yamenisumbua sana
1. dereva anawezaje kuwasha indicator huku akiendesha gari (washa zima washa zima)
2. utakuta home umeme umekatika alaf linapita gari na taa zake zinawaka.
 
Nilikuwa nawaza sana nikisikia mtu amekula hela,,
najiuliza amekulaje zile noti au sarafu? Anazitafuna?
 
Mimi kilichonipa utata ni hichi hapa na mpaka leo bado nashangaa tu.

Sensual Paradise[ edit ]
In Islam, the concept of
72 virgins (houri) refers
to an aspect of Jannah
(Paradise). This concept
is grounded in Qur'anic
text which describe a
sensual Paradise where
believing men are
rewarded by being wed
[1] to virgins with "full
grown", "swelling" or
"pears-shaped" breasts.
[2][3] Conversly, women
will be provided with
only one man, and they
"will be satisfied with
him".

hizo ni fikra potofu mabikra 72?? Pasua kichwa kweli kweli
 
nilikuwa najua shetani ana sura mbaya..nikiambiwa shetani uyo anakuja nalia natoka nduki then najificha!

Hapo kwenye "shetani" replace na sindbadi, home palikuwa hapatoshi ikibidi na msosi nasamehe kabisa. Nilikuwa namuogopa sindbadi aibuuuuu!!!!
We acha tu.
 
Mi mwanangu wa miaka 5 huwa ananiuliza 'hivi baba na wewe ulikuwaga mtoto kama mimi',basi nikamuonyesha picha yangu nilivyokuwa mtoto kabla sijaanza hata kutambaa lakini nakaa,alitoa macho kwa mshangao sana,sasa huwa najiliza hivi yeye huwa ananichukuliaje,kwamba nilizuka tu kama mzuka au la
 
Baba alinunuaga viatu flani kama vya Kungfu nikaviiba kupeleka kwa fundi avipunguze nivivae mimi fundi akasema haiwezekani.

Niliwahi kuchukua saa ya baba nikaivaa mguuni kwa sababu mkononi ilikuwa haitoshi (inapwaya).

Niliwahi kuweka maji kwenye kibatari nikidhani itakuwa kama mafuta ya taa.

Wewe lazima ulikuwa kipanga!!
 
Mi naishi mkoani wakati mdogo nikisikia MTU anataja Dar-es-salaam picha niliyokuwa naitengeneza kichwani ni kuwa hakuna vumbi wala mchanga ni cement na maghorofa mwanzo mwisho.Ss likizo moja tukapata kachance ka kwenda dar Nilipofika kakaangu ananiambia tushafika aisee ckumuelewa nililia namwambia nataka kwenda dar hapa mbona kuna michanga?

Hako ka picha ka daslam wengi kanawachanganya. Hii hadi watu wazima ndivyo wanavyofikiri.
 
nikiwa darasa la tatu mama akiwa amekaa na wamama wenzie nilimsikia akisema siku hizi wanatumia MIPIRA kuzuia UKIMWI. baada ya mama kugundua kuwa niko eneo hilo alinifukuza nakunifokea kwa nini nasikiliza maongeza ya watu wazima. Nilipotoka hapo nilijiuliza saaaaaana, hiyo mipira wanayotumia kuzuia ukimwi ni ipi, ni kama hizi za manati tunayotumia kuwindia ndege? ni mipira/mirija inayotumiwa hospitalini, au ni mipira yaani kama mpira wa miguu(football) yaani gozi tunalosakata kabumbu. hilo swali lilinitesa sana
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom